DC amkwida diwani katika chakula

Wote walipungukiwa busara. Kwa nini ajichomeke pasipo kufuata itifaki iliyokuwa ikitangazwa? Na DC kwa nini akwide....hakukuwa na askari wa kumsaidia hilo? Wote hopeless kabisa.
 
Kama tatizo ni ITIFAKI mbona diwani wa TLP aliachwa inamaana hakumfahamu? Tatizo wateuliwa wote wanafahamu mkakati maalum wa kuakikisha CDM wanazibitiwa kwa ghalama yoyote ndio maana wakionekana tu watu wanajua ajira zao zipo hatarini. Kwa mwenendo huu 2015 kazi ipo CCM wanaonekana wazi hawajajiandaa kushindwa hivyo ikitokea hivyo hawatakubali.
 
Kulikuwa na ulazima gani kula cha bure ? na hii ndio maana sipendi vyakula vya visheree
 
Diwani wangu ameniangusha, kupigwa Tanganyika jeki kwa ajili ya ubwabwa tu......
Mbona sijasikia njaa ya chakula huko wilayani Kahama? Udhalilishwaji mwingine mtu unajitakia mwenyewe.
 
Kuna watu wana roho ndogo aisee!
When it comes to ubwabwa! DC unasimamia mstari wa ubwabwa!! Huyu hata nyumbani kwake anahesabu finyango!

...Umeniwahi Mkuu, nilitaka kusema hivyo hivyo! 'Raisi' wa Wilaya unasimamia foleni ya Ubwabwa kujua nani ale na nani asile?? Kwani angemuachia huyo jamaa akala kungekuwa kumepunguka nini?? Huyo diwani angekuwa ni raia wa kawaida asiyekuwa na cheo si angweza hata kujikuta akipigwa na 'kitu kizito'??!!
 
...nani alionewa nani alimkwida mwenzie doesn't matter as such. mannerism ya mtu inapimwa sana tena sana kwenye msosi. ili kuonesha dharau ya hasa, kwenye mstari siendi bila kuitwa, na nisipoitwa kama hakuna ratiba za maana zinazoendelea naaga wadau wa karibu yangu naondoka hata kama msosi ni lobster.
msosi? ukiuendekeza utakuua
 
Aisee ni aibu isiyovumilika! Yaani mtu unapigwa tanganyika jeki halafu unakabidhiwa kwa policy? Hata kama ni chakula gani siwezi tena kula wala kuonekana tena ktk eneo Hilo! Labda tu kwa vile binadamu tunatofautiana! Nimewahi kumshuhudia mshkaji wangu mmoja na heshima zake kwenye bufee ya mnuso fulani hivi kapakua msosi Wa ajabu (lumbesa) kiasi sikuamini macho yangu! Wapo watu wana-mind ubwabwa kushinda maelezo!
 
Nashawishika kuamini DC ana matatizo yake binafsi na CDM kama suala ni itifaki mbona alimwita diwani wa Musoma mjini na hakumkwida diwani wa TLP wote hao si madiwani ukizingatia DC alikuwa mbunge wa MBEYA MJINI kabla ya kushindwa na SUGU
 
Naogopa kujuaa nyumbani kwake huyu DC na kuwahesabia matonge na finyango za nyama watoto wake!!!!sintashangaaa!!!
 
swala si chakula !!!!! ni itifaki kutozingatiwa na kwa sasa dhifa kama hizo imeonekana zitumike kadi watu wahusikwa kupewa na si yeyote aingie humo mpaka watu wa kujilipua (wazamiaji)
 
KABLYA YA KUDHALILISHWA TAYARI MHESHIMIWA DIWANI ALISHAJIDHALILISHA MWENYEWE! KWANI ANGEFATA UTARATIBU ANGEBADILIKA NINI?? MIMI SI SHABIKII SIASA WALA SI MWANACHAMA WA CHAMA CHOCHOTE ILA WHEN IT COMES TO " KUFUATA UTARATIBU" HUWA NAHESHIMU SANA.UKIENDA NYUMBANI KWA MTU UKIONA MWENYEWE ANAVUA VIATU MLANGONI INABIDI NA WEWE UVUE HATA KAMA SI KAWAIDA YAKO....HAPA SI SUALA LA UCHADEMA WALA UCCM, LETS BE OPEN MINDED...MAJITU YA NAMNA HII YAKIENDA NCHI ZA WATU NDO YANATIA AIBU HAYA. ON another side of the coin, pamoja na mheshimiwa diwani kukaid amri ya mkuu wa wilaya, mkuu wa wilaya angetumia busara kuwaomba watu wa usalama kumuomba mh. diwani afuate utaratibu kuliko kumpiga jeki hadharani kwani hiyo si kazi yake, ni kazi ya vyombo vya usalama...japo diwani alikosea lakini busara nayo ya kiungwana inabidi itumike kwa wale wasioonesha uungwana.
 
Wali nyama na mirinda orange a hv naweza pika mwenyewe hata kama wife hayupo, cjapanga foleni bado ya manyanyaso.huyu wakimpa ucku mmoja lakairo hoteri c atasaliti chama.
 
Back
Top Bottom