maneno ya kafulila jana jioni hapa dodoma
" huu mjadala watu kukana hauna maana kabisa. wote wanaokana ndio wapiga debe wakubwa. waliyasema haya wanayoyakana. ni unafiki ndio unaowasumbua na uoga. kabla ya kuondoka, wote tulikaa pale sinza na kwa pamoja wakasema wanamuunga mkono, tukafika Kigoma wakarudia maeno yale yale ya kumuunga zitto. Iweje leo wanakana? Asilimia 85% ya wabunge wanamuunga mkono zitto kugombea urais. Wana kigoma tumeonewa sana. Muda umefika kuwepo usawa katika uongozi wa hii nchi. Hatuwezi kuwa wasindikizaji siku zote, wakati uwezo tunao. Tunaungwa mkono kila kona ya nchi na hata nje ya nchi, na kama ni demokrasia 2015 rais na makamu wake lazima watokee Kigoma. Rais wa Tanzania, Afrika Kusini, ujerumani na Malaysia wote wanataka umuona rais kijana Tanzania.Vyama vyote vya siasa humu nchini wanamtaka rais kijana, Kikwete mwenyewe anamtaka atakayemrithi awe kijana"
1.Inaelekea Taifa linakabiliana na ombwe la kiitikadi: sasa ni ukabila, ukanda na udini mtindo mmoja. Kwa mtindo huo miaka michache ijayo Tanzania haitakuwa na mshikamano wa utaifa ambao ndiyo umeiweka nchi yetu katika nafasi ya kuigwa na jamii zinazotuzunguka. Jitengeni na wanasiasa wanaotaka kuchochea ukabila, ukanda na udini.
2. Mwalimu alionya kuwa tuwaogope wanasiasa wanaotaka kuingia ikulu(kupata uongozi) kwa udi na uvumba. Wapuzeeni wote ambao wanaoutaka uraisi kwa sababu wengi wao wana uchu wa madaraka na ajenda za siri.
3. Naamini kuna Watanzania wengi wenye uzalendo na uwezo mkubwa wa kuitumikia nchi hii katika nafasi mbalimbali ukiwemo Uraisi. Lakini kawaida watu kama hao hawajitokezi mara moja. Wanahitaji kutambuliwa na kuhimizwa kujitokeza. Hivyo panueni wigo wa utafiti wa viongozi wanaofaa ndani ya vyama vya siasa katika ngazi mbalimbali-siyo tuu ngazi ya taifa. Pia tazama ndani ya serikali katika ngazi mikoa, wilaya , ubalozini, wizarani, vyuo vikuu nk. Tazama pia katika sekta mbalimbaili za kitaifa -wafanyabishara, asasi zisizo za kiserikali, majeshini nk.