Dkt. Christopher Timbuka: Tutunze mazingira ili tupambane na mabadiliko ya tabia nchi

Blasio Kachuchu

Senior Member
Sep 7, 2016
156
112
Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe. Dkt Christopher Timbuka akipanda mti wakati akizindua kampeni ya utunzaji mazingira iliyopewa jina (Go green, save nature) iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita iliendana na kongamano la siku mbili lililowajumuisha wadau mbali mbali wa misitu.

Mhifadhi Mkuu (TFS) West Kilimanjaro PCO Robert Faida akipanda mti wakati akizindua kampeni ya utunzaji mazingira iliyopewa jina (Go green, save nature) iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita iliendana na kongamano la siku mbili lililowajumuisha wadau mbali mbali wa misitu.

Mratibu wa kampeni hiyo, Mensieut Elly akipanda mti wakati akizindua kampeni ya utunzaji mazingira iliyopewa jina (Go green, save nature) iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita iliendana na kongamano la siku mbili lililowajumuisha wadau mbali mbali wa misitu.

Mmoja ya wadau wa Mazingira toka nchini Kenya, Jesca nae alipata wasaa wa kupanda mti na kushuhudiwa na viongozi.


Kongamano kwa njia ya mtandao likiendelea.


Mhifadhi Mkuu (TFS) West Kilimanjaro PCO Robert Faida akifafanua jambo mbele ya wanahabari.


Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe. Dkt Christopher Timbuka (kushoto) akijadiliana jambo na Mhifadhi Mkuu (TFS) West Kilimanjaro PCO Robert Faida mara baada ya kumaliza zoezi la upandaji miti katika kampeni ya "Go green, save nature".

Na Cathbert Kajuna - MMG/Kajunason, West Kilimanjaro.

Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kupitia hifadhi ya Misitu ya West Kilimanjaro wakishiriana na Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro wameanzisha kampeni ya Upandaji wa Miti ili kukabiliana na Mabadiliko ya Tabia nchi.

Kampeni hiyo inajumuisha kutoa elimu kwa Jamii, upandaji wa miti hasa pembezoni mwa milima Kilimanjaro ili kusaidia kukabiliana na mabadiliko ya Tabia Nchi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni hiyo ya utunzaji mazingira iliyopewa jina (Go green, save nature) iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita iliendana na kongamano la siku mbili lililowajumuisha wadau mbali mbali wa misitu na kuongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe. Dkt Christopher Timbuka.

Mhe. Dkt Timbuka alisema kuwa ni vyema jamii ikajiongeza katika utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti ili kusaidia upatikanaji wa mvua kwa wakati.

"Eneo la Siha lilikuwa kijani ila shughuli za kibinadamu ikiwemo kukata miti na uchomaji holela wa maeneo imepelekea kuwa jangwa na kufanya wananchi wapolomoke kiuchuni, wananchi wanategemea mvua sasa ikikosekana hali inakuwa ngumu," alisema Dkt Timbuka.

Aliwaomba wana Siha wote kujitokeza kupata elimu ya utunzaji wa mazingira pamoja na kupanda miti ili kusaidia upatikanaji wa mvua na kurejesha uoto wa asili.

Kwa upande wake Mhifadhi Mkuu (TFS) West Kilimanjaro PCO Robert Faida alisema ili kuhuhisha uharibifu ilikuokoa adhari za mabadiliko ya tabia nchi ni vyema jamii ikaacha tabia ya kuchoma moto pindi wanapoandaa mashamba jambo ambalo husababisha athari za kuunguza misitu na kusababisha hasara.

Aliongeza kuwa TFS West Kilimanjaro kwa sasa wameshaanza kutoa elimu kwa jamii inayoizunguka na kuwapa miti wapande ili kufanya Siha inakuwa ya Kijani.

Alisema endapo Jamii itafuata yale yote ambao wakuwa wakifundishwa kayika utunzaji wa mazingira basi tunaweza kukabiliana moja kwa moja na mabadiliko ya tabia nchi pia aliishukuru TFS na Serikali ya Wilaya ya Siha pamoja na wadau wa maendeleo kwa ushirikiano ambao wamekuwa wakifanya pamoja katika kupambana na mabadiliko ya tabia nchi.
 
Back
Top Bottom