Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wewe unaongea haya kwa kuwa hujawahi hata kupigwa ngeta na majambazi. Ila ugewahi kuona waathirika wa matukio ya ujambazi, wala usingekuwa na huruma. Juzi tulikuwa na mzee mmoja ukimwangalia kichwani kumebondeka na sehemu nyingine za mwili zimejaa makovu. Alivamiwa na majambazi na kunyang'anywa pesa. Wakati tukiwa wadogo tunakaa mkoani Mza, tulivamiwa na majambazi. Mzee wangu alichezea kichapo sijawahi ona. Majambazi sio watu. Ni bora ukutane na simba kuliko kukutana na jambazi.Risasi za miguu na wakafariki wakiwa njiani kuelekea hospital... Huu msemo hauna mbadala? Kila mara ni hivo hivi.
Sent using Jamii Forums mobile app
Dah lllKwa polisi wa Tanzania walivyo "shupavu", hata wakikuangalia muda mrefu unakufa sembuse risasi za miguu!?
kikosi kazi maalum huwa hakina mipaka mkuuSinema hizo.
Halafu kwanini askari wa Dar wakaue Kibaha, mkoa mwingine kabisa?
Haya ni maandishi ambayo huwa yanasomwa kwa sauti kila wakatiRisasi za miguu na wakafariki wakiwa njiani kuelekea hospital... Huu msemo hauna mbadala? Kila mara ni hivo hivi.
Sent using Jamii Forums mobile app
Niambie range gani hufundishwa majeshi yetu kuanzia kiunoni kushuka chini ukijibu hilo swali nitajua unaelewa kitu. Na pia kwa mujibu was sheria zako hakuna jeshi lolote lina ruhusiwa kuua.na ukijifanya unajua sana sheria lazima utakuwa mpumbavu mana sheria hufunga vitu vyenye msingi na tija ili tuwe wajinga tusiweze songa mbeleMkuu usibishane nami!!
Policeman always shot not to kill, na tageti yao ni kuanzia kiunoni kushuka chini. Ila akua lazima atoe utetezi(mfano RPC's hujitetea kwamba huwapiga majambazi risasi za miguuni ila wanakufaga njiani wakiwa wana wahishwa hospital)
Soma sheria mkuu usikariri
5/5
Risasi za miguu na wakafariki wakiwa njiani kuelekea hospital... Huu msemo hauna mbadala? Kila mara ni hivo hivi.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hadithi ni hiyo hiyo kila siku, kuonyesha zilipo silaha na au majambazi kukimbia na kupigwa risasi.Risasi za miguu na wakafariki wakiwa njiani kuelekea hospital... Huu msemo hauna mbadala? Kila mara ni hivo hivi.
Sent using Jamii Forums mobile app
Najikuta nacheka bila sababuNext time polisi wawe wanawalenga WATUHUMIWA risasi za tumbo tu! Maana za miguuni huwa daima zinapelekea vifo vyao na kuwanyima nafasi ya kujitetea ambayo ni ya msingi kwa wote! Au angalau wawe wanalenga vichwa!!
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewaua majambazi watano na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa wanne, kukamata silaha nne na risasi 59 katika matukio matatu tofauti.
Marchi 3 mwaka huu majira ya saa kumi na mbili na nusu jioni huko maeneo ya Kibaha Maili moja Jeshi la Polisi likiwa katika ufuatiliaji lilimkamata mtuhumiwa moja aitwaye Friday Samson (29)askari wa JWTZ Kikosi cha 36KJ Kibaha Msangani na katika mahojiano ya kina alikiri kumiliki silaha mbili kinyume cha sheria na kwamba huzihifadhi silaha hizo nyumbani kwa mke mdogo mtaa wa Muheza Kibaha Pwani na hufanyia matukio ya uhalifu katika maeneo mbalimbali.
Baada ya mahojiano Jeshi la Polisi pamoja na mtuhumiwa huyo walifika kwenye nyumba hiyo na kufanikiwa kukamata silaha aina ya AK 47 yenye namba NM174844 ikiwa na risasi 20 ndani ya magazine, boksi moja likiwa na risasi 27,bastola moja yenye namba 3249 ikwa na risasi 7 ndani ya magazine na risasi 3 za silaha ya G3.
Mtuhumiwa alikubali kuwaonyesha wenzake watatu anaoshirikiana nao katika matukio hayo na askari walipofika kwenye nyumba wanayoishi watuhumiwa hao walianza kukimbia kupitia mlango wa nyuma na hatimaye askari walirusha risasi hewani kuwaamuru wasimame lakini walikaidi na ndipo walipowafyatulia risasi za miguu ambazo ziliwajeruhi na walifariki dunia wakiwa njiani kupelekwa hospitali.