Msacky kaamua kuingia rasmi kwenye timu ya ushindi 2015!, sisi wasoma trend, tunasema kaamua kuchukua uamuzi wa busara!. Sio unakuwa tuu mwandishi wa habari siku zote za maisha yako, lazima ujiandae for changes!,
Hakuna ubishi kuwa Mwananchi ndilo gazeti makini kuliko yote na top in town, ila kuendelea kuajiriwa na MCL ni kukubali kuwa mwandishi wa habari maisha yako yote na utazeekea newsroom!. Kwa lugha nyingine pale Msacky alipofikia akiwa Mwananchi ndio palikuwa mwisho wake akisubiri kuzeeka, hivyo amefanya uamuzi wa busara sana kwenda mahali ambapo atapanda juu zaidi na zaidi kufuatia trend ya Mtanzania!.
Angalieni alianza Salva, mwangalie alipo sasa!, akafuatia Muhingo, mwangalie alipo sasa!, akaja Kibanda ambaye niliamini ndie angekuja kumpokea Salva mikoba, come 2015!, sasa Msaky nae kaenda, duu na mimi najiuliza sijui niamue kurejea newsroom?!, yaani nijirudishe mwenyewe utumwani kukubali kuwa mtumwa for 2015!.
Any way, hakuna ubishi kuwa Msaky ni jembe, ili ikubukwe siku zote mafanikio ya mfugaji bora, ni watoa pasi wazuri, its a team work that matters!, unaweza kukuta Msaky aliweza kungara Mwananchi kutokana na timu iliyokuwepo Mwananchi, msishangae kama ata flop Mtanzania!.
Sakina Datoo ilikuwa hivyo hivyo, aling'ara sana na Sunday Citizen kulifanya ni gazeti la never miss!, alipohama na kuhamia Guardian on Sunday aliishia ku flop!.
Ila pia hii concentration ya mafahali katika hili hili zizi moja la mgombea wetu wa 2015, linaniogopesha!, huku Bashe, kule Kibanda, sasa Msaky! who's next?!.
Pasco.