DART kuleta mabasi mapya 95 ya mwendokasi

John Haramba

JF-Expert Member
Feb 4, 2022
365
1,373
Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) umesema mwaka huu utaongeza mabasi mengine mapya 95 ikiwa ni sehemu ya hatua za kupunguza msongamano wa abiria kwenye vituo vya mabasi hayo.

Mtendaji Mkuu wa Wakala huo, Dk. Edwin Mhede alibainisha hayo jana wakati akifungua mafunzo kuhusu mipango ya mitaa kwa Jiji la Dar es Salaam.

Alisema wakala ulijitahidi kuongeza mabasi 70 hivi karibuni kwa ajili ya kupunguza msongamano huo lakini kutokana na wananchi wengi kuchangamkia usafiri huo, mahitaji yanaendelea kuongezeka.

Alisema zamani abiria alilazimika kusubiri basi kwa dakika 30 lakini walipoongeza mabasi 70, muda huo ulipungua na kufikia dakika tano na kwamba mpango uliopo unalenga kuondoa hata hizo dakika tano ili abiria akifika tu apande basi na kwenda anakotaka.

“Kabla ya mwisho wa mwaka huu tunakusudia kuongeza mabasi mengine mapya 95 na tunaamini kwa kufanya hivi tutaondoa kabisa muda wa kusubiri kwa sababu maana ya kuwapo kwa mabasi haya ni watu kuwahi makazini," alisema.

Dk. Mhede alisema ujio wa mabasi hayo pia utapunguza kawaida ya watu kukimbizana kupanda mabasi, hali ambayo imekuwa ikisababisha ajali kwenye vituo hivyo kutokana na watu kukanyagana au kugongwa na mabasi.

Aliwaomba wananchi kuacha tabia ya kukatisha kwenye njia za DART kwa kuwa si salama kwao na kwa mabasi, akionya kuwa wananchi wengi wamekuwa wakipata majeraha wanapokatisha kwenye njia hizo.

“Hakuna haja ya kukimbilia basi, ukakatisha njia ya UDART uwezekano wa kugongwa ni mkubwa. Sasa ni muhimu ukazingatia usalama wako kwanza kabla ya kuchukua uamuzi wa kukatisha kwenye njia hizo,” alionya Dk. Mhede.

Kiongozi huyo pia alisema wakazi wa Kigamboni wajiandae kupokea huduma hiyo kwa kuwa fedha za kujenga mradi huo kuelekea maeneo yao zimeshapatikana na kinachosubiriwa ni utekelezaji wa mradi.

Alisema ujenzi wa DART kuelekea Kigamboni utafanywa kwenye awamu ya tano, akidokeza kuwa ziara za Rais Samia Suluhu Hassan nje ya nchi zimefanikisha upatikanaji wa fedha kwa ajili ya kugharamia mradi huo kwa awamu ya tano.

Alisema ujenzi wa mradi huo kuelekea Kigamboni utapitia kwenye Daraja la Nyerere na maandalizi kwa ajili ya utekelezaji wake yanaendelea vizuri.

DART kwa kushirikiana na Shirika la Makazi Duniani (UN- HABITAT) na Taasisi ya Usafiri na Maendeleo (ITDP), wameandaa mafunzo hayo ya siku mbili kwa ajili ya watumishi wanaohusika na mipango miji na mitaa ya Jiji la Dar es Salaam.


Source: Nipashe

mabasi.jpg
 
Utayakuta yamepaki vituoni yanaunguruma tu huku abiria wakiwa wamejaa tu kwenye foleni hawaelewi wanaondokaje.. Unaeza ukasimama kwenye foleni ya kupanda mwendokasi, ukaunga bando labuku, ukatumia na adi likaisha ukiwa bado kwenye foleni huku unaona mabasi yanakuja yanapaki madereva wanashuka sijui wanaendaga wapi na kufanya nn?
 
Japo yanafanya vyema ila kuna mida huwa yanazingua sana. Mfano wakati wa saa sita kwenda saa saba hali ni mbaya sana. Utakuta mpo kituoni foleni kubwa na bado mabasi yamepaki yanaunguruma tu.
Ni bora kama madereva wanabadilisha shift basi yule anayechukua shift afike nusu saa kabla ili dereva anayemaliza shift akishuka tu, basi mwingine achukue zamu.
Pia pale kimara ticketi za kwenda mbezi waongeze dirisha la kukatia ticketi maana hali huwa inakuwa ngumu sana wakati wa kukata ticketi za mbezi
Pamoja na yote, huduma imeimarika kwa sasa, ambapo at least unakuwa na uhakika wa kuondoka mapema.
 
Hivi nikwa nini hakuna ofisi ya meneja kwenye vituo vikubwa wanaotumia redio call kuwasiliana mfano mmoja awe gerezani, morocco, kivukoni, ubungo,kimara na mbezi kuhakikisha abiria hawaendelei kupoteza mida kisubiria mabasi ilihali yanakuja na kusimama bila kuondoka na abiria na wale madereva saa hizo wanajiona wa maana kumbe hakuna lolote. Yaani sioni tofaiti na madereva wa daladala wanavyokuwa na nyodo hasa mida wa jioni abiria wanavyohangaika vituoni.
 
Yaliopo tu nina uhakika yote yangekua barabarani Huo mrundikano unao ongelewa usinge kuwepo

Mnaongeza ma bus ambayo najua mnakuja yaendesha wiki 1 tu kwa ajili ya show off wiki zingine zote

ma bus yatakua yanapaki kwa visingizio chungu nzima,Huu mradi sio mwepesi kama mnavyotuaminisha hapa

nyie tu ongezeni ma bus yenu ila kuhusu swala la kukaa muda mrefu kituoni,kuliondoa labda Arudi JPM leo ila sio kwa awamu hii ya MAMA.
 
Dart Mnasaidia sana usafiri kwa watu wasio na haraka yani Hana Akimbiliapo,

ila kwa ambao kupoteza dk 5 ni kosa la jinai Huo mradi wenu sio wakushobokewa

maana unaweza jikuta umetukana matusi yoteeee
 
Mabasi yaliyopo tu sasa hivi yanatosha sana ila utaratibu wao ni mbovu mno. Yaani hawajui hata muda gani abiria ni wengi waingize mabasi barabarani. Yaani ni kama vile ndio wanaanza biashara leo. Unakuta abiria wamejaa vituoni lakini mabasi yapo matupu yamepaki tu yananguruma Kimara, Ubungo, Jangawani na Gerezani. Kama wangekuwa na mpangilio mzuri kusingekuwa na haja ya kuagiza hayo mengine sasa hivi labda mpaka njia ya Mbaga itakapokamilika.
 
Yaje na mataa yale ya kuwaka usiku...kuna moja hivi basi zima linawaka taa aisee ukikutana nalo usiku vibe lake ni so fantastic utasema tupo Atlanta
 
Kigamboni yaende Mpaka Pemba mnazi na Buyuni huko.Sio yanaishia Fery tumefika Kigamboni ela manakula.
 
Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) umesema mwaka huu utaongeza mabasi mengine mapya 95 ikiwa ni sehemu ya hatua za kupunguza msongamano wa abiria kwenye vituo vya mabasi hayo.

Mtendaji Mkuu wa Wakala huo, Dk. Edwin Mhede alibainisha hayo jana wakati akifungua mafunzo kuhusu mipango ya mitaa kwa Jiji la Dar es Salaam.

Alisema wakala ulijitahidi kuongeza mabasi 70 hivi karibuni kwa ajili ya kupunguza msongamano huo lakini kutokana na wananchi wengi kuchangamkia usafiri huo, mahitaji yanaendelea kuongezeka.

Alisema zamani abiria alilazimika kusubiri basi kwa dakika 30 lakini walipoongeza mabasi 70, muda huo ulipungua na kufikia dakika tano na kwamba mpango uliopo unalenga kuondoa hata hizo dakika tano ili abiria akifika tu apande basi na kwenda anakotaka.

“Kabla ya mwisho wa mwaka huu tunakusudia kuongeza mabasi mengine mapya 95 na tunaamini kwa kufanya hivi tutaondoa kabisa muda wa kusubiri kwa sababu maana ya kuwapo kwa mabasi haya ni watu kuwahi makazini," alisema.

Dk. Mhede alisema ujio wa mabasi hayo pia utapunguza kawaida ya watu kukimbizana kupanda mabasi, hali ambayo imekuwa ikisababisha ajali kwenye vituo hivyo kutokana na watu kukanyagana au kugongwa na mabasi.

Aliwaomba wananchi kuacha tabia ya kukatisha kwenye njia za DART kwa kuwa si salama kwao na kwa mabasi, akionya kuwa wananchi wengi wamekuwa wakipata majeraha wanapokatisha kwenye njia hizo.

“Hakuna haja ya kukimbilia basi, ukakatisha njia ya UDART uwezekano wa kugongwa ni mkubwa. Sasa ni muhimu ukazingatia usalama wako kwanza kabla ya kuchukua uamuzi wa kukatisha kwenye njia hizo,” alionya Dk. Mhede.

Kiongozi huyo pia alisema wakazi wa Kigamboni wajiandae kupokea huduma hiyo kwa kuwa fedha za kujenga mradi huo kuelekea maeneo yao zimeshapatikana na kinachosubiriwa ni utekelezaji wa mradi.

Alisema ujenzi wa DART kuelekea Kigamboni utafanywa kwenye awamu ya tano, akidokeza kuwa ziara za Rais Samia Suluhu Hassan nje ya nchi zimefanikisha upatikanaji wa fedha kwa ajili ya kugharamia mradi huo kwa awamu ya tano.

Alisema ujenzi wa mradi huo kuelekea Kigamboni utapitia kwenye Daraja la Nyerere na maandalizi kwa ajili ya utekelezaji wake yanaendelea vizuri.

DART kwa kushirikiana na Shirika la Makazi Duniani (UN- HABITAT) na Taasisi ya Usafiri na Maendeleo (ITDP), wameandaa mafunzo hayo ya siku mbili kwa ajili ya watumishi wanaohusika na mipango miji na mitaa ya Jiji la Dar es Salaam.


Source: Nipashe

View attachment 2144465
DART iko na business nzuri sana, wateja kama wote and their market is extensible too, inashangaza sana kusikia na DART nayo inapta hasara.
 
Utayakuta yamepaki vituoni yanaunguruma tu huku abiria wakiwa wamejaa tu kwenye foleni hawaelewi wanaondokaje.. Unaeza ukasimama kwenye foleni ya kupanda mwendokasi, ukaunga bando labuku, ukatumia na adi likaisha ukiwa bado kwenye foleni huku unaona mabasi yanakuja yanapaki madereva wanashuka sijui wanaendaga wapi na kufanya nn?
Mtu we management anakwama sana linaweza kuja basi likaondoka tupu na watu wamejaa kituoni. Sijui manager route anamanage vipi maana huwa sielewi kabisa.
 
Mtu we management anakwama sana linaweza kuja basi likaondoka tupu na watu wamejaa kituoni. Sijui manager route anamanage vipi maana huwa sielewi kabisa.
Kuna kuwa na driver exchange hasa wakati wa mchana na kubadirishana ni mpaka ulipeleke pale jangwani ukasign out kwa bus kukaguliwa.

Hiyo inaepusha kumuuzia mwenzako kesi kwa kumpa juu kwa juu kumbe uligonga au lina itilafu.

Tofauti na mnavyofanya kwenye daladala zenu.
 
DART iko na business nzuri sana, wateja kama wote and their market is extensible too, inashangaza sana kusikia na DART nayo inapta hasara.
Elimu.
Watanzania wanasoma ili kupasi mitihani.
Kuna tofauti kubwa Sana Kati ya mtu aliyesoma na mtu mwenye akili.
MTU anaweza kua na Master's degree ya uchumi/commerce/ transportation and transport management lkn ka mradi kadogo Kama DART kanamshinda kuendesha huku abiria wako wakumwaga.
Hapo hapo Kuna wazee wenye mabasi ya mikoani au wenye daladala mpaka Mia .abiria wakugombania , hawana hata certificate ya transport MGMT lkn kampuni zao zinapata faida na Kodi ya serikali wanalipa.
 
Back
Top Bottom