dell wazindua tablet 4 muhimu sana

dell wazindua tablet 4 muhimu sana

Chief-Mkwawa

Platinum Member
Joined
May 25, 2011
Posts
32,229
Reaction score
44,239
kampuni ya dell si ngeni machoni mwetu wengi tunaijua kua ni kampuni inayotengeneza desktop na laptop zinazotumia windows, lakini dell anatengeneza pia vifaa vya android na windows mobile lakini havijawa tu maarufu.

dell atakumbukwa sana kwa kuanzisha simu leo hii zinazoitwa phablet (simu kubwa) , simu hii si nyengine bali ni dell streak 5. -------

Dell naona sasa anataka kurudisha historia nyuma kwa kutupa tablet 4 ambazo naweza kusema ni perfect kuuzwa nchi yoyote duniani. tablet hizi zipo za android na za windows.

DELL VENUE 7
hii ni tablet ya kwanza ambayo dell ameizindua itakua na kioo cha inch 7 na itarun android 4.2.2 na dell wamepromise kua itapata update zote 2 za android zinazokuja yani android 4.3 na 4.4 au kitkat.


tablet hii itakua inatumia processor ya intel atom yenye speed ya 1.6ghz dualcore na ram ya 2gb internal memory itakua 16gb na inakubali memory card, camera nyuma itakua ni 3.2 mp na ina front camera. resolution ya kioo ni hd ya 1200x800. tablet hii itakua na option ya line ikija na network ya hspa+ hivyo itakubali zote 2g na 3g pamoja na kua na specification kubwa tablet hii itauzwa dola 149 tu za kimarekani ambazo ni kama shilingi za tanzania 240,000

DELL VENUE 8
hii ni kama hio hapo juu hakuna cha kuongezea zaidi ila itakuja na kioo cha inch 8 na same version ya android


kwenye processor dell wame upgrade itakua ni 2ghz dual core na ram ya 2gb camera ya nyuma itakua 5mp na ya mbele pia ipo battery itabaki vile vile na itakua na option ya line ya simu hapa bei imeongezeka kidogo itakua dola 179 ambayo ni around 290,000 za kitanzania.

DELL VENUE 8 PRO
dell hawakuishia kwenye android tu wakaja kwenye windows na venue 8 pro inarun full windows 8.1 kwenye screen ndogo ya inch 8


tablet hii itatumia processor mpya za intel ziitwazo baytraill ambazo zinakaa sana na charge dell wamesema utapata masaa 10 kwenye tablet hii. itakua na ram 2gb na internal ya 32 gb. kwenye appearence inafanana na venue 8 kwa kua na umbo na kioo kinachofanana pamoja na resolution ya 1200x800. tablet hii itasuport kalamu kwa hio wazee wa photoshop hii inawahusu, na bei itakua dola 299 kama 480,000 shilingi za kitanzania

DELL VENUE 11
hii pengine ndio tablet ilioshangaza wote itakuja na kioo cha inch 10.8 (11) na itakua na specification kama za pc kubwa.


tablet hii itakua na kioo cha full hd 1920x1080 na itakua powered na intel hasswel processor i5 pamoja na ram ya 8gb. internal storage itakua gb 256 na ina uwezo wa kutumia memory card. tablet hii pia itakua na kalamu pamoja na nfc, dell pia wamesema itakaa na charge masaa 10 na battery yake itakua inatoka ili ukitaka uwe na battery ya akiba. tablet hii itauzwa dola 499 ambayo ni kama shilingi 800,000 na kuiacha mbali surface pro 2 ya microsoft.

ANGALIZO
hizi bei ni za marekani na zimeekwa kwa specification za hapo juu, mfano kama unataka tablet iongeze internal storage iende labda 64gb itabidi na hela nayo iongezeke
 
Tumekupata mkuu ila shida ni kwamba tz wajanja wengi utakuta US tablet $91 bongo anauza laki 4 hilo ndo tatizo
 
Tumekupata mkuu ila shida ni kwamba tz wajanja wengi utakuta US tablet $91 bongo anauza laki 4 hilo ndo tatizo

Dah na hiko ndicho kinachofanya bongo tuendelee kutumia vitu vilivyopitwa na wakati
 
Tumekupata mkuu ila shida ni kwamba tz wajanja wengi utakuta US tablet $91 bongo anauza laki 4 hilo ndo tatizo

sku hz kuna jamaa hapa tz unaagizia kitu nje wanakuletea unawalipa na hela ya usafirishaji unaweza kuwatumia
 
Kwa wenzetu simu sasa ni kupiga na kupokea tablet ndizo wanazo tumia kuperuzi internet ndio maana soko la simu limepungua kwa sasa tablet zipo hadi $35
 
Tatizo ni kuwa ukinunua USA, unalipa na kodi na gharama za Service ikiharibika.

Ikija Tanzania, unalipa mara ya pili hizo gharama na faida ya muuzaji na gharama zake kama zilivyosemwa.

Zingelikuwa zinaletwa moja kwa moja kutoka China aa Dell, bei ingelikuwa poa sana.

Asante kwa Info Mkuu, ngoja nimuagize mshikaji hiyo ya kwanza. Ila Betri zao vipi na Heating?
Tumekupata mkuu ila shida ni kwamba tz wajanja wengi utakuta US tablet $91 bongo anauza laki 4 hilo ndo tatizo

Dah na hiko ndicho kinachofanya bongo tuendelee kutumia vitu vilivyopitwa na wakati

sku hz kuna jamaa hapa tz unaagizia kitu nje wanakuletea unawalipa na hela ya usafirishaji unaweza kuwatumia
 
Tatizo ni kuwa ukinunua USA, unalipa na kodi na gharama za Service ikiharibika.

Ikija Tanzania, unalipa mara ya pili hizo gharama na faida ya muuzaji na gharama zake kama zilivyosemwa.

Zingelikuwa zinaletwa moja kwa moja kutoka China aa Dell, bei ingelikuwa poa sana.

Asante kwa Info Mkuu, ngoja nimuagize mshikaji hiyo ya kwanza. Ila Betri zao vipi na Heating?

kaka zimezinduliwa juzi bado sjajua kuhusu heating na battery ila kwa 4100mah itatosha matumizi ya siku na kuchaji usiku tu.

upatikanaji wake ni mwishon mwa mwez huu
 
no comment tunashukuru kwa uchambuzi
 
Ninaisubiri kwa hamu hiyo DELL VENUE 11
 
Kwa wenzetu simu sasa ni kupiga na kupokea tablet ndizo wanazo tumia kuperuzi internet ndio maana soko la simu limepungua kwa sasa tablet zipo hadi $35
  • .......na kufanya video call
 
sijaelewa sababu inayo sababisha kitu kiwe ghali kikifika hapa kuliko hata uko kinapotoka!
 
sijaelewa sababu inayo sababisha kitu kiwe ghali kikifika hapa kuliko hata uko kinapotoka!

inasababishwa na manufacture mwenyewe kukizindua eneo husika au la,

mfano nokia kitochi tz inapatikana kwa sh 25,000 wakati nokia kikawaida anaiuza dola 20 (kama elf 32) bei hapo imedrop sababu nokia kaileta mwenyewe tz kalipa usafiri kalipa na
kodi we unachofanya unanunua kwake tu.

lakini manufacture asipozindua eneo husika inabidi ukifate eneo kinapouzwa kifaa kwa dell hapa itabidi kifatwe marekani hivyo cost inazid kuwa kubwa usafiri na kodi,

mambo yanazid kuwa mabaya kama kitu kimetengenezewa china halafu hakiuzw china bali kinauzwa marekan, hapa dell ana incur cost ya kukitoa china na we una incur cost ya kukitoa marekan na kodi.

ila dell akizizindua hz tablet nchi kama india, china, vietnam na malyasia basi itakua rahisi maana wafanyabiashara wetu huvileta kodiless.
 
Nashukuru kwa Info. Nimeziona pia GSMARENA, na sijui kwa nini niliuliza hilo swali la Betri kwa huko wameandika hizo data zote. Ngoja zitoke nisome Comments za watu....
kaka zimezinduliwa juzi bado sjajua kuhusu heating na battery ila kwa 4100mah itatosha matumizi ya siku na kuchaji usiku tu.

upatikanaji wake ni mwishon mwa mwez huu
 
Back
Top Bottom