Daraja la kati ni wale waendesha ma-baloon - Dr. Jakaya Kikwete

Kweli naamini kabisa kuwa mheshimiwa haelewi kwa nini Tanzania ni maskini, ishu hapa sio waendesha ma-baloon bali ni uongozi mmbaya wenye rushwa na usioheshimu demokrasia (siasa safi).

Ili nchi yeyote ile iendelee inahitaji Ardhi, Watu na uongozi bora (siasa safi), TZ tuna Ardhi ya kumwaga, watu kibwena ila tatizo ni Uongozi....
.

Mkuu with all due respect for your views, hakuna tena nasisitiza HAKUNA uhusiano wowote kati ya nchi kuendeshwa kidemokrasia (siasa safi) na maendeleo ya kiuchumi. Hakuna tafiti yoyote iliyothibitisha kuwa democratic countries zinapata maendeleo ya kiuchumi zaidi ya zile nchi ambazo zinakandamiza demokrasia.

Mifano michache ya nchi zilizoendelea na demokrasia yake inatia shaka ni China, Singapole, Indonesia. Hata ukiangalia jirani zetu Ruanda wao wana record higher economic growth every year more than Tanzania wakati kidemokrasia tuko juu zaidi yao!!
 
thats our president, tena anajinasibu as msomi wa uchumi. Nadhani kama kuna mtu ambaye angesikitika na umaskini wa TZ ni yeye kwa kupata exposure ya kutosha akiwa waziri wa mambo ya nje na safari alizozifanya zisizo na tija mwanzoni wa uraisi wake. Kama kweli ni mtu kujiofunza kwa wengine angesikitika na uamsikini wa taifa lake
 
Jana nilikuwa naangalia taarifa ya habari TBC nikamuona Mh.Dr.Dr.Kikwete akizindua rasmi awamu ya pili ya mpango wa elimu ya sekondari katika kutekeleza MDGs.

Katika hotuba yake alisisitiza kuwa ili nchi yeyote ile duniani iendelee kimaendeleo inahitaji watu wa daraja la pili...na kwa Tanzania watu hao ni wale waendesha ma-baloon na wenye elimu ya sekondari.....

Kweli naamini kabisa kuwa mheshimiwa haelewi kwa nini Tanzania ni maskini, ishu hapa sio waendesha ma-baloon bali ni uongozi mmbaya wenye rushwa na usioheshimu demokrasia (siasa safi).

Ili nchi yeyote ile iendelee inahitaji Ardhi, Watu na uongozi bora (siasa safi), TZ tuna Ardhi ya kumwaga, watu kibwena ila tatizo ni Uongozi....

Mheshimiwa wake up, tabaka la kati sio waleta maendeleo, bali sera safi, na uongozi bora ndo kitu muhimu kwa sasa...hayo mabaloon yasikufanye uamini kuwa Wa-Tz wameendelea, zaidi ya asilimia 87 ya Watanzania wanaganga njaa kupindukia.
Amen, Kweli kabisa.:frusty:
 
...mabaloon haya watu wengi wamekopeshwa na mabenk yameona kwamba wanakopesheka, hivyo watu hawa wakiwa wengi kuweza kukopa uchumi utakua kwani uwekezaji utapanuka na ajira kuwa nyingi nchini....nakubaliana na mheshimiwa rais asilimia 100...ila kwa watu wenye upeo mdogo ni vigumu kumuelewa.
Kitakachokuza uchumi na ustawi wa nchi ni mikopo itakayoingia kwenye uzalishaji sio kununua mabaloon. Mtu anapochukua mkopo na kununua baloon anakuza uchumi na ajira za huko anakonunua baloon.

Tungekuwa na kiwanda cha kutengeneza hizo baloon tungestahili kutoa 'comment' kama hii! Tofauti na hivyo Rais alipasa kuonyesha ni kwa kiwango gani wajasiriamali wamekopesheka, SIO WANUNUA BALOON!
 
Aliandikiwa akasoma, nothing more. And i guess it doesn't mean anything to him. Kikwete hana political will ya kuona watanzania wanaondokana na umaskini, he is busy kufanya madili yake.

Duh! hii red imenishtuaaa?
 
Naombeni kuuliza Political Economy imefanana per se na Economics? Nauliza hivi kwasababu nilishawahi kuopt course ya political economy na haikuwa ngumu kiviiile....PE ndio Economics yenyewe?

PE-resource distribution while Pure Economics=resource allocation; need more?
 
Mkuu with all due respect for your views, hakuna tena nasisitiza HAKUNA uhusiano wowote kati ya nchi kuendeshwa kidemokrasia (siasa safi) na maendeleo ya kiuchumi. Hakuna tafiti yoyote iliyothibitisha kuwa democratic countries zinapata maendeleo ya kiuchumi zaidi ya zile nchi ambazo zinakandamiza demokrasia.

Mifano michache ya nchi zilizoendelea na demokrasia yake inatia shaka ni China, Singapole, Indonesia. Hata ukiangalia jirani zetu Ruanda wao wana record higher economic growth every year more than Tanzania wakati kidemokrasia tuko juu zaidi yao!!
Wel said mkuu, na hata kama tafiti hiyo itapatikana, for sure ita-lack kile kinachoitwa "impirical evidence" ya ku-support hilo-thenksi
 
alishasemaga foleni za magari ni maisha bora, hivyo ni kama amerudia kilekile, yeye kwake anafikiri watanzania kuwa na mabaloon ndo kuendelea, mrudisheni class
 
Alikuwa sahihi. Nchi yoyote kuendelea inahitaji kujenga "middle class" ambayo "definition" yake inatofautiana nchi moja hadi nyingine. Lakini kwa Tanzania ni ukweli kuwa daraja la kati (middle class) ni hao wanaoendesha ma-"baloon". Inawezekana ni ya mikopo, lakini ukweli ni kuwa hawa wana kipato kiasi kwamba mabenki yamewaona wanakopesheka.

Hawa watu wa aina hii "proportion" yao inapokuwa kubwa katika nchi, ni ukweli kuwa hiyo inakuwa ishara ya mafanikio kwa nchi. Tanzania tukifikia level ambapo asilimia 80% ni hawa waendesha mabaloon, basi tumetoka. Serikali inatakiwa ijenge mkakati madhubuti wa kuhakikisha hili tabaka linakuwa kwani hawa ndo consumers. Uchumi ukiwa na consumers, viwanda vitajengwa kwani soko ni kubwa.

Hapa rais kasema ukweli. Tunaweza kutofautiana maoni ya jinsi gani ya kufikia kiwango cha kuwa na majority ya watu wetu katika daraja hili la kati, lakini ukweli ni kuwa tunahitaji kuwa na "strong middle class" kwa wingi.

Naungana na wewe kaka kuhusu umuhimu wa "middle class" na ni kweli kabisa hawa ndio consumers wa bidhaa za viwandani kwa kiasi kikubwa na wana umuhimu sana kuinua uchumi wa nchi.
Lakini hilo ni moja ili uchumi ukiwe lazima kuwe na unyanjuaji wa sectors na matabaka yote kwa wakati maana ukiwapa sana nafasi waendesha "mabaloon" bila shaka "third class" ndio wataumia zaidi, hivyo jambo la msingi ni kuelewa uchumi wa nchi ni matokeo ya mchanganyiko wa mabo membi yaliyotiliwa jitihada kwa kwa kuzingatia umuhimu ulio sawa!
 
Ni kweli alisema hivyo,akisistiza umuhimu wa kuwa na middle class kubwa,akasema duniani pote middle class ndo nguzo ya kunyanyuka kwa uchumi,majority wanapokuwa lower class ni ngumu sana,tunabaki chini............Its not surprising at all when it come sfrom him,he was very confident whe talking!!!:smile-big:

nilimsikiliza, and it is tru he was confident. lakini nilikuwa namtazama alivyokuwa anaongea na kushuhulika na yale makaratasi. it was obvious hiyo hotuba aliandikiwa na mtaalamu ambaye hajui nini kinatokea tz sasa hivi na JK hakuweza ku edit. what i am saying ni kwamba rais anatakiwa kila mara atoe hotuba inayojikita katika hali ya kisiasa na kiuchumi ya nchi na wala siyo kutusomea high school economic theories.
 
nilimsikiliza, and it is tru he was confident. lakini nilikuwa namtazama alivyokuwa anaongea na kushuhulika na yale makaratasi. it was obvious hiyo hotuba aliandikiwa na mtaalamu ambaye hajui nini kinatokea tz sasa hivi na JK hakuweza ku edit. what i am saying ni kwamba rais anatakiwa kila mara atoe hotuba inayojikita katika hali ya kisiasa na kiuchumi ya nchi na wala siyo kutusomea high school economic theories.

Aliandikiwa na nani Dkt Bana? aaa sory! I mean Dkt ....mvuaaaaaaaaaaa
 
JK hakukosea kudokeza kuwa watu wa daraja la pili ni kielelezo cha maendeleo ya nchi. Ni ukweli usiopingika kwamba tabaka la pili (middle class) linapokuwa kubwa kuliko la juu na la chini basi hapo ujue mambo yanaiendea nchi vyema kiuchumi. Lakini hicho ni kielelezo tu; si mkakati wa maendeleo. Rais Museveni alishawahi kutoa mada kuhusu dhana hii miaka ya nyuma. Labda tatizo linakuja alivyoliainisha tabaka hilo hapa nchini kama la wenye mabaloon na elimu ya sekondari. Kwamba mabaloon (kama ndio kipimo chenyewe) ni ya mikopo au la si suala. Ila ni wangapi wanaweza kuyamudu; iwe kwa mikopo au fedha taslimu? Kama inafikia angalau asilimia 40 basi hatuna kero siye; tukiudhika tunaweza hata kuwarushia mayai na nyanya viongozi wanaotukera badala ya mawe.

Tatizo si kauli hiyo, bali angeendelea zaidi kuainisha mikakati ya serikali ya chama chake kuhakikisha tabaka la kati linaongezeka kwa kasi katika miaka michache ijayo. Vinginevyo, inakuwa kama kuwasimulia wajukuu ndoto za alnacha - na hapo ndipo lilipo tatizo kubwa la wakulu wetu Afrika. Wanajua sana kuielezea pepo bila kudhamiria kwa dhati mikakati ya kutufikisha huko.
 
JK hakukosea kudokeza kuwa watu wa daraja la pili ni kielelezo cha maendeleo ya nchi. Ni ukweli usiopingika kwamba tabaka la pili (middle class) linapokuwa kubwa kuliko la juu na la chini basi hapo ujue mambo yanaiendea nchi vyema kiuchumi. Lakini hicho ni kielelezo tu; si mkakati wa maendeleo. Rais Museveni alishawahi kutoa mada kuhusu dhana hii miaka ya nyuma. Labda tatizo linakuja alivyoliainisha tabaka hilo hapa nchini kama la wenye mabaloon na elimu ya sekondari. Kwamba mabaloon (kama ndio kipimo chenyewe) ni ya mikopo au la si suala. Ila ni wangapi wanaweza kuyamudu; iwe kwa mikopo au fedha taslimu? Kama inafikia angalau asilimia 40 basi hatuna kero siye; tukiudhika tunaweza hata kuwarushia mayai na nyanya viongozi wanaotukera badala ya mawe.

Tatizo si kauli hiyo, bali angeendelea zaidi kuainisha mikakati ya serikali ya chama chake kuhakikisha tabaka la kati linaongezeka kwa kasi katika miaka michache ijayo. Vinginevyo, inakuwa kama kuwasimulia wajukuu ndoto za alnacha - na hapo ndipo lilipo tatizo kubwa la wakulu wetu Afrika. Wanajua sana kuielezea pepo bila kudhamiria kwa dhati mikakati ya kutufikisha huko.

Kweli mzee. Tatizo ni kusema kuwa middle class ni watu wenye ma-baloon!! i thought middle class ni watu walio na degree wanaopiga kazi katika sector mbali mbali...kwa mfano financial advisors, walimu, madaktari, ma-professor, nk. Tatizo ameshindwa kuelewa middle class ni nini (alafu ni mchumi)!! Yeye mwenyewe alitakiwa kuwa middle class, sema katuibia na sasa anatutesa!
 
Back
Top Bottom