Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,814
- 11,991
Alikamatwa Mei 2020 na kukaa mahabusu ya polisi Central kwa siku 14 kwa amri ya utawala wa awamu ya tano kwa tuhuma za kuposti taarifa za wagonjwa wa Covid19 kukimbia Amana Hospital.
Pamoja naye Mhariri na Mkurugenzi wa Raia Mwema Mbaraka Islam naye alikamatwa na wote walipekuliwa nyumbani kwao.
Hadi sasa simu za Maria Victor, Islam na wenzake bado ziko polisi kwa miaka miwili sasani.
=====
MWANDISHI wa Habari wa gazeti la Raia Mwema, Marry Victor Mahundi (Maria Victor Mahundi) amefikishwa mahakamani kwa tuhuma zilizoanzia kwenye group la WhatsApp la gazeti hilo.
Marry pamoja na Mhariri na Mkurugenzi wa gazeti hilo Mbaraka Islam, walikamatwa Mei 2020, baada ya polisi kupelekewa taarifa za kuwapo post katika WhatsApp group yenye sauti ya wagonjwa wa Covid19 kutoroka hospital ya Amana, wilayani Ilala, Dar es Salaam.
Marry Victor ambaye amekua akijihusisha zaidi na kuandika habari za afya alikaa mahabusi ya polisi Central kwa wiki mbili kabla ya kuachiwa kwa dhamana.
Pamoja na Mary walikamatwa pia wenzake wawili, Aisha Peter Mahita na Rogers Wilfred Simeo, wakitajwa kumsaidia kusajili laini ambayo aliitumia kuposti taarifa hizo katika group la WhatsApp.
Mhariri wake Mbaraka Islam alilamatwa kwa kuwa alikua Admin wa group hilo, lakini haifahamiki kuhusu wenzake ambao walikua Admin wa group hilo.
Watuhumiwa wote waliokamatwa waliacha simu zao polisi tokea Mei 2020 hadi kesi hiyo iliposomwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala ya Kinyerezi Septemba 8, 2022.
Katika kesi hiyo iliyosomwa mbele ya Hakimu Mfawidhi wa wilaya ya Ilala Glory Nkwera ikiwa na watuhumiwa watatu, Maria, Aisha na Rogers ambao walishitakiwa kwa kosa la kutumia laini ya simu bila kufuata taratibu za kubadilisha umiliki toka kwa Asha kwenda kwa Maria.
Rogers alikua wakala wa usajili.
Marry ameshtakiwa kwa tuhuma za kushindwa kusajili laini ya simu iliyokua imesajiliwa kwa Kitambulisho cha Asha na Rogers kwa kumsaidia Maria kutenda kosa hilo na kutotoa taarifa kwenye mamlaka kuhusu kutotumia laini waliyosajili.
Rogers ni wakala wa Tigo aliyesajili line yenye jina la Asha lakini ikawa inatumiwa na Maria.
Pamoja naye Mhariri na Mkurugenzi wa Raia Mwema Mbaraka Islam naye alikamatwa na wote walipekuliwa nyumbani kwao.
Hadi sasa simu za Maria Victor, Islam na wenzake bado ziko polisi kwa miaka miwili sasani.
=====
MWANDISHI wa Habari wa gazeti la Raia Mwema, Marry Victor Mahundi (Maria Victor Mahundi) amefikishwa mahakamani kwa tuhuma zilizoanzia kwenye group la WhatsApp la gazeti hilo.
Marry pamoja na Mhariri na Mkurugenzi wa gazeti hilo Mbaraka Islam, walikamatwa Mei 2020, baada ya polisi kupelekewa taarifa za kuwapo post katika WhatsApp group yenye sauti ya wagonjwa wa Covid19 kutoroka hospital ya Amana, wilayani Ilala, Dar es Salaam.
Marry Victor ambaye amekua akijihusisha zaidi na kuandika habari za afya alikaa mahabusi ya polisi Central kwa wiki mbili kabla ya kuachiwa kwa dhamana.
Pamoja na Mary walikamatwa pia wenzake wawili, Aisha Peter Mahita na Rogers Wilfred Simeo, wakitajwa kumsaidia kusajili laini ambayo aliitumia kuposti taarifa hizo katika group la WhatsApp.
Mhariri wake Mbaraka Islam alilamatwa kwa kuwa alikua Admin wa group hilo, lakini haifahamiki kuhusu wenzake ambao walikua Admin wa group hilo.
Watuhumiwa wote waliokamatwa waliacha simu zao polisi tokea Mei 2020 hadi kesi hiyo iliposomwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala ya Kinyerezi Septemba 8, 2022.
Katika kesi hiyo iliyosomwa mbele ya Hakimu Mfawidhi wa wilaya ya Ilala Glory Nkwera ikiwa na watuhumiwa watatu, Maria, Aisha na Rogers ambao walishitakiwa kwa kosa la kutumia laini ya simu bila kufuata taratibu za kubadilisha umiliki toka kwa Asha kwenda kwa Maria.
Rogers alikua wakala wa usajili.
Marry ameshtakiwa kwa tuhuma za kushindwa kusajili laini ya simu iliyokua imesajiliwa kwa Kitambulisho cha Asha na Rogers kwa kumsaidia Maria kutenda kosa hilo na kutotoa taarifa kwenye mamlaka kuhusu kutotumia laini waliyosajili.
Rogers ni wakala wa Tigo aliyesajili line yenye jina la Asha lakini ikawa inatumiwa na Maria.