Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,010
- 9,875
Mahakama ya Wilaya ya Ilala imemuhukumu, Stambuli Yusufu (35) kifungo cha maisha jela baada ya kumkuta na hatia ya kumuingilia kinyume na maumbile mtoto wa kike wa miaka nane.
Mshtakiwa huyo anadaiwa kumfanyia kitendo hicho mtoto huyo anayesoma darasa la nne kati ya mwaka 2017 na 2018.
Imeelezwa kuwa baada ya kitendo hicho alikuwa akimpatia Sh1,000 hadi 2,000, kumtaka asiseme kwa mtu yeyote.
Akisoma hukumu hiyo leo Jumanne Januari 28, 2020 hakimu mkazi, Jimson Mwankenja amesema kifungo cha maisha jela kitaanza kuhesabiwa baada ya mshtakiwa kumlipa Sh2 milioni mtoto huyo.
Amesema ikiwa atashindwa kulipa fidia hiyo, atachapwa viboko 12 na kuanza kutumikia kifungo hicho.
Hakimu Mwankenja amesema ametoa hukumu hiyo baada ya kuzingatia ushahidi uliotolewa na mashahidi sita wa upande wa mashtaka, utetezi wa mshtakiwa na uzito wa kosa hilo.
Chanzo: Mwananchi
Mshtakiwa huyo anadaiwa kumfanyia kitendo hicho mtoto huyo anayesoma darasa la nne kati ya mwaka 2017 na 2018.
Imeelezwa kuwa baada ya kitendo hicho alikuwa akimpatia Sh1,000 hadi 2,000, kumtaka asiseme kwa mtu yeyote.
Akisoma hukumu hiyo leo Jumanne Januari 28, 2020 hakimu mkazi, Jimson Mwankenja amesema kifungo cha maisha jela kitaanza kuhesabiwa baada ya mshtakiwa kumlipa Sh2 milioni mtoto huyo.
Amesema ikiwa atashindwa kulipa fidia hiyo, atachapwa viboko 12 na kuanza kutumikia kifungo hicho.
Hakimu Mwankenja amesema ametoa hukumu hiyo baada ya kuzingatia ushahidi uliotolewa na mashahidi sita wa upande wa mashtaka, utetezi wa mshtakiwa na uzito wa kosa hilo.
Chanzo: Mwananchi