Mm mwenyewe sijuagi kabisa kutumia wifi mkuu.naomba nielekeze
UTANGULIZI.
Siyo kila sehemu kuna Wi-Fi,sehemu nyingine hazina Wi-Fi.Utajua kama hii sehemu ina Wi-Fi kwa kuona kialama cha Wi-Fi kwenye screen yako,kujua hii sehemu kama ina Wi-Fi au haina lazima uturn Wi-Fi on,ikishakuwa ON hapo ndiyo utajua kama hapa kuna Wi- Fi au hakuna.Sehemu isiyo na Wi-Fi hautaona kialama cha Wi-Fi,na sehemu yenye Wi- Fi utakiona kialama cha Wi-Fi.Sehemu zenye Wi-Fi nyingi ni mijini,yaani stendi za daladala,kwenye maofisi,mahoteli,migahawa n.k,ili mradi iwe mjini.
Baada ya kufika mjini ukiwasha Wi-Fi yako usikae kitako sehemu moja,unaweza kata tamaa kwamba nimeenda mjini nikawasha Wi-Fi halafu sijapata Wi-Fi,kumbe kosa ni la kwako la kukaa kitako sehemu moja,jaribu kutembea barabarani mjini pembezoni mwa maofisi,stendi,mashule,mahoteli.Sasa ukishakuwa unatembea mjini barabarani,hakikisha unaangalia kwenye screen yako iliyo na Wi-Fi on,hapo utaona vialama vya Wi-Fi,kuna Wi-Fi nyingine private,hizi kuzitumia huwezi kwa sababu lazima uwe na password ya hiyo Wi-Fi,utazijuaje private Wi-Fi?,zenyewe zinakuwa zina vikufuli.Wi-Fi nyingine ni public Wi-Fi,hizi ndiyo unaweza kuzitumia,utazijuaje?,zenyewe zinakuwa hazina alama ya vikufuli,maana yake hazina haja ya password.
JINSI YA KU-TURN ON Wi-Fi
Nenda settings,halafu nenda Wi-Fi,ukishakuwa kwenye Wi-Fi chagua options,halafu enable on.
UNAANZAJE KUTUMIA Wi-Fi?
Ukiishaichagua public Wi-Fi unayotaka,kwa simu za touch,long press hiyo Wi-Fi,itakuja options,halafu chagua connect Wi-Fi.Kwa simu za button,chagua options,halafu connect Wi-Fi.
N.B: Wi-Fi nyingine vifurushi vinakuwa vimeisha(nimetumia lugha hiyo ili nieleweke),kwa hiyo kifurushi kikiisha hautoperuzi internet hapo,itaload mpaka itakata yenyewe,ukiona hivyo kwenye hiyo Wi-Fi achana nayo tembea kwenye Wi-Fi nyingine.
Enjoy Wi-Fi