Deni la taifa lafikia trillion 40

Deni la taifa lafikia trillion 40

mimi nafikiri kuna haja ya kupeleka mswada bungeni kufuta pensheni zote za rais yeyote atakae itia hasara nchi hii itasaidia sana kuendelea kutotumia kodi zetu kumtunza mtu alieliletea hasara taifa

Naunga mkono hoja.
 
Kwa nini unalilisha maneno? Siyo mimi niliyesema kwamba uchumi unakuwa bali ni wataalumu wa kiuchumi na nimekupa link hapo sasa kama wewe unapingana nao una haki ya kufanya hivyo lkn pia ni vizuri ukaja na takwimu zako ambazo zinakinzana na hizo!
hatutaki takwimu,tunataka uhalisia.hiyo ni sawa na pale zamani tulikuwa tunafundishwa historia ya ufaransa wakati tuko tanzania!
 
hatutaki takwimu,tunataka uhalisia.hiyo ni sawa na pale zamani tulikuwa tunafundishwa historia ya ufaransa wakati tuko tanzania!


Hilo unabidi umwambie aliyeleta Mada, mimi nilikuwa namjibu tu kwa takwimu kama yeye alivyoleta hizo takwimu pia!
 
Sasa kama walikuwa wanalipa madeni deni la taifa si lingepungua ? unajua deni la Taifa lilikuwa shilingi ngapi 2015 ?
Ndiyo ujue mkuu hao unao jibishana nao ni watu wanaopewa nini cha kujibu
 
Nafikiri labda una upungufu wa uelewa wa mambo ya Kiuchumi, nchi kuwa na yenye Uchumi mkubwa Duniani USA ina deni la 102% ya uchumi wake wote (GDP)!
Ebu nenda ukajenge madungu ya kujiokoa na mafuriko ndiyo utakayo yaweza haya mambo ya kisomi waachie wenye uwezo nayo
 
Katika miezi hii sita? Lete takwimu!
Kukopa sio issue. Matumizi ya mkopo ndiyo issue. Ukikopa ukatengeneza reli Standard Gauge kuna tatizo gani kwa mfano?
Tatizo ni Kukopa ilizitumike kwenda kubembea Jamaica!
Tatizo mkuu umejitoa akili mzee jk aliacha deni ambalo ni ~trilioni 30 ,kila mwezi Awamu ya tano imekusanya zaidi ya trilioni Moja mpaka sasa sasa nijibu z
Deni limefikaje trilioni 40 ? Kama zilikopwa japani au kwingine Mpaka sasa tumezifanyiwa au ziko wapi ?


NB kumbuka kitaa tunadanganyana na kuaminishwa hela haipo sababu moja wapo ikiwa ni kulipa Madeni aliyoacha Jk kaacha mzigo mkubwa, kwanini deni linaongezeka ? .
 
Unamaanisha nini unaposema Uchumi unazidi kudorola? Uchumi wetu unakuwa kwa zaidi 7% na sisi ni wa Pili wa ukuaji kasi wa uchumi Afrika baada ya Ivory Coast na hii kulingana na UN, WB,IMF sasa huko kudorola unamaanisha nini labda?
Unaweza ukawa unapendeza nguo nzuri gari safi nyumba familia inasoma pazur chakula saf kila mtu atasema we unamafanikio zaidi ya wengine ila shughuli izo zote ulikua unafanya kwa pesa ya mkopo inamaana unazidi kudaiwa pamoja na kua unamaendeleo kwa kasi yani unapendeza kwa hela ya shemeji kwa namna nyingine siku dada akiachika ndo utaaibika ndo mana deni linakua coz barabara na majengo yote hela ni ya mzungu ulaya sio kodi yako au unajua mjapani na mchina wanatoa hela bure nn wanasema msaada kisa ni mkopo wa riba nafuu yani pesa ya riba ni ndogo tofauti na mwingine tena kisa unampa kipande cha aridhi chenye madini ndo mana jaribu kuumiza kichwa kwel binadamu tunatofautiana ndo mana ukitaka kujua ilo mte mtt hesabu nguvu mvivu akiona tu anaanza mapema bwatuka izi sijawai fundishwa wala sijui siwezi ila mwenye akili ataangalia kwa toka namba ya kwanza hadi ya mwisho na kufanya kwa kichwa atapata jibu kua hii bado kidg cjaelewa sasa na we vilevile umiza kichwa kidg kabla ya kusapoti au kupinga hoja
 
Uchumi wetu Ni mlemavu kwakuwa hatuna mbinu chanya zinazoweza kutuhakikishia tuendako...kilimo/ufugaji Doro,viwanda Doro,technolojia,uchukuzi,utalii,madini hoi!! Katika hali kama hii huwezi kujitokeza mbele za watu timamu ukiisifu hali tuliyonayo...ni kama mtu anayekuwa mwili bila kukuwa akili. Ajira kubwa kwa vijana kwasasa Ni bodaboda na biashara wanayoiwaza Ni ya viroba,bange,shisha,gongo navitu vifananavyo. What type of a country are we building?? We have to change na mh. Rais kwa ukali wake tunaweza fika mahali
 
Kwa Africa tumepitwa hata Rwanda ,ethiopia ... ivory cost inaongoza acha uongo
www.tradingeconomics.com/tanzania/gdp-growth-annual
GDP kwa mujibu wa data wa IMF na WB hawa ndo wenye uchumi wao Tanzania ni ya pili kwa ukuaji wa uchumi na imeiplace Ghana katika hiyo nafasi japo ukuaji ni chini ya 7%. Sasa wewe chanzo chako ulichotuwekea hapo ni cha kuaminika? Sio unaokoteza kila unaloliona kwenye internet na kudhani ni sahihi, umefanya assessment ya hicho chanzo chako cha habari na kujiridhisha? Kama unapinga WB na IMF ambao ndo wanacontrol uchumi unataka ukweli gani?
 
Deni sio lazima ulipe, hata hvo poa tu
Hili ndilo deni linalotukabili, ni deni lilioongezeka mara nne (4) zaidi ukilinganisha na hali ilivyokuwa miaka 10 iliyopita.

Nadhani magufuli hana choice Bali kuendesha nchi kadri utashi wake wa kizalendo utakavyomwongoza. Kama hatafunga boot ataondoka na deni likiwa limeongezeka tena , hapo hatakuwa na distinction hata aweza kujiona kama hakukuwa na maana ya kuwa kiongozi.

Tunamuombea kwa Mungu ampe sura na moyo wa simba
 
riba inazidi kutuumbua..
ndipo IQ za CCM zilipoweza kulifikisha taifa hapo..
 
kinachoshangaza ndani ya muda mfupi amekopa kiwango kikubwa cha pesa na hakuna chochote cha maana kinachofanyika ndio kwanza hali ya maisha ya mtanzania wa kipato cha chini inazidi kuwa ngumu

Sent from my TECNO M7 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom