ikhlas
JF-Expert Member
- Jun 25, 2015
- 1,097
- 1,432
Mida hi ya ucku naskia milio mfano wa jengo linalo ungua moto au kama risas au mfano wa mabomu....Walio karibu watujuze 12:05pm.....kina happen in milio tuuuuu
========
Hamna mabomu wala risasi ni fataki zinapigwa na wahindi yapo kwenye sherehe zao sema hayo mafataki yana vishindo vikubwa na mwanga wa kutosha
Kwa upande mwingine nadhan itakuwa kero kwa watu wa maeneo ya karibu maana usingzi hauji kabsa kwa kelele hizi.
kuna sauti ya mizinga na mabomu mahali nilipo mimi(kinondoni) naisikia inatokea katikati ya jiji maeneo ya kariakoo, ilala au magomeni
kuna mtu yuko Town kanipigia simu kuniambia hivyo. kwenye simu wakati tutaongea nilikua nasikia milipuko. mwenye kujua kuna nini atupe taarifa zaidi
========
Leo ni sherehe za kihindi inaitwa diwali ni fataki hizo zinazolia mi niko kariakoo nashindwa hata kulala wanapiga mafataki mazito utafikiri mizinga
Ni Fataki zinapigwa hapo maeneo ya Kisutu. Ndugu zetu wana shughuli yao pale tangu Jioni. Hata hivyo waliomba Kibali Polisi.
Nashauri wakiwa Wanategemea kufanya hizo Shughuli zao zinazoambatana na Fataki, basi siku nyingine wawe wanatoa Tangazo Hapa JamiiForums au hata Radio TBC Taifa au TBC1 ili kututoa hofu na kutuweka tayari, vinginevyo watakuja kuua watu kwa Presha.
Hii ya leo ni kubwa kuliko