Dar lands official arrested

Dar lands official arrested

Hii safi sana. Next, ahamie makao makuu-maana huko ndio kumeoza kabisaa yaani hata hakunuki tena!!
 
By the way ni nani mwenye mamlaka ya kufukuza kazi hao maafisa Ardhi? Nijuacho mimi Afisa Ardhi hana uwezo wa mwisho kwenye maamuzi ya kugawa ardhi. Ni process na hata madiwani huhusishwa. Je Lukuvi aliliona hilo? Au ndio anajipigia debe aendelee kuwa Rc wa Dar tambarare? Je wafanyakazi wa serikali wafuate matakwa ya nani. sheri au wakuu wa Mikoa?

Nina wasiwasi mkubwa na hii njia wanyotumia hawa viongozi. Disliplinary procedures sii hizi wala hazifanani na hizi zao - Tanga, na hii Lukuvism.
 
By the way ni nani mwenye mamlaka ya kufukuza kazi hao maafisa Ardhi? Nijuacho mimi Afisa Ardhi hana uwezo wa mwisho kwenye maamuzi ya kugawa ardhi. Ni process na hata madiwani huhusishwa. Je Lukuvi aliliona hilo? Au ndio anajipigia debe aendelee kuwa Rc wa Dar tambarare? Je wafanyakazi wa serikali wafuate matakwa ya nani. sheri au wakuu wa Mikoa?

Nina wasiwasi mkubwa na hii njia wanyotumia hawa viongozi. Disliplinary procedures sii hizi wala hazifanani na hizi zao - Tanga, na hii Lukuvism.

Lukuvi hajawafukuza kazi, amewakamata na kuwakabithi TAKUKURU kwa sababu ya tuhuma za rushwa. Kitu ambacho hata wewe ukiwa na msaada wa Polisi unaweza kufanya. Cheo la Lukuvi hapa kimetumika kwenye kufunga hizi ofisi tu na kuunda tume ya uchunguzi.

Hili la kuunda Tume sijui lina umuhimu gani wakati ameshawakabithi watuhumiwa TAKUKURU.
 
as usual zima moto. ngoja tuendelee kuona jinsi hakutokuwako na mwisho unaoeleweka... tutakuja kuona tu ni uzugagi ule ule.

kind of very tired.
 
Hii safi sana. Next, ahamie makao makuu-maana huko ndio kumeoza kabisaa yaani hata hakunuki tena!!

Huko Makao makuu kuna Chiligati, Katibu Mwenezi wa Chama. Hakuingiliki kirahisi. Ni jambo la kusikitisha kwamba leo hii bado tunategemea operesheni za watu binafsi kuturudishia imani kwamba serikali ipo - watu ambao hata uwezo wao kamili na malengo yao hatuna uhakika nayo (Lukuvi, magufuli, Kalembo, n.k.). Tena wakati mwingine inabidi wafumbie macho sheria kusafisha uozo. Yaani tumeshindwa kabisa kuwa na mifumo imara inayodhibiti uozo kwa mtindo endelevu. Ndio maana wengine tunabakia kuwa wabezaji tu (cynics) hata kwa yale yanayoonekana kuwa na dalili njema kama hili. Tunachokiona ni ama Lukuvi kweli amepigwa na radi ya mageuzi na kuamua kwenda kinyume na mfumo wa uongozi uliopo (hivyo asubiri tu kutemwa) au ni mkakati mahsusi wa kuwapiga watanzania changa jingine la macho kuelekea uchaguzi.
 
Lakini Ardhi Kinondoni wamezidi. Kule Mikumi (Snow cap karibu na lango la jiji katika barabara ya Mikumi magomeni) kuna Kijana tajiri amegeuza garage ya kupaki magari yake watu wanalalamika anasema Pesa zake ndiyo zinafanya kazi. Cha ajabu zaidi kachukua life time parking ya gari zake kwenye barabar hiyo ilitowekwa lami hivi karibuni na kusababisha barbara iwe finyu na ajali za kukwanguana magari kibao. waut wa kawaida wanashangaa sana na uongozi wa manispaa ya kinondoni wanavyokaa kimya.
maafisa wote wanajua na wanalindana kwa vile kila mtu ana mradi wakwe wa kunginga pesa.
ultimately anaeuumia ni mwananchi wa hali ya chini ambaye mtoto wake hana pa kuchezea wala hawezi tena kuiona beach kwenye bahari ya Hindi.
Swali la kujiuliza ni kwamba hivi wale walioweka sehemu za open kwa ajili ya kuchezea na shughuli za kijamii walikuwa hawana akili na kwa nini zito zipotee hivi sasa?
Jamani tujitahidi haya mabo yafike mwisho hivyo tutakuwa tulalamikika tu mpaka lini wakati wengine wanatuona wendawazimu wakiuza haki za wenzao.
 
Pamoja na kwamba hatua aliyochukua Lukuvi inaweza kuwa ndiyo dawa sahihi ya uozo uliopo kwenye Serikali ya CCM na watendaji kwa ujumla. Lakini, kwanza timing yake inatia mashaka kwamba ndio yaleyale ya kutaka kuwa-impress wapigakura waone kwamba Serikali ya CCM inafanya kazi.

Hata hivyo, ingekuwa ni faraja zaidi kama Lukuvi angelitutajia majina ya watu ambao wamewahi kupewa viwanja kwa njia za aina hiyo kwa sababu mpokea rusha na mtoa rushwa wote wanahesabiwa ni wakosaji. Hao watu wenye kwenda kuhonga maofisa ardhi ili wapate viwanja ni wahalifu wakubwa sawa na akina Magesa wanaopokea hiyo rushwa na kutoa viwanja isivyo halali.Pia tusisahau kwamba kuna 'vigogo' ambao wanatumia nafasi zao na majina yao makubwa kupata viwanja. Matumizi hayo mabaya ya nafasi zao nayo ni kosa linalohitaji kushughulikiwa kama watajavyoshughulikiwa wengine wanaoshawishi maafisa ardhi kutenda kosa la upendeleo katika ugawaji viwanja. Tunataka kusikia majina ya mameya akina Londa, Kimbisa n.k. yakitajwa kwa sababu Mameya na viongozi wa Halmashauri huwataka maafisa ardhi watoe viwanja kwa vigogo na matajiri kadha wa kadha nchini kwa manufaa yao hao viongozi husika. Mfano hai niliowahi kuusikia ni juu ya kiwanja kimoja cha wazi pale Msasani ambacho kiligawiwa kwa Meya, Afisa mmoja Mwandamizi Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje na kwa Waziri wa Ulinzi kwa majina na si kwa ajili ya matumizi ya ofisi zao. Sasa viongozi kama hao wakianza kuvamia maeneo ya wazi yaliyotengwa kwa matumizi ya umma, maafisa ardhi watashindwaje kuiga?
 
atafungwa miezi sita, te te te! uo si ndio mwendo wa sasa, wanasiasa washajua watu wanachekela mtu anapoburuzwa mahakamani ila baada ya apo kama kawa! kwa sasa hawa mafisadi hata kupelekwa mahakamni kwao si tatizo wanjua sentence itakua upande wao au itachelewa sana! mzee liyumba si anapeta mwaka mmoja then anarudi kitaaa a clean person! si unajua jela siku ni 12 hrs kwa iyo, 2yrs ni mwaka mmoja! yaani anatoka hata shavu halijaisha kwanza jela yake anayokaa si kule kwa kunyea debe!
 
Back
Top Bottom