Daraja la mto Mkondoa ,Dumila: Tatizo ni kubwa sana!

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Oct 20, 2014
15,327
24,209
1548058130698.png

Majuzi mto Mkondoa umepita juu ya daraja pale Dumila.
Hii si mara ya kwanza, kama sikosei ni karibia ya nne hivi.
Na mara zote tuta la barabara linachukuliwa.

Kina cha mto kwa sasa hivi ni mita moja na nusu hadi mbili hivi.

Nimepita hapo miaka ya 1990, kina cha juu cha maji nilikuona ni karibia mita 8 au zaidi.

Nini kimetokea?


EROSION au mmomonyoko wa ardhi unaleta udongo mwingi sana tokea sehemu za nyanda za juu kuliko na ukulima usio na weledi.

Sasa hivi pale darajani kuna mchanga wenye kina cha zaidi ya mita 6!

Kwa hiyo tatizo ni kubwa kuliko linanavyofikiriwa.
Solution yangu ni hii:

1. Mikoa ya Morogoro, Dodoma, Tanga na Arusha inayopakana na mto Mkondoa ,wasimamie kwa karibu sana ukulima bora usioendeleza mmomonyoko wa ardhi.

2. Kwa karibia kilometa 4, toka Dumila kuelekea kale kapori karibu na Gereza, tuta la barabara linyanyuliwe si chini ya mita 4 ikiwa ni pamoja na kuongeza ma culvert ya kutosha.

3. Hili si tatizo la TANROADS peke yao, ni tatizo la kitaifa.

4. Mchanga pale mtoni ni mali. Mchangabunaweza kuvunwa kwa winhi sana nabkusagirishwa hadi Dar au Zanzibar , sehemu zenye uhaba mkubwa wa mali asili hiyo.

Nawasilisha.
 
Lile daraja wamelijenga chini sana waangalie madaraja mengine yalivyojengwa juujuu mfano lile la rufiji.
Kwa utatuzi wa muda mfupi nahisi wachimbe chini kuondoa michanga ili maji yapite chini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo la daraja la dumila ni pale mamlaka husika zinapokataza kutoa ule mchanga uliopo Chini ya daraja ambapo ingesaidia Sana kupatikana kwa kina na maji yasingepita juu ya daraja

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu pale hua kuna mchanga mwingi sana kiasi cha distance kati ya daraja na ardhi kuwa ndogo mara kwa mara, hivyo mvua kidogo tu inatosha kupajaza maji kiasi cha kupita juu ya daraja. Hata ukiangalia leo palivyo utaona pako na kifusi kikubwa sana pale cha mchanga..

1. Kuwa na routine program za kuondoa mchanga kwa kutumia excavator ili daraja hilo hilo liendelee kutumika.
2. Kulinyanyua daraja juu sana na chini kuwe na nguzo tu za kutosha....
 
Mkuu pale hua kuna mchanga mwingi sana kiasi cha distance kati ya daraja na ardhi kuwa ndogo mara kwa mara, hivyo mvua kidogo tu inatosha kupajaza maji kiasi cha kupita juu ya daraja. Hata ukiangalia leo palivyo utaona pako na kifusi kikubwa sana pale cha mchanga..

1. Kuwa na routine program za kuondoa mchanga kwa kutumia excavator ili daraja hilo hilo liendelee kutumika.
2. Kulinyanyua daraja juu sana na chini kuwe na nguzo tu za kutosha....
Ni kweli kabisa mkuu.
Draja hili lilijengwa wakati huo mvua zilikuwa hazibebi udongo.Sasa hivi hali imebadilika sana, iabidi wataalam wetu nao wabadilike.
Naonyesha ramani ya Dumila ilivyo na madhara ya mvua kwenye daraja hilo.
1548058462230.png


Kwa hii google map, twaweza kuona jinsi daraja lilivyo songa mto,na jinsi lilivyo dogo.
Pili mchanga umetapakaa kila mahalikuonyesha kuwa kuna sand deposition kubwa tu.
 
View attachment 1000953
Majuzi mto Mkondoa umepita juu ya daraja pale Dumila.
Hii si mara ya kwanza, kama sikosei ni karibia ya nne hivi.
Na mara zote tuta la barabara linachukuliwa.

Kina cha mto kwa sasa hivi ni mita moja na nusu hadi mbili hivi.

Nimepita hapo miaka ya 1990, kina cha juu cha maji nilikuona ni karibia mita 8 au zaidi.

Nini kimetokea?


EROSION au mmomonyoko wa ardhi unaleta udongo mwingi sana tokea sehemu za nyanda za juu kuliko na ukulima usio na weledi.

Sasa hivi pale darajani kuna mchanga wenye kina cha zaidi ya mita 6!

Kwa hiyo tatizo ni kubwa kuliko linanavyofikiriwa.
Solution yangu ni hii:

1. Mikoa ya Morogoro, Dodoma, Tanga na Arusha inayopakana na mto Mkondoa ,wasimamie kwa karibu sana ukulima bora usioendeleza mmomonyoko wa ardhi.

2. Kwa karibia kilometa 4, toka Dumila kuelekea kale kapori karibu na Gereza, tuta la barabara linyanyuliwe si chini ya mita 4 ikiwa ni pamoja na kuongeza ma culvert ya kutosha.

3. Hili si tatizo la TANROADS peke yao, ni tatizo la kitaifa.

4. Mchanga pale mtoni ni mali. Mchangabunaweza kuvunwa kwa winhi sana nabkusagirishwa hadi Dar au Zanzibar , sehemu zenye uhaba mkubwa wa mali asili hiyo.

Nawasilisha.
Sijui kama wasomi wetu mawizarani wamelidadavua tatizo hili.
Kwa picha linaonekana dhahiri.
 
Kama zilivyo barabara, mito pia inahitaji matunzo na ukarabati wa kingo zake ikiwemo kuondoa tope na mchanga unaojaa kufuatia mmomonyoko wa ardhi. Vifa vya namna hiyo kama yalivyo matrekta, vijiko na winchi vinapatikana kwenye masoko ya mitambo ya kujenga miundombinu. Nadhani ni kitu kigeni kwetu na ndio maana mito yetu karibu yote haijawahi kufanyiwa usomaji wa ramani zake na kuhifadhi taarifa zake.

Eneo la Dumila liko bondeni na hata daraja lenyewe liko chini sana kiasi kwamba, siku moja mvua zikizidi sana tutashuhudia gharika katika eneo zima. Barabara hiyo inahitaji kuinuliwa kwa kutengeneza tuta litakalo weza kujengwa barabara na daraja linalopitika muda wote.
 
Ni kweli kabisa mkuu.
Draja hili lilijengwa wakati huo mvua zilikuwa hazibebi udongo.Sasa hivi hali imebadilika sana, iabidi wataalam wetu nao wabadilike.
Naonyesha ramani ya Dumila ilivyo na madhara ya mvua kwenye daraja hilo.
View attachment 1000959

Kwa hii google map, twaweza kuona jinsi daraja lilivyo songa mto,na jinsi lilivyo dogo.
Pili mchanga umetapakaa kila mahalikuonyesha kuwa kuna sand deposition kubwa tu.

Nashukuru mkuu kwa kushare hii picha, inaonekana clear kabisa hiyo sand deposite na watu hapa wanahitaji kufikiri na kuja na permanent solution maana hilo daraja ni kiungo muhimu sana, Tatizo la sand deposit lipo kwenye madaraja mengi sana muhimu Tanzania mfano mwingine ni pale mpakani mwa DSM na PWANI bagamoyo road inaonekana dhahiri kabisa ipo siku tutaongea mengine... Gharama ya excavation for 10 years inaweza kabisa kutosha kutafuta suluhu la kudumu na kama kusafisha ukawa unatumia Gharama kidogo sana.

Kuna uwezekano kabisa wakuweka kitu kama filter umbali kidogo na maji yanapotoka na mchanga wote ukaishia huko na hapo darajani yakaja maji tu. Kwa kipindi fulani mvua ikikata watu wanaruhusiwa kuvuna huo mchanga kwa matumizi mengine.
 
View attachment 1000953
Majuzi mto Mkondoa umepita juu ya daraja pale Dumila.
Hii si mara ya kwanza, kama sikosei ni karibia ya nne hivi.
Na mara zote tuta la barabara linachukuliwa.

Kina cha mto kwa sasa hivi ni mita moja na nusu hadi mbili hivi.

Nimepita hapo miaka ya 1990, kina cha juu cha maji nilikuona ni karibia mita 8 au zaidi.

Nini kimetokea?


EROSION au mmomonyoko wa ardhi unaleta udongo mwingi sana tokea sehemu za nyanda za juu kuliko na ukulima usio na weledi.

Sasa hivi pale darajani kuna mchanga wenye kina cha zaidi ya mita 6!

Kwa hiyo tatizo ni kubwa kuliko linanavyofikiriwa.
Solution yangu ni hii:

1. Mikoa ya Morogoro, Dodoma, Tanga na Arusha inayopakana na mto Mkondoa ,wasimamie kwa karibu sana ukulima bora usioendeleza mmomonyoko wa ardhi.

2. Kwa karibia kilometa 4, toka Dumila kuelekea kale kapori karibu na Gereza, tuta la barabara linyanyuliwe si chini ya mita 4 ikiwa ni pamoja na kuongeza ma culvert ya kutosha.

3. Hili si tatizo la TANROADS peke yao, ni tatizo la kitaifa.

4. Mchanga pale mtoni ni mali. Mchangabunaweza kuvunwa kwa winhi sana nabkusagirishwa hadi Dar au Zanzibar , sehemu zenye uhaba mkubwa wa mali asili hiyo.

Nawasilisha.
Vijana wa Dumila wako tayari kuchota mchanga ulio chini ya daraja kwa usimamizi wa wataalam bahati mbaya Tanroad hawataki! Tanroad wako tayari kuona daraja linaziba kabisa kuliko kuruhusu uchotaji wa mchanga kina kiongezeke!
 
Vijana wa Dumila wako tayari kuchota mchanga ulio chini ya daraja kwa usimamizi wa wataalam bahati mbaya Tanroad hawataki! Tanroad wako tayari kuona daraja linaziba kabisa kuliko kuruhusu uchotaji wa mchanga kina kiongezeke!
Matokeo ya kutoondoa mchanga kwa miaka mingi ndiyo tunayaona sasa.
Watu wana postpone tatizo na wanafikiri litaondoka lenyewe.
 
Nashukuru mkuu kwa kushare hii picha, inaonekana clear kabisa hiyo sand deposite na watu hapa wanahitaji kufikiri na kuja na permanent solution maana hilo daraja ni kiungo muhimu sana, Tatizo la sand deposit lipo kwenye madaraja mengi sana muhimu Tanzania mfano mwingine ni pale mpakani mwa DSM na PWANI bagamoyo road inaonekana dhahiri kabisa ipo siku tutaongea mengine... Gharama ya excavation for 10 years inaweza kabisa kutosha kutafuta suluhu la kudumu na kama kusafisha ukawa unatumia Gharama kidogo sana.

Kuna uwezekano kabisa wakuweka kitu kama filter umbali kidogo na maji yanapotoka na mchanga wote ukaishia huko na hapo darajani yakaja maji tu. Kwa kipindi fulani mvua ikikata watu wanaruhusiwa kuvuna huo mchanga kwa matumizi mengine.
Ni kwelli mkuu.
Hili suala la sand deposits limeingiliwa na jamaa wa Mazingira NEMC, ambao hawajui lolote juu ya jiografia na tabia za mito.

Kukataza kuondoa michanga itokanayo na mmomonyoko wa ardhi upstream ni kielelezo cha kutoelewa tabia za mito na matatizo yake.

Kutokana na NEMC kuingilia mambo wasiyojua ndo tunapata matatizo ya kuzolewa tuta la barabara.

Kama mkuu ulivyoona matatizo hayo yametokea:
1. Daraja la Mpiji
2. Daraja la mto Mbezi, kwa Malecela
3. Daraja la Mkondoa , hapo Dumila(sasa ni mara ya nne takriban)
4. Mto Mbezi kule Morogoro rd , mwaka jana.

Mifano ni mingi nchini, wataalam wajifunze kutokana na tabia nchi, wasisubiri wazungu wawafundishe.
 
Back
Top Bottom