Daraja la Mzinga lakatika

Daraja la Mzinga lakatika

Nimefurahi sana kuliona STK linakuwa la kwanza kuionja adha ya ujenzi wa miundombinu chini ya kiwango!

Uko sahihi kuwaza hivyo. Ila kaa ukijua kodi yako itanunua stk nyingine mpya na ya kisasa zaidi ya hiyo. Tafakari, chukua hatua!
 
Habar wanajamvi, kama unatumia barbara ya mbagala - kongowe pale mzinga darajani hakuna njia kutokana na daraja hilo kuvunjika
NAWASILISHA
 
Leta basi picha kama wenzako walivyoleta jana kuhusu daraja la Bagamoyo au leo lile la Ruvu.
 
serikali na wananch washirikiane kutatua hilo swala ili kunusur ajari
 
Hivi hazina pakoje kwa sasa?

Kitengo cha maafa?

Maana tutaanza kampeni za kuomba misaada wa wafanyabiashara na baadae wakwepe kodi na tuwaonee aibu
 
...nilisikia ni lile la njia ya kigamboni,tujuze vyema mkuu maana wengine yanatuchanganya hili la mbagala mwisho kabla ya kituo cha mzinga....
 
Wabunge 620 wa bunge la katiba X siku 90 X shs 300,000 kwa siku ni sawa na tshs billioni 16.8. Hizi ni sawa na barabara ya lami ya km ngapi?

Mamdogo nafikiri kwa hesabu za kifisadi hatupati hata 50
 
...nilisikia ni lile la njia ya kigamboni,tujuze vyema mkuu maana wengine yanatuchanganya hili la mbagala mwisho kabla ya kituo cha mzinga....

Ukitokea mbagala kwenda kongowe kna daraja la mzinga lile limebomoka ingawa sio lote ila magari hayapiti. Pia ukitoka kongowe kwenda kigamboni kuna daraja pale limebomoka lote. Watu wa kongowe hawana mawasiliano pande zote mbili.
 
tatizo tumekuwa watu wa kujishughulisha na matatizo, badala ya kuzuia yasitokee ayo matatizo. kitengo cha maafa sijui kinazuia nini.
 
Back
Top Bottom