Dhana dhanifu juu ya kutekwa Mo Dewji

Dhana dhanifu juu ya kutekwa Mo Dewji

Moderator huu ni uchambuzi wa viashiria mbalimbali na uhalisia wa tukio baada ya Mo kutekwa hivyo naomba msiunganishe huu uzi na zile nyingine zinazoripoti

Habari huanza kama tetesi ama uvumi hilo limekwisha fanyika
Baada ya tetesi ama uvumi kuthibitika ni kweli habari husika hukoma kuwa tetesi ama uvumi.

Kinachofuata baada ya hapo ni breaking news hapa kila mtu huongea lake la masikitiko la majonzi la huruma nknk....tuko kwenye hatua hii kwa sasa

Vumbi likishatulia ndio uchambuzi huanza..na sasa ni muda wa uchambuzi na sio tetesi wala breaking news tena!

MO KATEKWA! ndio habari kubwa kwa asubuhi hii ya tarehe 11.October.2018
Kila tuko linalotokea huwa na mlolongo huu
Wazo
Sababu
Mchoro/mpango
Muda
Wahusika
Vitendea kazi
Bajeti
Uchaguzi wa eneo la tukio
Nani afanye nini nknk

Matukio ya utekaji huambatana na
Visasi
Fidia
Vita ya kibiashara
Mambo ya kisiasa
Mapenzi na mahusiano...nknk

Kutekwa si jambo geni masikioni mwetu ,wengi walishatekwa ....wachache wkapatikana wakiwa hai na wengine wafu....wengine hawakupatikana tena.

Kwanini MO?
Huyu si mtu mdogo ni mfanyabiashara mkubwa mwenye mafanikio mengi...amewahi kuingia kwenye kumi bora na ishirini bora za matajiri vijana duniani, Afrika na hata katika mgawanyo wa kikanda... Kumteka huyu maandalizi yake si ya kitoto
Wiki moja Kabla nilimuona akifanya mahojiano na mwandishi mmoja ..sikumbuki ni kituo gani cha luninga ...lakini katika mahojiano yale alitaja mafanikio yake mengi na pia kuelezea ratiba yake ya siku nzima na wiki pia
Kwa maneno yake mwenyewe hii ndio ratiba yake

Anafika ofisini saa 12 asubuhi na kuanza kusoma na kujibu emails mpaka saa mbili asubuhi
Baada ya hapo hujipanga kuingia kwenye vikao vya bodi mbalimbali kuhusiana na makampuni yake.

Akimaliza kwenye saa sita nadhani hupata wasaa wa kupitia magazeti mbalimbi,kupumzika na ikifika saa nane HUENDA GYM kupata lunch na baadae kurudi ofsini mpaka usiku...weekend hukutana na marafiki na hupata muda wa kuwa na familia pia.

Leo alfajiri katekwa akienda/akitoka gym! Ni wazi kwenye yale mahojiano alidanganya kuwa anaendaga gym mchana...hii haina shida ni mbinu shirikishi ya kujilinda

Je, watekaji wanataka nini kwake?

Ni wazi hawana nia ya kumdhuru la sivyo wangeshamaliza mchezo pale pale walipomtekea.

Kwa jicho la haraka hawa wanataka fidia (ransom )na kama hili likithibitika basi tutakuwa tumeingia kwenye zama mpya mbaya sana kiuchumi na swala zima la uwekezaji....

Je kwasasa yuko wapi?
Its a million dollar question...lakini watekaji ni watu waliojiandaa hasa...eneo walilomtekea lina ulinzi wa kampuni binafsi ya ulinzi yenye vifaa vya uhakika lakini pia kuna CCTV CAMERAS...hivyo basi walijua wanachokifanya na hata kuruhusu waonekane kama ni wazungu ni cover up nyingine...siku hizi kuna vinyago vya kila aina.

Kiinteligensia Dar ni padogo sana na eneo letu la bahari liko huru mno...ni rahisi mno kutega speed boat ufukweni maeneo ya Coco na kuondoka na mtu salama salimini...

Neno la Makonda
Kwa kawaida baada ya mtu kutekwa watu husubiri masaa24 kusikia watekaji watasema nini...kipindi hiki cha mpito mamlaka husika hukaa kimya kabisa zikifuatilia kwa Karin kila taarifa...sanasana zitatoa tu taarifa kuthibitisha tetesi...huwa hazikurupuki kupayuka!

Ndugu yetu huyu kwa nafasi yake ya mkuu wa mkoa kasema WALE WAZUNGU NI WAGENI!
Kajuaje kama ni wazungu kweli
Kajuaje kama ni wageni!?
Ana taarifa zao?
Wamekamatwa?
Kwa kupayuka huku mtu anaweza kuharibu kila kitu ama kugeuka na kuwa chanzo cha habari na kuacha mashaka mengi.....

Mpaka kinachosemwa ni Mo katekwa na majambazi...lakini bado hatuna hakika kwa asilimia zote ninini hasa kimetokea....wakati tukiendelea na huu mjadala tuwe makini na kauli zetu,tusije tukajikuta ni sehemu ya ushahidi..

Tumuombee...tuiombee familia yake ndugu jamaa na marafiki katika kipindi hiki kigumu cha sintofahamu kubwa


Keshasema amenukuliwa vibaya, kwa hiyo wanaopotosha watengue walichosema...

viongozi wengi wa tanzania ni wajinga na wanapenda sifa sana bila kuangalia madhara ya wanachokikurupukia.
 
Keshasema amenukuliwa vibaya, kwa hiyo wanaopotosha watengue walichosema...

viongozi wengi wa tanzania ni wajinga na wanapenda sifa sana bila kuangalia madhara ya wanachokikurupukia.
maneno ni kama risasi...haina rivasi..ikitoka Imetoka...apambane tu na hali yake sasa
 
awamu ya tano jamani haya matukio yamekuwa mengi sana
mkuu hii analysis ni ya kiinteligensia
 
Mkuu Mshana Junior kwani ukitumia ile darubini yetu ya kichawi bado hujafanikiwa kupata leads kuhusu tukio zima.

Maana hapa umechambua kiintelijensia zaidi. Sasa naomba kidogo turudi kwenye ulimwengu wa roho.

Bado hujang'amua au mizimu bado imelala?
 
Ninavyoga post humu kwamba watu wengi huongea kwanza kisha akili hufuata watu wengi huwa hawanielewi
 
Ninavyoga post humu kwamba watu wengi huongea kwanza kisha akili hufuata watu wengi huwa hawanielewi
 
Mm nachojiuliza n kwamba iweje tajiri mkubwa kama Mo aishi bila kuwa na ulinzi wa bodyguard,?? Inamaana anajichukulia kawaida ,sawa na sisi makabwela au walinzi wake walishindwa kuwakabili watekaji???
Ifikie kipindi watu wajue kuwa utajiri huja na kutokuwa free na kufanya upendalo maana wanaokuwinda ni wengi....tajiri kama Mo yafaa awe na walinzi binafsi kama alivyo Mayweather na sio kukaa kiboyaboya tu et anapiga jogging asubuh akiwa mwenyewe....next time watamfyekelea mbaliiiiiiii
Hata mzee Mengi sijawahi kumuona ana ulinzi. Mimi nashauri vyombo vyaulinzi na usalama wawashauri watu hawa wawe na ulinzi. Unajua mtu asiyekuwa na makuu akijaliwa kupata pesa, yeye kawaida yake anaendelea kujiona yuko sawa tu na wengine, na anaendelea kuishi maisha simple tu kama alivyokuwa anaishi kabla hajawa na hela. Hiki kitu ni kizuri sana lakini sasa inabidi wakumbuke pia kuwa ukishakuwa na pesa nyingi macho mengi yanaelekezwa kwako, baadhi yake yakiwa ni yale yasiyokuwa na nia njema. Tafadhali hawa watu nashauri waweze kufanya mpango wa kuwa na Ulinzi
 
Sijui kwanini huwa wanakosea kumpa Makonda nafasi ya kutolea ufafanuzi jambo kama hili ,huwa lazima aache maswali nyuma ya kauli zake ...

Ni mapema kuhukumu ila tayari kuna sketch zinazo onyesha uhalisia wa jambo hili

Anyway "Wakiwamaliza wale watawageukia ninyi " hakuna aliye salama. Ni akina nani hao mimi na wewe hatujui ila kuna siku hata mawe yatapaza sauti .
 
Kusema kweli kwenye masuala ya majanga na namna ya kuyasimamia tuko very Poor! Na hapa ndipo Jeshi letu linafaa kupigwa msasa!
Huu mwendo wa kuwa na majbu ndani ya masaa machache siyo afya hata Kidogo. Jingine kazi ya kusemea haya mambo inafaa iachwe kwa wataalamu kwa muda wa kutosha kupata tafakuri ya kitaalamu kabla ya kuja mbele ya wanahabari .
 
Back
Top Bottom