Dhana dhanifu juu ya kutekwa Mo Dewji

Dhana dhanifu juu ya kutekwa Mo Dewji

giphy.gif
 
Moderator huu ni uchambuzi wa viashiria mbalimbali na uhalisia wa tukio baada ya Mo kutekwa hivyo naomba msiunganishe huu uzi na zile nyingine zinazoripoti

Habari huanza kama tetesi ama uvumi...hilo limekwisha fanyika
Baada ya tetesi ama uvumi kuthibitika ni kweli habari husika hukoma kuwa tetesi ama uvumi....
Kinachofuata baada ya hapo ni breaking news ...hapa kila mtu huongea lake la masikitiko la majonzi la huruma nknk....tuko kwenye hatua hii kwa sasa
Vumbi likishatulia ndio uchambuzi huanza..na sasa ni muda wa uchambuzi na sio tetesi wala breaking news tena!

MO KATEKWA! ndio habari kubwa kwa asubuhi hii ya tarehe 11.October.2018
Kila tuko linalotokea huwa na mlolongo huu
Wazo
Sababu
Mchoro/mpango
Muda
Wahusika
Vitendea kazi
Bajeti
Uchaguzi wa eneo la tukio
Nani afanye nini nknk

Matukio ya utekaji huambatana na
Visasi
Fidia
Vita ya kibiashara
Mambo ya kisiasa
Mapenzi na mahusiano...nknk

Kutekwa si jambo geni masikioni mwetu ,wengi walishatekwa ....wachache wkapatikana wakiwa hai na wengine wafu....wengine hawakupatikana tena.....
Kwanini MO?
Huyu si mtu mdogo ni mfanyabiashara mkubwa mwenye mafanikio mengi...amewahi kuingia kwenye kumi bora na ishirini bora za matajiri vijana duniani, Afrika na hata katika mgawanyo wa kikanda... Kumteka huyu ...maandalizi yake si ya kitoto
Wiki moja Kabla nilimuona akifanya mahojiano na mwandishi mmoja ..sikumbuki ni kituo gani cha luninga ...lakini katika mahojiano yale alitaja mafanikio yake mengi na pia kuelezea ratiba yake ya siku nzima na wiki pia
Kwa maneno yake mwenyewe hii ndio ratiba yake
Anafika ofisini saa 12 asubuhi na kuanza kusoma na kujibu emails mpaka saa mbili asubuhi
Baada ya hapo hujipanga kuingia kwenye vikao vya bodi mbalimbali kuhusiana na makampuni yake...
Akimaliza kwenye saa sita nadhani hupata wasaa wa kupitia magazeti mbalimbi,kupumzika na ikifika saa nane HUENDA GYM... kupata lunch na baadae kurudi ofsini mpaka usiku...weekend hukutana na marafiki na hupata muda wa kuwa na familia pia....

Leo alfajiri katekwa akienda/akitoka gym! Ni wazi kwenye yale mahojiano alidanganya kuwa anaendaga gym mchana...hii haina shida ni mbinu shirikishi ya kujilinda

Je watekaji wanataka nini kwake?
Ni wazi hawana nia ya kumdhuru la sivyo wangeshamaliza mchezo pale pale walipomtekea...
Kwa jicho la haraka hawa wanataka fidia (ransom )na kama hili likithibitika basi tutakuwa tumeingia kwenye zama mpya mbaya sana kiuchumi na swala zima la uwekezaji....

Je kwasasa yuko wapi?
Its a million dollar question...lakini watekaji ni watu waliojiandaa hasa...eneo walilomtekea lina ulinzi wa kampuni binafsi ya ulinzi yenye vifaa vya uhakika lakini pia kuna CCTV CAMERAS...hivyo basi walijua wanachokifanya na hata kuruhusu waonekane kama ni wazungu ni cover up nyingine...siku hizi kuna vinyago vya kila aina...
Kiinteligensia Dar ni padogo sana na eneo letu la bahari liko huru mno...ni rahisi mno kutega speed boat ufukweni maeneo ya Coco na kuondoka na mtu salama salimini...

Neno la Makonda
Kwa kawaida baada ya mtu kutekwa watu husubiri masaa24 kusikia watekaji watasema nini...kipindi hiki cha mpito mamlaka husika hukaa kimya kabisa zikifuatilia kwa Karin kila taarifa...sanasana zitatoa tu taarifa kuthibitisha tetesi...huwa hazikurupuki kupayuka!
Ndugu yetu huyu kwa nafasi yake ya mkuu wa mkoa kasema WALE WAZUNGU NI WAGENI!
Kajuaje kama ni wazungu kweli
Kajuaje kama ni wageni!?
Ana taarifa zao?
Wamekamatwa?
Kwa kupayuka huku mtu anaweza kuharibu kila kitu ama kugeuka na kuwa chanzo cha habari na kuacha mashaka mengi.....

Mpaka kinachosemwa ni Mo katekwa na majambazi...lakini bado hatuna hakika kwa asilimia zote ninini hasa kimetokea....wakati tukiendelea na huu mjadala tuwe makini na kauli zetu,tusije tukajikuta ni sehemu ya ushahidi..

Tumuombee...tuiombee familia yake ndugu jamaa na marafiki katika kipindi hiki kigumu cha sintofahamu kubwa
Dhana yako dhanifu imekaa kichochezi..inaonesha kama unataka kushutumu mtu fulani..
maswali uliyo ya bold yamefuata baada ya maelezo ya RC.. kuwa muwazi tuuh unataka kumshutumu mtu fulani au?.
 
Mimi najiuliza tu huyu Makonda huwa anapata je taarifa za haraka za watekaji?

Kipindi cha Roma, aliahidi siku mbili atapatikana na ikawa hivyo. Leo hili la Mo, keshawajua watekaji.

Kama Makonda si mhusika, basi anaujua mtandao wa wahalifu hawa.
Huyu anaweza kuisaidia sana polisi kwa kuanzia.
 
This is fast n furious....! Coco beach again ....what a coincidence!!!View attachment 894225


Brother Mshana Jr ... hii ni picha la kuchongwa..... MO anaweza akawa hausiki kwenye kuiandaa hii movie.

Mbili ni indicator kwa wengine kwamba mtu yoyote akileta fyoko fyoko kuna uwezo wa kupotezwa haijalishi uwezo wako au pesa au utajiri.

Tatu Mungu anajua yote, maana yupo ana wacheki tu... na hata walio fanya hilo tukio kuna kila dalili ni ma proffesion sio vilaza, lile eneo lina TISS wa kutosha
 
Mkuu unafanya kazi Polisi mana ulivyotiririka nadhani kwa nadharia hizo hapo ni kama umebobea sana kwa analysis hizi nadhani kwa muda huu ni vyema Polisi au vyombo vikatulia na kuwa makini kutoa taarifa mana taarifa changanyi huvuruga upepelelezi. tunaamani watu hawa watajulikana
 
Dhana yako dhanifu imekaa kichochezi..inaonesha kama unataka kushutumu mtu fulani..
maswali uliyo ya bold yamefuata baada ya maelezo ya RC.. kuwa muwazi tuuh unataka kumshutumu mtu fulani au?.
Vipi utakata kumrithi shehe Yahaya nini?
 
Moderator huu ni uchambuzi wa viashiria mbalimbali na uhalisia wa tukio baada ya Mo kutekwa hivyo naomba msiunganishe huu uzi na zile nyingine zinazoripoti

Habari huanza kama tetesi ama uvumi hilo limekwisha fanyika
Baada ya tetesi ama uvumi kuthibitika ni kweli habari husika hukoma kuwa tetesi ama uvumi.

Kinachofuata baada ya hapo ni breaking news hapa kila mtu huongea lake la masikitiko la majonzi la huruma nknk....tuko kwenye hatua hii kwa sasa

Vumbi likishatulia ndio uchambuzi huanza..na sasa ni muda wa uchambuzi na sio tetesi wala breaking news tena!

MO KATEKWA! ndio habari kubwa kwa asubuhi hii ya tarehe 11.October.2018
Kila tuko linalotokea huwa na mlolongo huu
Wazo
Sababu
Mchoro/mpango
Muda
Wahusika
Vitendea kazi
Bajeti
Uchaguzi wa eneo la tukio
Nani afanye nini nknk

Matukio ya utekaji huambatana na
Visasi
Fidia
Vita ya kibiashara
Mambo ya kisiasa
Mapenzi na mahusiano...nknk

Kutekwa si jambo geni masikioni mwetu ,wengi walishatekwa ....wachache wkapatikana wakiwa hai na wengine wafu....wengine hawakupatikana tena.

Kwanini MO?
Huyu si mtu mdogo ni mfanyabiashara mkubwa mwenye mafanikio mengi...amewahi kuingia kwenye kumi bora na ishirini bora za matajiri vijana duniani, Afrika na hata katika mgawanyo wa kikanda... Kumteka huyu maandalizi yake si ya kitoto
Wiki moja Kabla nilimuona akifanya mahojiano na mwandishi mmoja ..sikumbuki ni kituo gani cha luninga ...lakini katika mahojiano yale alitaja mafanikio yake mengi na pia kuelezea ratiba yake ya siku nzima na wiki pia
Kwa maneno yake mwenyewe hii ndio ratiba yake

Anafika ofisini saa 12 asubuhi na kuanza kusoma na kujibu emails mpaka saa mbili asubuhi
Baada ya hapo hujipanga kuingia kwenye vikao vya bodi mbalimbali kuhusiana na makampuni yake.

Akimaliza kwenye saa sita nadhani hupata wasaa wa kupitia magazeti mbalimbi,kupumzika na ikifika saa nane HUENDA GYM kupata lunch na baadae kurudi ofsini mpaka usiku...weekend hukutana na marafiki na hupata muda wa kuwa na familia pia.

Leo alfajiri katekwa akienda/akitoka gym! Ni wazi kwenye yale mahojiano alidanganya kuwa anaendaga gym mchana...hii haina shida ni mbinu shirikishi ya kujilinda

Je, watekaji wanataka nini kwake?

Ni wazi hawana nia ya kumdhuru la sivyo wangeshamaliza mchezo pale pale walipomtekea.

Kwa jicho la haraka hawa wanataka fidia (ransom )na kama hili likithibitika basi tutakuwa tumeingia kwenye zama mpya mbaya sana kiuchumi na swala zima la uwekezaji....

Je kwasasa yuko wapi?
Its a million dollar question...lakini watekaji ni watu waliojiandaa hasa...eneo walilomtekea lina ulinzi wa kampuni binafsi ya ulinzi yenye vifaa vya uhakika lakini pia kuna CCTV CAMERAS...hivyo basi walijua wanachokifanya na hata kuruhusu waonekane kama ni wazungu ni cover up nyingine...siku hizi kuna vinyago vya kila aina.

Kiinteligensia Dar ni padogo sana na eneo letu la bahari liko huru mno...ni rahisi mno kutega speed boat ufukweni maeneo ya Coco na kuondoka na mtu salama salimini...

Neno la Makonda
Kwa kawaida baada ya mtu kutekwa watu husubiri masaa24 kusikia watekaji watasema nini...kipindi hiki cha mpito mamlaka husika hukaa kimya kabisa zikifuatilia kwa Karin kila taarifa...sanasana zitatoa tu taarifa kuthibitisha tetesi...huwa hazikurupuki kupayuka!

Ndugu yetu huyu kwa nafasi yake ya mkuu wa mkoa kasema WALE WAZUNGU NI WAGENI!
Kajuaje kama ni wazungu kweli
Kajuaje kama ni wageni!?
Ana taarifa zao?
Wamekamatwa?
Kwa kupayuka huku mtu anaweza kuharibu kila kitu ama kugeuka na kuwa chanzo cha habari na kuacha mashaka mengi.....

Mpaka kinachosemwa ni Mo katekwa na majambazi...lakini bado hatuna hakika kwa asilimia zote ninini hasa kimetokea....wakati tukiendelea na huu mjadala tuwe makini na kauli zetu,tusije tukajikuta ni sehemu ya ushahidi..

Tumuombee...tuiombee familia yake ndugu jamaa na marafiki katika kipindi hiki kigumu cha sintofahamu kubwa
usimuongelee mtu asiejua hata jinalake halisi
 
Moderator huu ni uchambuzi wa viashiria mbalimbali na uhalisia wa tukio baada ya Mo kutekwa hivyo naomba msiunganishe huu uzi na zile nyingine zinazoripoti

Habari huanza kama tetesi ama uvumi hilo limekwisha fanyika
Baada ya tetesi ama uvumi kuthibitika ni kweli habari husika hukoma kuwa tetesi ama uvumi.

Kinachofuata baada ya hapo ni breaking news hapa kila mtu huongea lake la masikitiko la majonzi la huruma nknk....tuko kwenye hatua hii kwa sasa

Vumbi likishatulia ndio uchambuzi huanza..na sasa ni muda wa uchambuzi na sio tetesi wala breaking news tena!

MO KATEKWA! ndio habari kubwa kwa asubuhi hii ya tarehe 11.October.2018
Kila tuko linalotokea huwa na mlolongo huu
Wazo
Sababu
Mchoro/mpango
Muda
Wahusika
Vitendea kazi
Bajeti
Uchaguzi wa eneo la tukio
Nani afanye nini nknk

Matukio ya utekaji huambatana na
Visasi
Fidia
Vita ya kibiashara
Mambo ya kisiasa
Mapenzi na mahusiano...nknk

Kutekwa si jambo geni masikioni mwetu ,wengi walishatekwa ....wachache wkapatikana wakiwa hai na wengine wafu....wengine hawakupatikana tena.

Kwanini MO?
Huyu si mtu mdogo ni mfanyabiashara mkubwa mwenye mafanikio mengi...amewahi kuingia kwenye kumi bora na ishirini bora za matajiri vijana duniani, Afrika na hata katika mgawanyo wa kikanda... Kumteka huyu maandalizi yake si ya kitoto
Wiki moja Kabla nilimuona akifanya mahojiano na mwandishi mmoja ..sikumbuki ni kituo gani cha luninga ...lakini katika mahojiano yale alitaja mafanikio yake mengi na pia kuelezea ratiba yake ya siku nzima na wiki pia
Kwa maneno yake mwenyewe hii ndio ratiba yake

Anafika ofisini saa 12 asubuhi na kuanza kusoma na kujibu emails mpaka saa mbili asubuhi
Baada ya hapo hujipanga kuingia kwenye vikao vya bodi mbalimbali kuhusiana na makampuni yake.

Akimaliza kwenye saa sita nadhani hupata wasaa wa kupitia magazeti mbalimbi,kupumzika na ikifika saa nane HUENDA GYM kupata lunch na baadae kurudi ofsini mpaka usiku...weekend hukutana na marafiki na hupata muda wa kuwa na familia pia.

Leo alfajiri katekwa akienda/akitoka gym! Ni wazi kwenye yale mahojiano alidanganya kuwa anaendaga gym mchana...hii haina shida ni mbinu shirikishi ya kujilinda

Je, watekaji wanataka nini kwake?

Ni wazi hawana nia ya kumdhuru la sivyo wangeshamaliza mchezo pale pale walipomtekea.

Kwa jicho la haraka hawa wanataka fidia (ransom )na kama hili likithibitika basi tutakuwa tumeingia kwenye zama mpya mbaya sana kiuchumi na swala zima la uwekezaji....

Je kwasasa yuko wapi?
Its a million dollar question...lakini watekaji ni watu waliojiandaa hasa...eneo walilomtekea lina ulinzi wa kampuni binafsi ya ulinzi yenye vifaa vya uhakika lakini pia kuna CCTV CAMERAS...hivyo basi walijua wanachokifanya na hata kuruhusu waonekane kama ni wazungu ni cover up nyingine...siku hizi kuna vinyago vya kila aina.

Kiinteligensia Dar ni padogo sana na eneo letu la bahari liko huru mno...ni rahisi mno kutega speed boat ufukweni maeneo ya Coco na kuondoka na mtu salama salimini...

Neno la Makonda
Kwa kawaida baada ya mtu kutekwa watu husubiri masaa24 kusikia watekaji watasema nini...kipindi hiki cha mpito mamlaka husika hukaa kimya kabisa zikifuatilia kwa Karin kila taarifa...sanasana zitatoa tu taarifa kuthibitisha tetesi...huwa hazikurupuki kupayuka!

Ndugu yetu huyu kwa nafasi yake ya mkuu wa mkoa kasema WALE WAZUNGU NI WAGENI!
Kajuaje kama ni wazungu kweli
Kajuaje kama ni wageni!?
Ana taarifa zao?
Wamekamatwa?
Kwa kupayuka huku mtu anaweza kuharibu kila kitu ama kugeuka na kuwa chanzo cha habari na kuacha mashaka mengi.....

Mpaka kinachosemwa ni Mo katekwa na majambazi...lakini bado hatuna hakika kwa asilimia zote ninini hasa kimetokea....wakati tukiendelea na huu mjadala tuwe makini na kauli zetu,tusije tukajikuta ni sehemu ya ushahidi..

Tumuombee...tuiombee familia yake ndugu jamaa na marafiki katika kipindi hiki kigumu cha sintofahamu kubwa
mkuu huu uchambuzi unanitia shaka pengine na wewe ni wale wale au muasi???
uchambuzi upo ki professionally...good
 
Back
Top Bottom