Mkuu Heri lee,
Kuna vitu hivi yakupasa uvitambue maana zake;-
(1) kukufuru ni neno linalo patikana kwa asili katika lugha za Semitic kama kiarabu, kiebrania, kiarmaic, nk, na maana yake ni kupinga au kukataa jambo au kumkataa mtu nk.
(2) Roho mtakatifu;- ni nguvu za utendaji wa Mungu, yaani Mungu anapotaka kufanya jambo lolote daima dawamu hutumia roho mtakatifu kwa lugha nyingine roho mtakatifu ni nguvu inayobebwa na malaika wa Mungu na ndiye yule Malaika aliyemtokea bikira Maria kumpasha habari ya kuzaliwa yesu.
(3) Kumkufuru yesu maana yake ni:- kumkataa au kumpinga yesu.
(4) kumkufuru roho mtakatifu maana yake ni:- kukataa/kupinga nguvu za utendaji za Mungu, sasa ukipinga nguvu za Mungu maana yake moja kwa moja umempinga Mungu na hapo hutasamehewa katika ulimwengu huu na ule ujao.
👆🏻Hapo Yesu alikuwa anawaambia Wana waisrael ambaye yeye alikuwa ni mtume wao (mathayo 12:24).