David Kafulila ahamia CHADEMA akitokea NCCR Mageuzi

David Kafulila ahamia CHADEMA akitokea NCCR Mageuzi

Kaenda kwa mkewe, sioni kama ita muimarisha yeye kisiasa bali ita msaidia mkewe zaidi.

Halafu kama wote NCCR na CDM ni UKAWA kuna haja gani ya Kafulila kuhama!? Au ndio umoja wa mashaka wenyewe!!
Umuhimu wa yeye kurudi tena Chadema, muulize babu Duni kwa nini aliamua kurudi CUF kutoka CDM
 
Ndani ya ukawa kuna vyama vitainuka na vingine vitakufa au kumalizwa nguvu na vyama vilivyokuwa n nguvu zaidi c hivyo tu hata nje ya ukawa kuna vyama vitakufa eg act wazalendo
Ningelishangaa ukashindwa kutaja chama kinacokunyima usingizi
 
Kafulila meoyesha ukomavu wa kisiasa, hope na wengine watatambua kuacha kutumika kugawa nguvu ya upinzani
Kafulila ahama NCCR, ahamia Chadema
Dar es Saam. Mbunge wa zamani wa Kigoma Kusini, (NCCR-Mageuzi) David Kafulila, amekihama chama hicho huku akieleza kuwa anajiandaa kuhamia Chadema.

Kafulila alithibitisha taarifa hizo na kusema tayari ameshawasilisha barua ya kujivua uanachama wa NCCR na kujiunga Chadema leo.

“Nimewashukuru kwa kuwa pamoja katika kujenga chama na nafasi ya uenezi waliyonipa mara zote. Nimeweka wazi kuwa natarajia kujiunga na Chadema. Nimeona kuwa kuna mahitaji ya watu wenye nia ya mabadiliko kuwa katika chama kimoja ili kufupisha safari.” alisema

View attachment 446944

SOURCE: Mwananchi

Kabla ya NCCR, Kafulila alikuwa mwanachama wa CHADEMA. Habari. zaidi soma=>David Kafulila ahamia NCCR Mageuzi akitokea CHADEMA
 
Hana pakula sasa inabidi awe anamfata mkewe popote alipo kwenye siasa asa za chadema
Hiyo inaitwa kula kulala kwa mke.Njaa mbaya.Hakuna kazi ngumu kwa mwanamke kama kazi ya kulisha dume.Pole sana mama kafulila zigo hilo unalo.
 
Machali CCM -Msaliti
Kafulila CDM - Shujaaa
(alikuwa ukawa kahamia ukawa) vyama vingine zindukeni mmeliwa
 
Kafulila alikuwa mahali ambako sio penyewe, uwezo wake ulijengwa na CDM na alikokimbilia hakuwa na nafasi ya kuonwesha uwezo alio nao. na jinsi CDM ilivyo na nguvu kama angegombea kwa tiketi ya CDM asingeshindwa. anahitaji mahali penye nguvu kama za kwake. ni lazima tukiri kwamba chama kama hakina nguvu ni hakina nguvu huwezi kukilazimisha na ndio maana system inatumia nguvu kubwa sana kupambana na chama kama CDM. kafulila anarudi Bungeni 2020,
 
hata mbatia mwenyewe anajua, na ubunge asingeweza kuupta kama sio CDM waliompa jimbo, kumbana na CCM na Mrema Vunjo sio kazi ndogo, na unajua kwa Vunjo Mbatia alitambulishwa na Mrema wakati wakiwa NCCR wote na akampigania Mbatia akawa Mbunge, wakati huo ilikuwa vigumu sana kwa Mtu kuwa Mbunge wa Moshi Vijijini au Vunjo kama Augustino Mrema hajakupeleka kukutambulisha. kwahiyo Mbatia mwenyewe hawawezi kupambana na Mrema bila nguvu kubwa kama ya UKAWA
 
People's Power

Strength in Number

Umoja ni

Ukawa si chama, wanasiasa wa Upinzani Pazia limefunguliwa na Kafulila. Tuna matumaini mtazika tofauti, kuyasahau yaliyopita na wote hata ACT kujiunga CDM
 
Wasalaam;
Mbunge wa zamani wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi) mh. David Kafulila amekihama chama hicho rasmi.

Kafulila asema tayari ameshawasilisha barua ya "kujivua" uanachama wa NCCR-Mageuzi na yuko tayari kujiunga na Chadema.

"Nimeweka wazi kuwa natarajia kujiunga na Chadema" Kafulila alisema

"Nimeona kuwa kuna mahitaji ya watu wenye nia ya mabadiliko kuwa katika chama kimoja ili kufupisha safari" Kafulila aliongeza
 
Back
Top Bottom