Dar: Watu Wawili kizimbani wakidaiwa kubaka

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,377
8,121
Vijana wawili, Erick Filbert (27) na Jafari Said (23) wakazi wa Wilaya ya Temeke wamefikishwa mbele ya Mahakama ya Wilaya ya Temeke kwa mashtaka ya ubakaji.

Wawili hao wamesomewa mashtaka yao wanayodaiwa kuyatenda kwa nyakati tofauti na Wakili wa Serikali, Amedeus Mallya mbele ya Hakimu Mkuu Mkazi, Ajali Milanzi.

Mshtakiwa Erick Filbert anakabiliwa na makosa mawili, kumbaka mwanafunzi mwenye umri wa miaka 17 anayesoma Shule ya Sekondari Taifa, kinyume na kifungu cha 130, (1) (2e) na 131 (1) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu namba 16 marejeo ya mwaka 2022.

Shtaka la pili ni kumpa ujauzito mwanafunzi huyo kinyume na kifungu 60A (3) cha Sheria ya Elimu namba 353 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2016.

Akisoma shtaka dhidi ya Jafari Said, wakili Mallya amesema, "Mtuhumiwa alifanya mapenzi bila ridhaa na binti wa miaka 18 mnamo Agosti 12, 2023 eneo la Saku Ilulu wilayani Temeke kinyume na Sheria ya Kanuni ya Adhabu namba 16 kifungu cha 130 (1) (2a) na 131 (1) marejeo ya mwaka 2022."

Washtakiwa wote wamekana makosa yao na kuachiwa kwa dhamana, mashauri yao yatasikilizwa tena Septemba 20, 2023.

MWANANCHI
 
Huu ujinga upo Tanzania tu??
Binti wa miaka 18 ni makubaliano soup ubakaji
 
Nadharia 1: Inawezekana huyu binti alikua kwenye mahusiano na hao vijana wote wawili, baada ya kupachikwa mimba na mmoja kati yao na wazazi wake kutambua wakaamua kumbananisha binti aseme alikua akijihusisha kwenye mahusiano ya kimapenzi na nani, binti kwa kushindwa kuelewa ni yupi haswa kati ya hao wawili aliyempachika mimba akaamua kuwataja wote, wazazi kwa hasira ya kuona binti yao amepatiwa ujauzito katika kipindi ambacho hawakutarajia wakaamua kushirikiana na polisi kutengeneza hoja kua hao wahusika walimbaka binti yao na kumpatia ujauzito, hii inaitwa kukomoana, ukikutana na msala kama huu kwa wazazi wenye PESA uwezekano wa kwenda jela ni 80%. Hizi kesi zipo sana uswahilini. Kama unajua hukumbaka ila mlikua kwenye mahusiano jitahidi kadiri iwezekanavyo muyamalize Kifamilia bila kupelekana mahakamani, mara nyingi wazazi wa upande wa binti huwa wanataka mlungula na uhakika wa kumuoa binti yao ama kuji commit kutunza mtoto.

Nadharia 2: Inawezekana ni kweli hao jamaa walimbaka huyo binti.

Kila upatapo nafasi ya kuvunja sheria kumbuka Law is for the poor but Justice is only for the rich and powerful.
Sheria ifuate mkondo wake
 
Nadharia 1: Inawezekana huyu binti alikua kwenye mahusiano na hao vijana wote wawili, baada ya kupachikwa mimba na mmoja kati yao na wazazi wake kutambua wakaamua kumbananisha binti aseme alikua akijihusisha kwenye mahusiano ya kimapenzi na nani, binti kwa kushindwa kuelewa ni yupi haswa kati ya hao wawili aliyempachika mimba akaamua kuwataja wote, wazazi kwa hasira ya kuona binti yao amepatiwa ujauzito katika kipindi ambacho hawakutarajia wakaamua kushirikiana na polisi kutengeneza hoja kua hao wahusika walimbaka binti yao na kumpatia ujauzito, hii inaitwa kukomoana, ukikutana na msala kama huu kwa wazazi wenye PESA uwezekano wa kwenda jela ni 80%. Hizi kesi zipo sana uswahilini. Kama unajua hukumbaka ila mlikua kwenye mahusiano jitahidi kadiri iwezekanavyo muyamalize Kifamilia bila kupelekana mahakamani, mara nyingi wazazi wa upande wa binti huwa wanataka mlungula na uhakika wa kumuoa binti yao ama kuji commit kutunza mtoto.

Nadharia 2: Inawezekana ni kweli hao jamaa walimbaka huyo binti.

Kila upatapo nafasi ya kuvunja sheria kumbuka Law is for the poor but Justice is only for the rich and powerful.
Sheria ifuate mkondo wake
Boss umejuaje kuwa binti anayehusishwa na vijana wote wawili ni mmoja?
 
Sheria inasema iwe amekubali au ajakubali kufanya mapenzi na mwanafunzi tena chini ya Miaka 18 automatical umebaka
 
Nadharia 1: Inawezekana huyu binti alikua kwenye mahusiano na hao vijana wote wawili, baada ya kupachikwa mimba na mmoja kati yao na wazazi wake kutambua wakaamua kumbananisha binti aseme alikua akijihusisha kwenye mahusiano ya kimapenzi na nani, binti kwa kushindwa kuelewa ni yupi haswa kati ya hao wawili aliyempachika mimba akaamua kuwataja wote, wazazi kwa hasira ya kuona binti yao amepatiwa ujauzito katika kipindi ambacho hawakutarajia wakaamua kushirikiana na polisi kutengeneza hoja kua hao wahusika walimbaka binti yao na kumpatia ujauzito, hii inaitwa kukomoana, ukikutana na msala kama huu kwa wazazi wenye PESA uwezekano wa kwenda jela ni 80%. Hizi kesi zipo sana uswahilini. Kama unajua hukumbaka ila mlikua kwenye mahusiano jitahidi kadiri iwezekanavyo muyamalize Kifamilia bila kupelekana mahakamani, mara nyingi wazazi wa upande wa binti huwa wanataka mlungula na uhakika wa kumuoa binti yao ama kuji commit kutunza mtoto.

Nadharia 2: Inawezekana ni kweli hao jamaa walimbaka huyo binti.

Kila upatapo nafasi ya kuvunja sheria kumbuka Law is for the poor but Justice is only for the rich and powerful.
Sheria ifuate mkondo wake
Umesoma kweli kilichoandikwa?
 
Nadharia 1: Inawezekana huyu binti alikua kwenye mahusiano na hao vijana wote wawili, baada ya kupachikwa mimba na mmoja kati yao na wazazi wake kutambua wakaamua kumbananisha binti aseme alikua akijihusisha kwenye mahusiano ya kimapenzi na nani, binti kwa kushindwa kuelewa ni yupi haswa kati ya hao wawili aliyempachika mimba akaamua kuwataja wote, wazazi kwa hasira ya kuona binti yao amepatiwa ujauzito katika kipindi ambacho hawakutarajia wakaamua kushirikiana na polisi kutengeneza hoja kua hao wahusika walimbaka binti yao na kumpatia ujauzito, hii inaitwa kukomoana, ukikutana na msala kama huu kwa wazazi wenye PESA uwezekano wa kwenda jela ni 80%. Hizi kesi zipo sana uswahilini. Kama unajua hukumbaka ila mlikua kwenye mahusiano jitahidi kadiri iwezekanavyo muyamalize Kifamilia bila kupelekana mahakamani, mara nyingi wazazi wa upande wa binti huwa wanataka mlungula na uhakika wa kumuoa binti yao ama kuji commit kutunza mtoto.

Nadharia 2: Inawezekana ni kweli hao jamaa walimbaka huyo binti.

Kila upatapo nafasi ya kuvunja sheria kumbuka Law is for the poor but Justice is only for the rich and powerful.
Sheria ifuate mkondo wake
Soma vizuri vijana ni wawili na mabinti ni wawili. Kila mtu na demu wake... Mmoja 17 na mwanafunzi na kajazwa mimba, mwengine 18 lkn alibakwa na kijana mwengine

Sent from my TECNO CI6 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom