Mangisandy
JF-Expert Member
- Apr 23, 2012
- 2,644
- 2,273
Ni kweli kwamba tuna mihimili mitatu, lakini siyo kweli kwamba serikali ni top over watu! Siyo tu Mbunge Hata wewe, raisi Magufuli ameomba Kazi ya uraisi ili awatumikie wananchi!Tuna mihimili mikuu mitatu kiuongozi kwa mujibu wa Katiba ya JMT. Utawala, Mahakama na Bunge.
Muh. Rais ndiye kiongozi mkuu wa utawala. Vilevile ndiye msimamizi mkuu wa mahakama na bunge. Jaji mkuu na Spika wako chini yake. Kimkoa na kiwilaya, Rais anawakilishwa na Wakuu wa Mikoa pamoja na Wakuu wa Wilaya.
Wakuu Wa wilaya, wakuu Wa mikoa hata ulaya na marekani wapo. wabunge kote duniani siyo viongozi Wa kiutendaji (executive).
Nchi zote zina executive, judiciary na legislature. Katika kila nchi executive (Rais na wasaidizi wake) ndiyo watekelezaji Wa sheria kiuongozi. Marekani magavana (tuwaite wakuu Wa mikoa na wilaya) wana nguvu sana kiutendaji.
Licha ya kubenea kuwa mbunge alipaswa kumheshimu Mkuu Wa wilaya Bila kubishana nae hadharani au kumtukana. Alimuita mhuni na kibaka hadharani.
Makonda ili kuhifadhi ushahidi, aliamua kuteka video camera ya startv ili ushahidi Wa matusi aliotukanwa usifutwe.
Jiweke ktk nafasi ya makonda. Rais Wa wilaya kutukanwa hadharani. Ikumbukwe kuwa makonda alikua ameahidi kumpeleka waziri kiwandani Leo.
Kiprotokali baada ya makonda kuongea na wafanyakazi, kubenea hakua na haki ya kutaka kuongea baada ya DC. DC aliogopa kuwa maneno ya kubenea yanaweza chafua hali ya hewa ambayo ilikua imetulia.
Tabia ya kijeuri ya kubenea aliionesha siku ya kufungua bunge alipomuomba Kange lugola kufuta maneno yke. Alitumia lugha ya kibabe sana Bila ulazima. Kubenea ajue kuwa kinga anayo bungeni siyo uraiani (executive) kwa akina makonda.
Tuweke siasa kando. Tuseme ukweli. Katiba ya 1977 ndiyo ituongoze hata kama INA mapungufu. Sheria n msumeno
Hicho kitu unacho sema kipo Marekani, umekosea. Kule mamlaka zinaheshimiana. Pia, mamlaka siyo mtu, ni taasisi ambayo imepewa mamlaka na watu kwa mujibu wa katiba. Umesema tuache USHABIKI wa kisiasa tuangalie ukweli ila jiangalie, hata wewe umeonyesha ushabiki mkubwa Sana Kwa Makonda! Kazi yake, Makonda, ni kusimamia Sheria
Tujiulize kilichomsukuma kumweka Kubenea ni kuchukua matusi au ni Yeye kutukanwa? Wewe hapo ukimtukana Mtu yeyote atakuweka ndani? Siku zote alipokua anamwita Lowasa fisadi, aliwekwa ndani na nani? Makonda hayupo juu Ya sheria na hana mamlaka ya kuamuru mtu yeyote awekwe ndani, amevunja sheria kwa kuvuka mipaka ya kazi yake.