Debate sherehe za uhuru na kuminywa kwa uhuru

Abdul Nondo

JF-Expert Member
Oct 28, 2016
515
2,875
Tulipokuwa tunapigania uhuru kutoka kwa wakoloni kulikuwa na mambo yetu ya msingi tuliyotaka sisi tuyapate.

Waasisi na wapigania uhuru wa Taifa letu walitaka uhuru (freedom) au self-determination(Yaani watu na taifa lao kwa ujumla wawe na haki ya kuunda serikali au utawala wao binafsi ) unaotokana na matakwa ya watu wake bila msukumo wowote wa nje au wa mtu yeyote.

Tulitaka tuwe huru kama kujiamulia masuala yetu binafsi ya kisiasa, kiuchumi na kijamii hata kitamaduni bila kuingiliwa na mtu.

Tulitaka tuwe na utawala au serikali itakayoheshimu katiba ya nchi na kuweka wananchi katika dhima ya kila jambo,tulitaka serikali inayojali maendeleo ya watu (People centered development) na sio vitu kama mkoloni alivyokuwa anafanya.

Hatukuhitaji utawala ambao utafinya uhuru na matakwa ya wananchi.Hatukutaka utawala ambao maendeleo, haki na huduma za kijamii hutolewa kwa ubaguzi, rangi na itikadi na fikra tofauti.

Hatimaye tulitapata uhuru ,tukaweka siku ya tar 9/Dec kila mwaka kama ni siku ya kumbukizi ya uhuru wetu. Maana yake sio kukumbuka kuwa siku ya tar 9/Dec/1961 ni siku tuliyopata uhuru, haina maana hiyo.

Ina maana kuwa tunajikumbusha kila mwaka kuyaenzi na kuzidi kuyaimarisha yale yote tuliyokuwa tunayadai kutoka kwa mkoloni,ile misingi tuliyoiamini na kupigania sisi kupata uhuru ndio inapaswa izidi kuimarishwa, pia kuwakumbuka wote waliosaidia nchi yetu kupata uhuru na kuzidi kuenzi fikra na misingi yao.

Ukweli upo wazi kuwa misingi yote na uhuru binafsi wa watu na kimfumo umeyumba sana, ubaguzi umezidi kuwa mpinzani wewe sio mzalendo, kufanya siasa ni uasi,bendera za chama pinzani ni kuhimiza uwasi, uhuru wa vyombo vya habari mfukoni.

Hivyo kuna fikra za makundi mawili kuna watu wanaoamini kwamba.

Kushiriki katika siku ya uhuru haina maana yeyote na sio nguzo ya kuimarisha umoja wa Kitaifa.

Sababu siku hiyo ina kosa maana, kwani ile maana ya uhuru tunaoadhimisha haipo tena, na ukweli ndio huo kuwa uhuru umefinywa,demokrasia inachezewa.

Watu hawa kutohudhuria kwao ni njia ya kuendelea kuonesha hisia zao kwamba uhuru hakuna, demokrasia hakuna.

Mamlaka watakapojirekebisha wanaonekana kuwa wapo tayari kushiriki. Hii ni (Passive Resistance).

Hawa wanaweza kuutaja kama mfano, hiki kitendo cha Mkuu wa Wilaya wa Sumbawanga aliyeagiza Bendera za Chadema kushushwa, hii haina tofauti na wakati wa mkoloni dhidi ya vyama vya ukombozi.

Hawa wanamini kwamba umoja wa Kitaifa sio kufanya sherehe, umoja wa Kitaifa ni kuyasimamia na kuishi katika hizo kumbukizi za uhuru. Wao wanaamini umoja wa kitaifa tayari umeshavurugwa na hao wanaofanya hizi sherehe kwa kutoheshimu na kufuata misingi yote na malengo yaliyofanya tupiganie Uhuru.

Hawa wametafsiri uhuru kwa upana sana. Wakiona ni kupotezeana muda kusherekea uhuru ikiwa hakuna uhuru ni kuunga mkono kufinyangwa kwa uhuru.

Hawa wanaweza kutoa public statement siku ya uhuru ikawa ni statement au ujumbe wa maandishi kwenda kwa umma na watawala wakiwaambia watawala wanapaswa kuheshimu uhuru na demokrasia kwa vitendo kama waasisi wetu walivyofanya na sio kupitia sherehe tuu.Hiyo pia itasomwa na watawala pia ni njia moja wapo pia ya kusherekea.

2. Kuna kundi lina amini kwamba ,siku ya uhuru ni siku ambayo wanapaswa kuhudhuria sababu wanaamini ni siku muhimu ya Kitaifa na ina onganisha watu,n a ni siku ya maslahi ya Taifa Zima.

Njia hii ni (Collaboration), wakiamini kupitia siku hii labda wanaweza toa ujumbe kwa mamlaka juu ya umuhimu wa kuheshimu misingi ya uhuru na demokrasia.

Ila changamoto yake ni kwamba kupata hiyo nafasi ya kutoa ujumbe kwa watawala ni jambo ambalo lipo katika uwezo wao, wanaweza kuamua viongozi wa vyama pinzani wasimame wasalimie tu. Na nafasi inaweza kukosekana.

Ila kama wakipewa nafasi na kuongea hata dakika 5 kuongea kwa kutoa ujumbe wa kudai uhuru na demokrasia itakuwa na maana sana, mbele ya umati wa watu, je nafasi hiyo ipo? Maana unaweza kwenda kushiriki siku ya uhuru hata uhuru wa kuongea na kutoa ujumbe wanaweza nyima watu.

Wote wawili wanapigania uhuru na demokrasia kwa namna wanavyoona ni sahihi.

Abdul Nondo.
 
Abdul Nondo,
Abdul, japo naunga mkono hoja zako, ili kama nilisikia ulirudi chuo kukamilisha masomo yako, nakushauri maliza kwanza shule ndipo ujiunge nasi huku kitaa tulisongeshe!, hizi nyakati sasa zimebadilika, ni nyakati nyingine, nyinyi mlioko shule, nawashauri shikeni moja tuu, shule, na masomo, someni, mkimaliza shule ndipo karibuni kitaa!.
Ni ushauri tuu.
P
 
Sasa wewe Nondo unadhani mtu kama mh Mbowe akipewa nafasi ya kuongea atasema nini wakati ndani ya chama chake wabunge na madiwani wanakimbia kwa kukosekana kwa uhuru wa kuongea na kutenda?!
Mbowe kakukaa sana naona una muwaza sana
Ngj ntawasiliana na swai cdm hapo anipatie namba yake nkurushie..... Ili Roho na nafsi yako itulie

Ova
 
Abdul, japo naunga mkono hoja, nilisikia ulirudi chuo kukamilisha masomo, nakushauri maliza kwanza shule ndipo ujiunge nasi huku tulisukume!, hizi nyakati sasa zimebadilika, ni nyakati nyingine, nyinyimlioko shule, shikeni moja tuu, masomo, someni, mkimaliza,karibuni kitaa!.
Ni ushauri tuu.
P
Mbona wakina Samuel sitta na wengineo walikuwa wanafanya siasa wakiwa chuoni
Mwache afanye ajuavyo yeye, mbona ccm vyuoni harakati wanafanya na hamuwasemi
Au ndiyo mupe muruke

Ova
 
Mbona wakina Samuel sitta na wengineo walikuwa wanafanya siasa wakiwa chuoni
Mwache afanye ajuavyo yeye, mbona ccm vyuoni harakati wanafanya na hamuwasemi
Au ndiyo mupe muruke

Ova
Uwe unasoma kilichoandikwa mkuu pasco kasema zama hizi hivi kila sita wapi mwaka wangapi hapo chuoni


Nasikia mbowe kiongozi wako kesho anakwenda kulamba viatu vya jpm ili angalau kamba isizidi kuvutwa

USSR
 
Tunahitaji Uhuru wa kiuchumi sio makelele ya mtaani kama haya

USSR
 
Uwe unasoma kilichoandikwa mkuu pasco kasema zama hizi hivi kila sita wapi mwaka wangapi hapo chuoni


Nasikia mbowe kiongozi wako kesho anakwenda kulamba viatu vya jpm ili angalau kamba isizidi kuvutwa

USSR
Jiwe ameishafeli SGR imemdidindia, deni LA taifa tril. 54 mwakani hakuna hela ya kugjaramia uchaguzi, Mpango kaenda kuomba kuambiwa hakuna hela bila demokrasia,
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Abdul, japo naunga mkono hoja zako, ili kama nilisikia ulirudi chuo kukamilisha masomo yako, nakushauri maliza kwanza shule ndipo ujiunge nasi huku kitaa tulisongeshe!, hizi nyakati sasa zimebadilika, ni nyakati nyingine, nyinyi mlioko shule, nawashauri shikeni moja tuu, shule, na masomo, someni, mkimaliza shule ndipo karibuni kitaa!.
Ni ushauri tuu.
P
Umemshauri kama baba na kama mdogo wake kwakuwa ww ni verified na unafahamika nadhani atazingatia ushauri wako, binafsi nilijaribu kumshauri ila niliambulia kebehi kutoka kwake.
 
Abdul, japo naunga mkono hoja zako, ili kama nilisikia ulirudi chuo kukamilisha masomo yako, nakushauri maliza kwanza shule ndipo ujiunge nasi huku kitaa tulisongeshe!, hizi nyakati sasa zimebadilika, ni nyakati nyingine, nyinyi mlioko shule, nawashauri shikeni moja tuu, shule, na masomo, someni, mkimaliza shule ndipo karibuni kitaa!.
Ni ushauri tuu.
P
Kaka Mayalla ,Muda sikuwepo huku nilikuwa namalizia Shahada yangu ya Sayansi ya siasa na utawala wa umma na Nov iliyopita ilikuwa siku ya Graduation yangu .Na rasmi kutunukiwa Degree yangu.Pia nikapata mshukuru Mungu kwa baraka zake.Pia shukrani na watu wote humu kwa ushauri wenu na encouragement kwangu kwa muda wote.Kaka Mayalla naomba kuwasilisha.
IMG_20191209_113020_072.jpeg
IMG-20191209-WA0109.jpeg
 
Sasa wewe Nondo unadhani mtu kama mh Mbowe akipewa nafasi ya kuongea atasema nini wakati ndani ya chama chake wabunge na madiwani wanakimbia kwa kukosekana kwa uhuru wa kuongea na kutenda?!
Madiwani na Wabunge wanakimbia au CCM inawanunua? Hakuna Diwani au Mbunge aliyekimbia wote ni siasa chafu za kuua upinzani
 
Kaka Mayalla ,Muda sikuwepo huku nilikuwa namalizia Shahada yangu ya Sayansi ya siasa na utawala wa umma na Nov iliyopita ilikuwa siku ya Graduation yangu .Na rasmi kutunukiwa Degree yangu.Pia nikapata mshukuru Mungu kwa baraka zake.Pia shukrani na watu wote humu kwa ushauri wenu na encouragement kwangu kwa muda wote.Kaka Mayalla naomba kuwasilisha.View attachment 1286254View attachment 1286257
Hongera sana, Mkuu Abdul Nondo, karibu rasmi, na 2020 tuingie kwenye ground zero.
Hata mimi natupa kalamu pembeni, naingia uwanjani kupambana.
P
 
Kuwa makini na akina dada Kawe Alumni wakiona hizi picha hujawa na ashki! Chunga wasikupotoshe

CC @wakudadavuwa
Kaka Mayalla ,Muda sikuwepo huku nilikuwa namalizia Shahada yangu ya Sayansi ya siasa na utawala wa umma na Nov iliyopita ilikuwa siku ya Graduation yangu .Na rasmi kutunukiwa Degree yangu.Pia nikapata mshukuru Mungu kwa baraka zake.Pia shukrani na watu wote humu kwa ushauri wenu na encouragement kwangu kwa muda wote.Kaka Mayalla naomba kuwasilisha.View attachment 1286254View attachment 1286257
 
Back
Top Bottom