Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,877
- 2,756
Nimesoma leo Mwanahalisi la jana na miongoni mwa habari zake ni zinazohusiana na madini. Kichwa kimoja kikinadi "Dhahabu ya damu Bulyanhulu". Kingine kikinadi "Usiri hatari migodini". Hizi habari mbili zinasikitisha sana. Moja (ya awali) inahusu jinsi wachimbaji walivyofukiwa wakiwa hai migodini huku serikali ikihusika katika mauaji hayo. Ya pili ikihusu wizi wa mchana wa madini katika migodi yetu iliyoko maporini huko Bukombe kwa kisingizio eti bado utafiti unaendelea. Miaka 8!
Waliosoma mwanahalisi wana picha halisi. Suala ni kwamba, kwa nini serikali inatufanyia hivi? Kwa nini serikali inahujumu wananchi kwa kushirikiana na hawa wawekezaji? Naona Ngeleja anahangaika na Dowans tu. Au ndio janja ya mafisadi kuhamishia hoja kwenye umeme na kuacha madini yapotee? Hii kiukweli inaumiza sana. Hatukupewa rasilimali ili zitutese. Au ndio laana ya baraka?
JK kama kweli unataka kuacha ukumbusho kwa taifa hili, shughulikia kilio hiki cha hawa wananchi walio pembezoni wanaotaabika kutokana na baraka waliyojaaliwa. Rasilimali tulizojaaliwa isiwe angamizo letu. Matendo sasa yafanyike
Waliosoma mwanahalisi wana picha halisi. Suala ni kwamba, kwa nini serikali inatufanyia hivi? Kwa nini serikali inahujumu wananchi kwa kushirikiana na hawa wawekezaji? Naona Ngeleja anahangaika na Dowans tu. Au ndio janja ya mafisadi kuhamishia hoja kwenye umeme na kuacha madini yapotee? Hii kiukweli inaumiza sana. Hatukupewa rasilimali ili zitutese. Au ndio laana ya baraka?
JK kama kweli unataka kuacha ukumbusho kwa taifa hili, shughulikia kilio hiki cha hawa wananchi walio pembezoni wanaotaabika kutokana na baraka waliyojaaliwa. Rasilimali tulizojaaliwa isiwe angamizo letu. Matendo sasa yafanyike