DC Temeke akutana na Baraza la Wazee wa Temeke

JUMA JUMA

JF-Expert Member
Jan 5, 2013
666
835
DC TEMEKE AKUTANA NA BARAZA LA WAZEE

Mkuu wa wilaya ya Temeke Mheshimiwa. Jokate Mwegelo amefanya kikao kifupi na Baraza la Wazee Wilayani hapo. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa halmashauri ya manispaa ya Temeke (DMDP) leo Julai,30,2021, majira ya saa nne asubuhi kufuatia ombi la Wazee hao.

Katika kikao hicho kilichohudhuriwa na wajumbe wa baraza la Wazee, lengo likiwa ni kumkaribisha na kumpongeza Mhe. Mwegelo kwa kuaminiwa miongoni mwa wengi na kuteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Temeke.

Aidha Mhe. Mwegelo amefurahishwa na uwepo wa Wazee hao, akisema umuhimu wao ni mkubwa katika kuleta maendeleo ya Temeke na hivyo kuwaomba wazee hao kusaidia katika kuwaombea viongozi wa nchi, hasa katika kipindi hiki cha janga la UVIKO 19 na pia ushirikiano juu ya maendeleo ya Temeke.

"..Ninawaomba sana ushirikiano wenu na ushiriki wenu, ili tuweze kuongoza vizuri zaidi".

Katika hatua nyingine Mhe. Mwegelo amewaomba Wazee hao kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya Sita katika mapambano dhidi ya UVIKO 19 kwa kuwahamasisha watu wao kufuata mwongozo na taratibu zinazotolewa na Serikali kupitia waataalamu wa afya.

Pia ameeleza namna serikali chini ya Mhe. Rais, Samia Suluhu Hassan ilivyo mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya COVID-19.
"... Mheshimiwa Rais amekuwa jemedari na ametuongoza vizuri sana katika haya mapambano .."

IMG_20210730_214806_013.jpg

IMG_20210730_214806_014.jpg

IMG_20210730_214806_015.jpg

IMG_20210730_214806_016.jpg
 
Haya alikuwa mtoto naona sasa kakulia kwenye UDC humo.

Nyota yake na ing'ae zaidi.
 
DC TEMEKE AKUTANA NA BARAZA LA WAZEE

Mkuu wa wilaya ya Temeke Mheshimiwa. Jokate Mwegelo amefanya kikao kifupi na Baraza la Wazee Wilayani hapo. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa halmashauri ya manispaa ya Temeke (DMDP) leo Julai,30,2021, majira ya saa nne asubuhi kufuatia ombi la Wazee hao.

Katika kikao hicho kilichohudhuriwa na wajumbe wa baraza la Wazee, lengo likiwa ni kumkaribisha na kumpongeza Mhe. Mwegelo kwa kuaminiwa miongoni mwa wengi na kuteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Temeke.

Aidha Mhe. Mwegelo amefurahishwa na uwepo wa Wazee hao, akisema umuhimu wao ni mkubwa katika kuleta maendeleo ya Temeke na hivyo kuwaomba wazee hao kusaidia katika kuwaombea viongozi wa nchi, hasa katika kipindi hiki cha janga la UVIKO 19 na pia ushirikiano juu ya maendeleo ya Temeke.

"..Ninawaomba sana ushirikiano wenu na ushiriki wenu, ili tuweze kuongoza vizuri zaidi".

Katika hatua nyingine Mhe. Mwegelo amewaomba Wazee hao kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya Sita katika mapambano dhidi ya UVIKO 19 kwa kuwahamasisha watu wao kufuata mwongozo na taratibu zinazotolewa na Serikali kupitia waataalamu wa afya.

Pia ameeleza namna serikali chini ya Mhe. Rais, Samia Suluhu Hassan ilivyo mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya COVID-19.
"... Mheshimiwa Rais amekuwa jemedari na ametuongoza vizuri sana katika haya mapambano .."

View attachment 1874495
View attachment 1874496
View attachment 1874497
View attachment 1874498
HIVI HAYA MABARAZA ya WAZEE kwanini Yawe ya WAZEE wa CCM tu ina maana Hakuwa hata Wazee wengine Wasio na Vyama?
 
Back
Top Bottom