Deni la Taifa lafikia Tzs trilioni 61.8

Deni la Taifa lafikia Tzs trilioni 61.8

si amesema tunatumia pesa za ndani...........?????????
 
Hii inamaana kuwa kwa wastani kila mtanzania anadaiwa Tsh 1,123,636.36. Hii ni kwa idadi ya Watanzania Millioni 55. Hivi kuna analysis yoyote iliyofanyika kuwa hii miradi inayoanzishwa inauwezo wa kulipa hili deni ndani ya muda husika? Isije ikatukuta ya Zambia rasilimali za Taifa kutaifishwa na Wachina.
 
Mbona ni dogo sana ukilinganisha na miradi mikubwa inayoendelea kwa sasa hapa nchini. Angalau tufikie 100 Trillioni basi.

Kwani miradi si huwa tunaambiwa tunaitekeleza kwa pesa zetu. Sasa deni la mradi upi hasa ambao tumewahi kuambiwa kama tunatekeleza kwa mkopo? Kumbe sisi siyo matajiri kama tunavoambiwa kuwa tuna pesa zetu za kutekeleza miradi.
 
Niliwahi sema huyu bwana atatuachia structures lakini tutabaki masikini wa kutupwa.

Kwa mujibu wa Zitto,ripoti ya Benki ya Dunia teyari imeonyesha ongezeko la watu masikini wapatao milioni 2 tangu huyu bwana achukue madaraka.

Tafsiri ya haya madeni ni serikali kutumia makusanyo ya ndani kuhudumia deni la Taifa na matokeo yake ni serikali kupunguza uwezo wa kuajiri,kununua madawa,kugharamia elimu,kutoa mikopo ya elimu ya juu,kupambana na umasikini,miradi ya maendeleo kuathirika kwa kukosa fedha za kutosha,serilali kushindwa kuongeza mishahara ya watumishi,kulipa madeni ya ndani,n.k.

Kwa kifupi, haya madeni ni janga kubwa sana kwa Taifa na yanachangia umasikini wa mtu mmoja mmoja kwa njia mbalimbali.

Na bahati mbaya sana,baadhi ya miradi tunayokopea fedha kuitekeleza ni white elephant projects kwahiyo ni hasara juu ya hasara.
Ubaya ni kwamba kuna complains bado za ajira ina maana watu wanafiki hawaseize opportunities katika hii miradi au hamna sera nzuri za uendeshaji ambazo zitaengage watu hata wa kawaida kujipatia vipato.

Kama kweli miradi ipo fedha inapaswa kuzunguka na watu kuona ilo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watanzania tusifurahie yanaonyeshwa maendeleo kwa nguvu zote ila tujue mchina sip rafiki mzuri tutauzwa Kama watumwa hivi karibuni ndani ya ardhi hii.

Kama kwa miaka 3 Magufuli kakopa zadi ya tril 28 Nini maana yake na kwa lipi Kama tunavunja rekodi ya makusanyo?

Yaani unapata mshahara mkubwa huku unakopa sana ili iweje.

Namashaka kuwa hata hili Deni tutakuwa tunafichwa ukweli kwa sababu tuliambiwa miradi yote inajengwa kwa fedha za ndani na sio mikopo.

Nawataarifu tu msije sema undertaker hajawaambia China watachuka JK airport, bandari, ziwa Victoria, mlima Kilimanjaro, gesi ni Yao, pale magogoni. Itakuwa ni balozi yao
 
Miaka 3 limefika 61 Miaka 7 si litazidi 200 Kwa return ipi ya kulipa miradi hio,huku tax inakimbiza investors, pana mikanganyiko twaambiwa miradi ni hela za ndani huku deni linapaa au wanakopea miradi pia za ndani wanapigia humohumo kupitia miradi.
 
Daima mtu yoyote anaye tumia nguvu kubwa kuaminika ama kutaka sifa, lazima matumizi yake ni makubwa, yaani kuna ghalama katika kuyapata hayo.
Ndo kinacho fanyika....

Eti tumuangalie mtu mmoja analifanyia nini taifa badala ya kuangalia wananchi wote wanalifanyia nini taifa kwenye ene hayo maendeleo, na maendelo yao wenyewe.

Mtu anataka sifa leo, tujue ni kutoka jasho kwa wajukuu zetu aise..
 
Alafu mnaimbishwa wimbo eti mabeberu wanawafilisi
Wao ndo wanawatuma mkope??
Sasa within short time tupo na mdeni wa aina hyo
How about 2025


TUTAPATA TAABU SANAA
 
Hapo chini kamati imemalizia vizuri katika kuishauri serikali, ila mimi kwa mawazo yangu. Ni serikali ijikite kuwajengea uwezo wananchi wake juu ya kufanya kazi.

Kama unataka kuku sanya kodi kwa lengo la kuleta maendeleo basi wajengee uwezo wale ambao utavuna kutoka kwao.

Mimi ni muumini wa ujamaa na ujamaa ulijikita kuwajengea uwezo wananchi ili serikali ipate kodi kutoka kwao. Kupanga ni kuchagua mimi naamini watanzania waki tengenezewa mazingira mazuri ya kibiashara na kukawa na mpango mkakati juu ya kilimo hatuta hitaji mikopo kuendesha nchi.

Nakumbuka wakati Rais anazungumza nawa kuu wamikoa aliwapa maelekezo juu ya kugawa mashamba kwa vijana ili walime waache kukaa vijiweni na kucheza pool table. Sijui huo mkakati uliishia wapi tatizo letu ndio ilo. Kama mpango ule ungewekewa mkazo na kuleta mapinduzi kwenye ufugaji hakika tanzania ingekuwa nchi yakuigwa.
 
Niliwahi sema huyu bwana atatuachia structures lakini tutabaki masikini wa kutupwa.

Kwa mujibu wa Zitto,ripoti ya Benki ya Dunia teyari imeonyesha ongezeko la watu masikini wapatao milioni 2 tangu huyu bwana achukue madaraka.

Tafsiri ya haya madeni ni serikali kutumia makusanyo ya ndani kuhudumia deni la Taifa na matokeo yake ni serikali kupunguza uwezo wa kuajiri,kununua madawa,kugharamia elimu,kutoa mikopo ya elimu ya juu,kupambana na umasikini,miradi ya maendeleo kuathirika kwa kukosa fedha za kutosha,serilali kushindwa kuongeza mishahara ya watumishi,kulipa madeni ya ndani,n.k.

Kwa kifupi, haya madeni ni janga kubwa sana kwa Taifa na yanachangia umasikini wa mtu mmoja mmoja kwa njia mbalimbali.

Na bahati mbaya sana,baadhi ya miradi tunayokopea fedha kuitekeleza ni white elephant projects kwahiyo ni hasara juu ya hasara.
Hamna nchi ambayo haina deni, nenda kaangalie deni la marekani uone balaa... hilo deni kulinganisha na mambo yanaofanyika ni level zetu! Kitu kingine ulitegemea zito aseme umasikini umepungua kweli?
 
Utawala wa jiwe ni majanga nchi haifiki popote ,soon itakuwa Zimbabwe jitu nchi imelishinda linang'ang'ania tu .
 
Nilishawahi kusema hapa bwana huyu mpaka kuja kutoka madarakani atatuachia deni lipatalo 75 trillion...

Ila kwa spidi hii ya kukopa naona wazi kabisa deni la taifa litafikia 95 trillioni...
 
Back
Top Bottom