Donatila
JF-Expert Member
- Oct 23, 2014
- 7,561
- 21,533
Mkuu wa wilaya ya Kilwa,mkoani Lindi,Christopher Ngubiagai,amewaagiza watendaji pamoja na wenyekiti wa vijiji vyote vya wilaya hiyo kuhakikisha wanawakataza wananchi katika maeneo yao kuacha mara moja tabia ya kuchoma moto mapori hasa kipindi hiki cha kuandaa mashamba kwa ajili ya msimu wa kilimo.
Amesema tukiwaachia wananchi kuendelea kuchoma moto mashamba kila kukicha bila kufanya chochote Kilwa itakuja kugeuka jangwa hali ambayo itasabisha ukame,lazima wahusika walifanyie kazi kwa kuwakataza wananchi katika maeneo yao kuacha tabia hiyo mara moja.
ITV