"Deep state" huu ni wakati wa kuandaa chama kingine kushika dola, kijani imeshindwa kutufikisha

Artificial intelligence

JF-Expert Member
Jan 28, 2021
1,262
2,191
Kwanza kabisa niwapongeze "deep state" kwa kazi nzito na iliyotukuka mliyoifanya tangu Tanzania ipate uhuru hadi leo, mumekuwa muhimili muhimu kuhakikisha Tanzania inavuka salama katika nyakati zote ngumu, huku mukihakikisha kuwa amani ya nchi haichezewi wala kutiwa doa na mtu yeyote.

Kijani hii imetawala tangu tupate uhuru hadi leo ni miaka 60 sasa ,Ila ni dhahiri shahiri imeshindwa kutuvusha kama nchi kutoka kwenye lindi la umasikini, rushwa n.k, katika miaka 60 ya uhuru Tanzania bado afya, umeme, maji, elimu, miundombinu, yamekuwa matatizo yasiyo tibika kama cancer.

Ni wazi kwamba "elites" wa chama hichi cha kijani mawazo yao yamegota na sera zao zimekosa vision kabisa na zimepitwa na wakati, taifa halieleweki linaelekea wapi, hivyo hawawezi kutuvusha tena hapa, ni wamefika mwisho kisera, kifikra, kimkakati na kimbinu.

"Deep state" ni wakati wenu mwingine sasa kuandaa chama kingine kimkakati ili kushika dola, chama ambacho kitakuja na sera mpya, hali mpya na vision mpya ya kuliongoza taifa letu, chama ambacho kitatufanya kutoka hapa tulipo gota na kwenda kule watanzania wengi wanapokuota.

Najua mumejitahidi sana kuandaa na bado mnaendelea kuwaandaa baadhi ya viongozi kwenye chama cha kijani na nchi kwa ujumla kwa nia yenu nzuri tu ya kulivusha taifa ila wamewaangusha kutokana na sera mbovu za chama cha kijani, hivyo siyo vibaya sasa tujaribu na chama kingine tuone kitatufikisha wapi, kwani sera za chama cha kijani zimeshindwa kabisa kutuvusha.

Watanzania ni ngumu sana kujichukulia sheria mkononi kutokana na historia ya nchi hii, hivyo ni ngumu sana watanzania kuandamana au kufanya vurugu wakidai haki yao ya mageuzi kama nchi zingine, kwani nchi hii, haijawahi kuwa na migogoro ya ndani, kwahiyo hata wenzetu kupandikiza mamluku Tanzania kuchochea harakati za mabadiliko ni ngumu sana.

"Deep state" mumehepusha mengi na kufanya makubwa na mazuri zaidi, hivyo naamini nyinyi ndiyo watu wa kwanza ambao mnaweza kuleta "transformation" katika taifa hili na mkihamua kwanza, basi na watanzania watafuata.

Katiba mpya na iliyo bora ni muhimu sana na kupitia katiba mpya , mnaweza sasa kuandaa chama kingine kwa ajili ya kuliongoza taifa hili, kwani kwa sasa hamna chama chenye ubavu wa kuishinda kijani iliyo ota mizizi kila sehemu, lakini naamini mkiamua itawezekana kwani hakuna linaloshindikana mbele yenu.

Tambueni ya kwamba kwa "nature" ya taifa letu ni ngumu sana wananchi kudai mageuzi ya kiutawala kwa nyakati hizi hata wapitie katika kipindi kigumu kiasi gani, Ila nyinyi mkihamua kuanza kuleta hayo mageuzi hata wananchi watafuata pia, kwahiyo ni vyema mkaandaa chama kingine na kuwagroom viongozi wengine wapya kwa ajili ya kushika dola kwa wakati ujao, ili tuone kama tutavuka hapa ilipotufikisha kijani.

Kwa sasa si KIJANI wanaoweza kutufikisha pale tunapopakusudia kama taifa kwani wameishiwa na wamefika mwisho kifikra, bali ni nyinyi tu "deep state" wenye maamuzi ya juu zaidi yaliyobeba mustakabali na dira ya taifa letu.
 
Katiba bora ndiyo deep state.

Uliowataja huyajui majumumu yao,ukiyajua kisheria kwa katiba hii CCM wataendelea na mbinu zao kila uchaguzi.

Uliowataja hawatungi sheria za Nchi bali wanasimamia kuhakikisha hakuna nyau atapindisha.
 
Katiba bora ndiyo deep state.
Uliowataja huyajui majumumu yao,ukiyajua kisheria kwa katiba hii CCM wataendelea na mbinu zao kila uchaguzi.
Uliowataja hawatungi sheria za Nchi bali wanasimamia kuhakikisha hakuna nyau atapindisha.
Kuhusu kutotunga sheria na kuhakikisha sheria hazivunjwi upo sahihi, Ila naomba nikuambie kwamba, hawa hawa wana uwezo wakuipiga chini hiyo sheria kama kuna jambo la kimkakati wanataka lifanyike na hakuna wa kuwauliza wala kuwazuia. Hivyo wakihamua jambo fulani liende wanavyotaka litaenda, au wakisema jambo fulani lisitishwe, linasitishwa mara moja na hamna wa kuwahoji.
 
deep state ni ccm wenyewe wanakubali kila kitu cha deep state hivyo wahaona hakuna haja ya kubadili
Wanakubali kila kitu ndiyo, kwa sababu wanajua bila hao kuridhia, hawawezi kushika dola. Lakini sasa ndiyo hivyo kijani hawana jipya tena, hivyo ni wakati wa kuandaa chama kingine kushika dola ili tujaribu sera mpya.
 
Kuhusu kutotunga sheria na kuhakikisha sheria hazivunjwi upo sahihi, Ila naomba nikuambie kwamba, hawa hawa wana uwezo wakuipiga chini hiyo sheria kama kuna jambo la kimkakati wanataka lifanyike na hakuna wa kuwauliza wala kuwazuia. Hivyo wakihamua jambo fulani liende wanavyotaka litaenda, au wakisema jambo fulani lisitishwe, linasitishwa mara moja na hamna wa kuwahoji.
I agree with u logic. Kwa mfumo wa wabunge wanaoulizwa wanaohofikia serikali Ndiyooooo.

Bunge likisimama kwa wananchi Deep state itakuwa nao kuisaidia sheria hizo zipite.

Hizi sheria zakuvilinda vyama kila mwaka tutakuwa tunajadili mahitaji ya vyoo
 
I agree with u logic. Kwa mfumo wa wabunge wanaoulizwa wanaohofikia serikali Ndiyooooo.

Bunge likisimama kwa wananchi Deep state itakuwa nao kuisaidia sheria hizo zipite.
Hizi sheria zakuvilinda vyama kila mwaka tutakuwa tunajadili mahitaji ya vyoo
Naamini kabisa wakisema katiba mpya na iliyo bora ipatikane, lazima serikali ya kijani itatekeleza, then kupitia hiyo katiba wananchi watakuwa wamepewa nguvu, kwahiyo kupitia hiyo nguvu ya wanachi, watakuwa tayari kutekeleza hili nililolisema.
 
Kwa asili ya wizi wa WaTz, hiyo deep state itakuwa inakomba kupita maelezo, kama watazikwa nazo vile!
 
Kwanza kabisa DEEP STATE ni serikali ndani ya serikali, kwa namna kubwa deep state huundwa na waasisi wa taifa ama washirika wa waasisi, inawezekana kwa upande wetu hapa waasisi na washirika wao wakawa na mlengo wa chama tawala.

Deep state pia huenda ikaundwa na jopo la wafanyabiashara wakubwa, ambao kwa namna pana wameshika uchumi wa taifa.

Deep state pia huenda ikawa imeundwa na maafisa wa ngazi ya juu wa majeshi ya ulinzi na usalama wa taifa.

Tuone kwa hapa kwetu kwa makundi hayo matatu.
Kundi la kwanza la waasisi, wao ndio walionunda chama tawala ambacho kimeshika dola tangu uhuru, ni ngumu hawa kukubali nchi ikawa chini ya chama kingine, kwani tayari huamini kwao ndipo hutoka watu wanaoifahamu nchi, A-Z na ikiwa kuna aliye bora kutoka nje, yapaswa aungane nao, hawa huwa tayari kwa namna yoyote kununua watu kutoka makundi mengine ya kisiasa. Kwa kuwa huamini wao ndio wanaoweza kushika dola na si vinginevyo.


Wafanyabiashara, nchi yetu ina “elites” ambao wengi wao ni watu wenye asili ya kutoka mashariki, hili kundi ndilo lenye ushawishi wa kiuchumi nyumbani kwetu, wala kusiwe na matarajio makubwa since watu hawa biashara zao zinamea na maslahi yao kukuwa kutokana na mfumo huu uliopo, they don’t have sense of nationalism, ndio mana wengi hawana feelings za harakati za kisiasa zaidi ya kuwa walamba nyao.

Maafisa wa jeshi; kama ulikuwa hujui historia ya jeshi letu ni chama cha TANU, baada ya mgomo wa jeshi la uhuru (Tanganyika Rifles) ambalo kwa namna kubwa liliundwa na wazungu mwaka 1964, jeshi likabadilishwa, recruitment kubwa ikafanywa na vijana wa tawi la TANU (TANU Youth League) ambalo kwa leo ni kama (VUMCC) usije kutegemea strike, kwa sababu msingi wa jeshi ni kutumikia chama. Kwa hivyo wao ndio watakaopika viongozi na kukabidhi nchi, no matter upinzani kuna viongozi wazuri namna gani, aidha waungane nao.

Wanasema “if they won’t kill you with NO EDUCATION they’ll kill you with POOR EDUCATION”

Kundi kubwa la taifa ni knowledge dead heads, ama kundi lililoelimika ni half cooked. Sio deep state wakubadilisha, hata wao wanaangalia upepo wetu.

Ni hayo.
 
Back
Top Bottom