Dawa ya kuondoa chelewa (hangover)

Dawa ya kuondoa chelewa (hangover)

Siku zote nimekua nikisumbuliwa na mning'inio siku ya 2 baada ya kutumia kilevi tafadhali anayejua tiba(sio kuacha utumiaji)anijuze..
Kunywa pombe kwa polepole....mfano 1Beer uinywe zaidi ya dakika 40.yani uwe unaweka interval ya dakika 40 kwa kila beer unayokunywa.
Pia chakula cha kushiba 30 minutes before beer.
Unywe kwa kuburudani......sio pupa pupa kama unakimbizwa.
 
Siku zote nimekua nikisumbuliwa na mning'inio siku ya 2 baada ya kutumia kilevi tafadhali anayejua tiba(sio kuacha utumiaji)anijuze..

Kunywa maji wakati unakunywa bia husaidia sana.Hushauriwa kila baada ya bia unywe maji walau kiasi sawa na ujazo wa bia,ni zoezi gumu lakini jaribu kiasi ambacho utakachoona hakikupi shida(tumbo kujaa kupita kiasi). Unywaji bia wa taratibu pia husaidia kama alivyoshauri madau hapo juu.
 
stay drunk! unapata hangover wakati pombe inaanza kuisha mwilini,actually unatengeneza sumu. sasa ukijiskia hangover,tundika pombe upyaa!
 
Kila unapokunywa beer nusu lita au chupa moja, unakojoa takribani chupa moja na robo hadi na nusu,hivyo unapunguza maji mwilini. Hii inakufanya uamke asubuhi na mning'inio. TIBA yake ni kunywa MAJI lita moja kila baada ya kupata KILAJI (pombe), asubuhi utaamka bila kukutana na MNING'INIO
 
Kila unapokunywa beer chupa 1 unakojoa takribani chupa 1.25 hadi 1.5,hivyo unapunguza MAJI mwilini. TIBA yake ni kunywa maji lita moja kila baada ya kupata kilaji(pombe), na asubuhi utaamka bila MNING'INIO
 
Dawa ya "hangover" ambayo ni bora kuliko zote. Ni kuacha kulewa.
 
dawa yake unaweza kushtua na mbili tena au ukanywa supu yenye pilipili nyingi na maji baridi au kula matikiti maji au oga na maji barid sana zote hizo ni dawa na nzuri kuliko zote ni kunywa kwa wastan usilewe sawa kijana
 
kunywa maji mengi ukishaamka tu kabla ya kupiga mswaki, kunywa kama lita moja, baada ya hapo kama unaweza fanya mazoezi utoke jasho kwa mda wa nusu saa hivi, hapo ukirudi ukioga utafikiri pombe ulikunywa wiki iliyopita.
 
dawa yake unaweza kushtua na mbili tena au ukanywa supu yenye pilipili nyingi na maji baridi au kula matikiti maji au oga na maji barid sana zote hizo ni dawa na nzuri kuliko zote ni kunywa kwa wastan usilewe sawa kijana
Mtaalam mmoja kanieleza sababu zote zilizotanjwa humu zinafanya kazi kama ukinywa bwaksi la kiasi vinginevyo dawa ni KULALA tena baada ya kuamka japo kwa masaa 3,hakuna fomula kamili ni USINGIZI tu
 
Wapwaz

Msaada wa kuondoa hangover! Jana baada ya kuona uchawi wa Genius Messi, nimejitunga kilaji na jamaa Mpaka asubuhi. Nipo Kama mgonjwa supu haipandi natamani kuendelea na unywaji. Dawa nifanyaje?
 
Mtaalam mmoja kanieleza sababu zote zilizotanjwa humu zinafanya kazi kama ukinywa bwaksi la kiasi vinginevyo dawa ni KULALA tena baada ya kuamka japo kwa masaa 3,hakuna fomula kamili ni USINGIZI tu

haya kijana endelea kulala kama kesho hukushndwa kwenda ofisin ukaamka na malaria au homa usiyo ielewa nini chanzo haya bana wewe lala tuu kumbe ndo unajifunza pombe kwa kupitia pombe za bure shaur yako kijana
 
Back
Top Bottom