haya madeni ya mtaa ni nouma sana,unaweza ukajifungia ndani na usitoke njee hata kwenda kucheki game ya simba na ahly au vita club ukaisikia kwa wachambuzi (shafih dauda na edga kibwana tu)hivi hili deni na sawa na madeni tunayo daiwa sisi mtaani au benk maana mpaka umri unakwenda na sikia tuna deni la taifa
Wako waloshahodhi gesi hayo yatakuwa ni marudio tu. Hatari ni kujikuta tumekuwa WATUMWA nchini kwetu. Hizi ndizo gharama za CCM ambazo kwa macho ya kawaida hazionekaniSiku wanaotudai wakija kutaka chao tutawalipaje? Au tutawaachia bandari na uwanja wa ndege?
Kwamba tutabaki masikini wa kutupwa ni ndoto za alinacha, USA Ndo anaongoza kwa madeni lakini pia ndo anaongoza kwa uchumi mkubwa. Mo ni tajiri lakini kuna mwaka alienda south Africa kukopa, hapa bongo benki hazikua na pesa anayotaka. Ishu ni unautumiaje mkopoNiliwahi sema huyu bwana atatuachia structures lakini tutabaki masikini wa kutupwa.
Kwa mujibu wa Zitto,ripoti ya Benki ya Dunia teyari imeonyesha ongezeko la watu masikini wapatao milioni 2 tangu huyu bwana achukue madaraka.
Tafsiri ya haya madeni ni serikali kutumia makusanyo ya ndani kuhudumia deni la Taifa na matokeo yake ni serikali kupunguza uwezo wa kuajiri,kununua madawa,kugharamia elimu,kutoa mikopo ya elimu ya juu,kupambana na umasikini,miradi ya maendeleo kuathirika kwa kukosa fedha za kutosha,serilali kushindwa kuongeza mishahara ya watumishi,kulipa madeni ya ndani,n.k.
Kwa kifupi, haya madeni ni janga kubwa sana kwa Taifa na yanachangia umasikini wa mtu mmoja mmoja kwa njia mbalimbali.
Na bahati mbaya sana,baadhi ya miradi tunayokopea fedha kuitekeleza inaweza kuja kugeuka kuwa ni white elephant projects na hivyo ikawa ni hasara juu ya hasara.
Tuko namba saba boss, sijajua hiyo update ni yalini labda atupe linkyamekuwa cleared juzi mkuu
Sijui umeanzisha uzi huu kwa sababu ipi zaidi, ila naona kama lengo lako ni kuaminisha kwamba Tanzania iko safe.. tunajaribu kuangalia ni jinsi gani hili deni letu linakuwa kwa kasi na Athari kama taifa ikoje.. Rais amekuwa anatuaminisha kwamba tunafanya miradi ya maendeleo kwa pesa zetu wenyewe.. kwa nn mikopo inachukuliwa kimya kimya!? Hiyo List isiwe kigezo cha kutafuta comfort zone.. hii nchi kwa sasa haiendi..Hii ndio orodha kamili ya mataifa ambayo yako na madeni makubwa Barani Afrika
1. Angola = KSh 4.28 trilioni
2. Ethiopia = KSh 1.37 trilioni
3. Kenya = KSh 980 bilioni
4. Republic of Congo = KSh 742 bilioni
5. Sudan = KSh 649 bilioni
6. Zambia = KSh 637 bilioni
7. Cameroon = KSh 556 bilioni
8. Nigeria = KSh 483 bilioni
9. Ghana = KSh 349 bilioni
10. Democratic Republic of Congo = KSh 342 bilioni
Tanzania bado tupo pazuri na hasa ukizingatia miradi mingi mikubwa inakwenda kwa kasi.
Sijui umeanzisha uzi huu kwa sababu ipi zaidi, ila naona kama lengo lako ni kuaminisha kwamba Tanzania iko safe.. tunajaribu kuangalia ni jinsi gani hili deni letu linakuwa kwa kasi na Athari kama taifa ikoje.. Rais amekuwa anatuaminisha kwamba tunafanya miradi ya maendeleo kwa pesa zetu wenyewe.. kwa nn mikopo inachukuliwa kimya kimya!? Hiyo List isiwe kigezo cha kutafuta comfort zone.. hii nchi kwa sasa haiendi..
Sent using Jamii Forums mobile app
Huyu mtoa post sijui amewaza nini usiku huu mpaka kuandika illusion hiihahahahaaahhaaaa..au mtoa mada ndo NDEZI?
Bila kuiona tanzania hapo siwezi kukubaliana na post yako
juzi hapo tumeletewa bili kua tunadaiwa tilion 68+ halafu leo kwenye list hatupo kweli? Au yamelipwa tayali jana?, au wanaotudai wametusamehe?
Sent using unknown device