Semilong
JF-Expert Member
- Mar 5, 2009
- 1,712
- 219
Wadosi 3...Samily Hassan,Nuzalt Hassan,Hassan Hassan na Faidh Abdulasuri..wakazi wa Kijiji cha Ihamila Ihanga, Tarafa ya Rujewa, wilayani Mbarali wanashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kumuua mwanafunzi wa kidato cha nne, Swaibu Moshi kwa madai ya kumkuta akiiba mapera.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya,alisema hao watuhumiwa wakiwa na mkoko wenye namba T 496 ALF Toyota Land Cruiser, waliwakuta katika shamba lao wanafunzi wawili, Salum Hamis na marehemu Moshi na kuwakamata kisha kuwaingiza katika gari hilo na kuondoka nao.
Baada ya kuona hivyo, Hamis aliruka kutoka kwenye gari na kukimbia huku watuhumiwa hao wakiondoka na marehemu Moshi.
Hamis baada ya kuona hivyo, aliomba msaada kwa raia wema ili kurudi kufuatilia alikopelekwa mwenzake. Wakati wakiwa njiani waliona gari hiyo ikisimama ghafla pembeni yao na kushuka watu wawili ambao walitaka wapande gari hiyo ili kumpeleka hospitali marehemu Moshi aliyonekana amelala nyuma ya gari, hata hiyo Hamis na raia mwema huyo walikataa.
Alielezwa kuwa watuhumiwa hao baada ya kuona wamekataa waliamua kumpeleka marehemu katika Hospitali ya Wilaya ya Mbarali na kumkabidhi kwa wauguzi ambao walimlaza.
Baba mdogo wa marehemu, Bw. Hashim Omari ambaye ni mwalimu wa Shule ya Msingi Ibara alisema marehemu Moshi, Aprili 5 mwaka huu saa 11 jioni aliondoka kwenda kuangalia mechi ya mpira wa miguu hakuonekana tena mpaka saa 2 usiku alipofika mke marehemu Hassan Mulla aliyekuwa Diwani wa Kata ya Rujewa akiwa na Salum.
Bw. Omari alisema mama huyo alimpa taarifa kuwa Hamis na mwenzake (marehemu) wamekamatwa wakiiba mapera na kwamba Hamis alikimbia na mwingine alianguka kwenye gari na kuumia na amelazwa hospitali kwa matibabu zaidi.
Alisema baada ya kusikia hivyo alikwenda hospitali na kukuta wauguzi na kuambiwa mgonjwa wake alikuwa ameshafariki wakati akipelekwa hospitalini hapo. Alikwenda chumba cha maiti ili kuthibitisha na kugundua kuwa alikuwa na majeraha kichwani, utosini, kisogoni, ubavuni na jichoni.
Alisema Aprili 6 mwaka huu alikwenda hospitali na kuomba mwili wa marehemu ufanyiwe uchunguzi ambapo aliomba madaktari wa Hosptali ya Mbarali wasitumike na kuamuliwa apeletwe daktari kutoka Hospitali ya Rufani ya Mbeya, Dkt. Mbaga aliyeufanyia uchunguzi mwili wa marehemu ambapo iligundulika alikuwa amepasuka utosini na shingo yake kuvunjwa na damu kuvilia na kusema taarifa kamili za uchunguzi za kifo hicho zitatolewa na Jeshi la Polisi.
Watuhumiwa hao waliachiwa kwa dhamana. Hata hivyo ndugu wa marehmu walikuja juu na kusababisha dhamana ya watuhumiwa hao kufutwa, hivyo kupelekwa Gereza la Ruanda wakisubiri upelelezi wa Polisi.
wanatuibia, wanatuua, mikopo wanapendelewa wao benki, (polisi, mahakama, viongozi, rais wote wamewaweka mfukoni) hivi TZ itaendelea kuwa ivi mpaka lini???????????
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya,alisema hao watuhumiwa wakiwa na mkoko wenye namba T 496 ALF Toyota Land Cruiser, waliwakuta katika shamba lao wanafunzi wawili, Salum Hamis na marehemu Moshi na kuwakamata kisha kuwaingiza katika gari hilo na kuondoka nao.
Baada ya kuona hivyo, Hamis aliruka kutoka kwenye gari na kukimbia huku watuhumiwa hao wakiondoka na marehemu Moshi.
Hamis baada ya kuona hivyo, aliomba msaada kwa raia wema ili kurudi kufuatilia alikopelekwa mwenzake. Wakati wakiwa njiani waliona gari hiyo ikisimama ghafla pembeni yao na kushuka watu wawili ambao walitaka wapande gari hiyo ili kumpeleka hospitali marehemu Moshi aliyonekana amelala nyuma ya gari, hata hiyo Hamis na raia mwema huyo walikataa.
Alielezwa kuwa watuhumiwa hao baada ya kuona wamekataa waliamua kumpeleka marehemu katika Hospitali ya Wilaya ya Mbarali na kumkabidhi kwa wauguzi ambao walimlaza.
Baba mdogo wa marehemu, Bw. Hashim Omari ambaye ni mwalimu wa Shule ya Msingi Ibara alisema marehemu Moshi, Aprili 5 mwaka huu saa 11 jioni aliondoka kwenda kuangalia mechi ya mpira wa miguu hakuonekana tena mpaka saa 2 usiku alipofika mke marehemu Hassan Mulla aliyekuwa Diwani wa Kata ya Rujewa akiwa na Salum.
Bw. Omari alisema mama huyo alimpa taarifa kuwa Hamis na mwenzake (marehemu) wamekamatwa wakiiba mapera na kwamba Hamis alikimbia na mwingine alianguka kwenye gari na kuumia na amelazwa hospitali kwa matibabu zaidi.
Alisema baada ya kusikia hivyo alikwenda hospitali na kukuta wauguzi na kuambiwa mgonjwa wake alikuwa ameshafariki wakati akipelekwa hospitalini hapo. Alikwenda chumba cha maiti ili kuthibitisha na kugundua kuwa alikuwa na majeraha kichwani, utosini, kisogoni, ubavuni na jichoni.
Alisema Aprili 6 mwaka huu alikwenda hospitali na kuomba mwili wa marehemu ufanyiwe uchunguzi ambapo aliomba madaktari wa Hosptali ya Mbarali wasitumike na kuamuliwa apeletwe daktari kutoka Hospitali ya Rufani ya Mbeya, Dkt. Mbaga aliyeufanyia uchunguzi mwili wa marehemu ambapo iligundulika alikuwa amepasuka utosini na shingo yake kuvunjwa na damu kuvilia na kusema taarifa kamili za uchunguzi za kifo hicho zitatolewa na Jeshi la Polisi.
Watuhumiwa hao waliachiwa kwa dhamana. Hata hivyo ndugu wa marehmu walikuja juu na kusababisha dhamana ya watuhumiwa hao kufutwa, hivyo kupelekwa Gereza la Ruanda wakisubiri upelelezi wa Polisi.
wanatuibia, wanatuua, mikopo wanapendelewa wao benki, (polisi, mahakama, viongozi, rais wote wamewaweka mfukoni) hivi TZ itaendelea kuwa ivi mpaka lini???????????