DAWASA, yajipanga kukabiliana na Upungufu wa maji ili kuepuka mgao

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,930
12,216
TAARIFA KWA UMMA

JITIHADA ZA KUPAMBANA NA UPUNGUFU WA MAJI MTO RUVU

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar-es-salaam (DAWASA) inawataarifu wakazi wa Bagamoyo hadi Kigamboni wanaohudumiwa na mtambo wa Ruvu Chini kuwa bado kuna hali ya upungufu wa maji katika mto Ruvu kutokana na kiangazi cha muda mrefu.

Ili kuhakikisha kuwa maji kidogo yaliyopo yanafika katika mitambo ili kuchakatwa kwa ajili ya matumizi ya binadamu, timu maalum ya wataalamu wa Wizara ya Maji na DAWASA imeendelea kuhakikisha kuwa vibali vya watumiaji wengine ikiwa ni pamoja na vya wakulima vinasitishwa.
Aidha shughuli za kunywesha mifugo katika mto pia zimesitishwa.

Kwa kawaida DAWASA huzalisha lita milioni 520 kwa siku, mabadiliko ya hali ya hewa yameathiri mititririko ya mikondo na mito (hususani Mto Ruvu) na kupelekea uzalishaji maji kupungua kwa asilimia 12 ambapo sasa maji yanayozalishwa kwa siku ni lita milioni 460 kwa siku. Kutokana na hali hiyo, maji yamekuwa yakipatikana kwa msukumo mdogo na katika maeneo mengine huduma itatolewa kwa mgawo.

Ili kupunguza changamoto hii, DAWASA imekuwa ikitekeleza mpango wa kuhamisha maji kutoka katika vyanzo vyake vingine ikiwemo, mtambo wa Ruvu Juu, ili kuhudumia maeneo ambayo awali yalikuwa yakipata huduma kutoka katika mtambo wa Ruvu Chini. Aidha vyanzo vyake vingine vya mtambo wa Mtoni pamoja na visima virefu vinaendelea kutoa huduma katika maeneo mengine ya jiji ili kupunguza changamoto ilioyopo.

Kutokana na ukubwa wa mtandao wa DAWASA, ratiba za migawo zinatolewa kwa wananchi kupitia mifumo ya kimawasiliano ya Mamlaka kupitia mikoa yake ya kihuduma ili kuwafikiwa wananchi husika kwa kwa muda muafaka.

DAWASA inaendelea kuwakumbusha wateja na wananchi kwa ujumla kutunza/kukinga maji ya kutosha wakati wa mgawo na kutumia maji kwa uangalifu.


Tupigie kupitia kituo cha huduma kwa wateja 0800110064 na 0735 202121 (WhatsApp tu)

Imetolewa na
Kitengo cha Mawasiliano na Jamii - DAWASA
 
Wajenge bwawa la maji. Miji yote mikubwa duniani hupata maji toka kwenye reservoirs.
 
Hii Mambo ya upungufu wa maji mjini Dar haujawahi kuwepo, tukumbuke wameanza kucapture maji kwenye bwawa la umeme huo ndio ukweli na hizi ndio athari walizokuwa wanasema so tukubali tu kwamba sasa tumetaka umeme kwa sifa tujiandae kuchota maji wa zamu.
 
Hivi kama dawasa hawawezi kuwekeza kwenye desalination kuliko kutegemea maji ya mito ambayo muongo mmoja baadae itatokea kama mji wa Cape Town?!
 
Waziri wa maji anendelea na Komedy zake mikoani na vijiji vyenye watu elfu mbili huku jiji lenye watu million zaidi ya sita hana habari nalo.
Hopless kabisa
 
Hii Mambo ya upungufu wa maji mjini Dar haujawahi kuwepo, tukumbuke wameanza kucapture maji kwenye bwawa la umeme huo ndio ukweli na hizi ndio athari walizokuwa wanasema so tukubali tu kwamba sasa tumetaka umeme kwa sifa tujiandae kuchota maji wa zamu.
Maji ya dar yanatoka mto ruvu, mradi upo mto rufiji. Mbalimbali
 
Miaka nenda rudi wanategemea mto ruvu.

Kwamba hawajajiwekea utaratibu wa kuongeza vyanzo vya maji vipya kila baada ya miaka mitano?
 
Miaka nenda rudi wanategemea mto ruvu.

Kwamba hawajajiwekea utaratibu wa kuongeza vyanzo vya maji vipya kila baada ya miaka mitano?
Ndo hapo Sasa wakati hiyo ni biashara na inahitaji production kubwa Ili mapato yazidi kuongezeka na umuhimu wao uonekane Sasa hapo akipatikana mwekezaji wa visima vya maji Nchi nzima akapewa hiyo tenda na ajira zao zikakoma ndo unasikia kelele za Nchi kuuzwa, tuone ttcl walivyodorola wateja hawana, tunasikia na miradi ya bandari watu wanapiga kelele wakiogopa ajira zao kukoma baada ya kuleta mshindani, ifike sehemu tuambiane ukweli wafanyakazi wanaofanya kazi kwenye biashara za serikali wawe wabunifu haraka kama siyo njia mbadala zitakuja kuwaweka pembeni.
 
Simutenki
IMG-20211119-WA0053.jpg
 
Back
Top Bottom