#COVID19 Dar: Askofu Ruwai’chi aagiza mapadri wote kupata chanjo dhidi ya UVIKO-19

Kama wangekuwa na akili wangeaminiwa na kuachwa waamue kwa hiari kwa kutumia hiyo akili yao!! Agizo hilo limewadhalilisha sana!! Moja ya miiko ya kitabibu ni kutolulazisha aina ya tiba/kinga kwa mgonjwa!
Kanisa katoliki Lina Intelligensia kubwa sana, mpaka wamefikia hatua yote hiyo watakuwa wamejiridhisha.. Catholic sio kanisa la Gwajima
 
Yule "bwana mropokaji" alishawahi KUMSHAMBULIA kwa maneno mabaya mwadhama Askofu msomi....

Sasa tunasubiri tena amshambulie msomi baba Askofu Ruwaichi......

Wenzake wanaitambua kuwa SAYANSI ni moja ya elimu MWENYEZI MUNGU ametupatia , yeye anatambua "CONSPIRACY THEORIES" kuwa ndiyo majibu makubwa zaidi ya SAYANSI.....

#ChanjoNiBoraKulikoTiba
#SiempreJMT
Nyie mnachanganya mambo, ya wakati ule issue ilikua ni KATIBA, tena huyo unae mtetea alikwenda kinyume na makubaliano na maaskofu wenzie waliokubaliana kwenye kikao chao cha TEC. Tusichanganye mambo, hili la chanjo na katiba ni vitu 2 tofauti sana
 
Waabudu sanamu ndiyo zao...Wanasahau uzima wa milele kwa miaka michache ya dunia hii mbaya na iliyojaa uasi
Hao wavaa kanzu hawana maana unafiki tu wakijifanya wema kumbe mbwa mwitu wakiabudu sanamu!
 
Jamaa anaongea ujinga sana, Angejua historia ya Mtakatifu Paulo asingeongea huu ujinga-Licha ya Paulo kuwa na historia ya kuua wafuasi wa KRISTU,lakini KRISTU alimchagua yeye ndo aeneze injili yake.YESU mwenyewe alisema mwema mkamilifu ni MUNGU pekee.
Hao ni wanafiki sana wanajiita watakatifu wakijitwalia uungu! Kristo ndo kichwa cha kanisa huyo papa ni vyeo tu!
 
Tulimwomba Mungu awajalie utashi wanasayansi ili chanjo ipatikane mapema. Tumepata mapema, tena tunaanza kuhoji.

Wana wa Mungu, tumshukuru Mungu kwa kuwa amesikia sala na maombi yetu, tukachanjwe..

Nilichanjwa wiki 3 zilizopita. Nilikiuka masharti kidogo, baada ya kuchanjwa sikusubiri dakika 30 kama wanavyoshauri. Kwa sababu nilikuwa safarini, nilchanjwa na kuingia kwenye gari, nikaendesha umbali wa kilometa 600 kwa masaa 8. Nimeendelea na kazi zangu kama kawaida. Bega kidogo lilinisumbua kwa maumivu siku ya pili na ya tatu. Na siku moja nilisikia homa kidogo, otherwise I am perfect 100%.
Bado unatakiwa uendelee kumshukuru Mungu maana sio wote wamepata matokeo kama yako baada ya kuchanjwa.
 
Yule "bwana mropokaji" alishawahi KUMSHAMBULIA kwa maneno mabaya mwadhama Askofu msomi....

Sasa tunasubiri tena amshambulie msomi baba Askofu Ruwaichi......

Wenzake wanaitambua kuwa SAYANSI ni moja ya elimu MWENYEZI MUNGU ametupatia , yeye anatambua "CONSPIRACY THEORIES" kuwa ndiyo majibu makubwa zaidi ya SAYANSI.....

#ChanjoNiBoraKulikoTiba
#SiempreJMT
.
IMG_20210825_103937.jpg
 
Askofu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Yuda Tadheus Ruwai’chi ameagiza mapadri wote kupata chanjo dhidi ya UVIKO-19 kwa kuwa ugonjwa huo unaumiza na kuondoa uhai
Askofu muongo mkubwa eti Tanzania tuliomba ipatikane Chanjo!!! Huyu Askofu mmmmmm.Kweli Ni sahihi kuitwa Yuda Ni Yuda Iscariote hasa

Sisi tuliomba Corona iondoke Tanzania hatujawaji omba tukaitaja chanjo midomoni mwetu tulipoomba kipindi Cha Magufuli

Yeye aliomba Nini? Si alisema tusikilize wanasayansi ? Hata hayo maombi ya kuomba changing alifanya wapi? Askofu muongo huyu looo.Eti watanzania tuliomba ipatikane Chanjo!!!! Askofu acha uongo
 
Askofu muongo mkubwa eti Tanzania tuliomba ipatikane Chanjo!!! Huyu Askofu mmmmmm.Kweli Ni sahihi kuitwa Yuda Ni Yuda Iscariote hasa

Sisi tuliomba Corona iondoke Tanzania hatujawaji omba tukaitaja chanjo midomoni mwetu tulipoomba kipindi Cha Magufuli

Yeye aliomba Nini? Si alisema tusikilize wanasayansi ? Hata hayo maombi ya kuomba changing alifanya wapi? Askofu muongo huyu looo.Eti watanzania tuliomba ipatikane Chanjo!!!! Askofu acha uongo
Una uhakika hakuna watanzania walioomba kwa Mungu hizo chanjo?!!!

Katika maombi yao yote ulikuwepo?!!
 
Una uhakika hakuna watanzania walioomba kwa Mungu hizo chanjo?!!!

Katika maombi yao yote ulikuwepo?!!
Askofu kasema tuliomba chanjo kaweka uwingi

Ina maana Sio Siri ndani ya Jimbo la Dar es salaam .Maana Akisema tuliomba Chanjo Ina maana hiyo hadhira ilihusika aliyohutubia

Nani ndani ya Katoliki aliomba na huyo Askofu kuombea chanjo? Muongo ataje hata padri au sista au bruda yeyote waliyeomba naye.Muongo
 
Askofu kasema tuliomba chanjo kaweka uwingi

Ina maana Sio Siri ndani ya Jimbo la Dar es salaam .Maana Akisema tuliomba Chanjo Ina maana hiyo hadhira ilihusika aliyohutubia

Nani ndani ya Katoliki aliomba na huyo Askofu kuombea chanjo? Muongo ataje hata padri au sista au bruda yeyote waliyeomba naye.Muongo
Uwingi unaanza na wawili....una uhakika hakuna maaskofu ,mapadri na maburuda walioomba hizo chanjo ?!!!

Akipita hapa atatuambia.....
 
View attachment 1906131
PICHA: Askofu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Yuda Tadheus Ruwai’chi

Askofu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Yuda Tadheus Ruwai’chi ameagiza mapadri wote wa jimbo hilo kupata chanjo dhidi ya Uviko 19 kwa kuwa ugonjwa huo unaumiza na kuondoa uhai.

Ametoa agizo hilo leo Jumanne Agosti 24, 2021 katika adhimisho la Misa Takatifu ya kumuombea Padri Paul Haule aliyekuwa Paroko Msaidizi katika Parokia ya Mtakatifu Petro na Mkurugenzi wa Tumaini Media.

Ruwai’chi amesema mwaka 2020 wakati wa awamu ya kwanza ya janga la Uviko-19 watu walimuomba Mungu ajaalie kupatikana kwa chanjo, ambayo sasa imepatikana.

“Tulimuomba Mungu ajaalie kupatikana kwa chanjo sasa imepatikana badala ya kutumika watu wameingia katika malumbano ya kusema haya na yale dhidi ya chanjo,” amesema.

“Tusingojee hadi mambo haya yatutinge, tutumie vizuri fursa alizotupa Mungu kujikinga na kujihami na kwa sababu hiyo, sijui ni mapdri wangapi ambao mmeshachanjwa, lakini leo naomba nitoe agizo, kila padre akachanjwe, kila padre akachanjwe, tusifanye utoto, tusifanye lelemama, hii uviko 19 haina mjomba na shemeji na inatuondolea uhai,” amesema Ruwai’chi

Amesema ni utashi wa Mungu kwa watu wawe hai na kuwa na uhai tele hivyo ni vyema kuujali uhai waliopewa.

“Tujihami na tuendelee kumuomba Mungu, atuhurumie na tujihami na atuondolee hili janga,” amesema Ruwai’chi.

Mwananchi
Hilo ni jambo jema. Ni vema na viongozi wa dini zingine waige mfano huu.
 
Hilo ni jambo jema. Ni vema na viongozi wa dini zingine waige mfano huu.
Bakwata na Katoliki ndio mfano bora wa KULIENDELEZA TAIFA HILI NA MSHIKAMANO WAKE...

Abarikiwe sana baba Askofu Ruwa'ichi aaamin aaaamin🙏

#ChanjoNiBoraKulikoTiba
#NchiKwanzaKablaYaYeyoteNaChochote
 
Askofu muongo mkubwa eti Tanzania tuliomba ipatikane Chanjo!!! Huyu Askofu mmmmmm.Kweli Ni sahihi kuitwa Yuda Ni Yuda Iscariote hasa

Sisi tuliomba Corona iondoke Tanzania hatujawaji omba tukaitaja chanjo midomoni mwetu tulipoomba kipindi Cha Magufuli

Yeye aliomba Nini? Si alisema tusikilize wanasayansi ? Hata hayo maombi ya kuomba changing alifanya wapi? Askofu muongo huyu looo.Eti watanzania tuliomba ipatikane Chanjo!!!! Askofu acha uongo
Jumbe Brown Yehodaya unaongea ujinga mtupu au ni dalili ya kukurupuka,Askofu amesema mwaka jana 2020 waumini wa RC walimwomba Mwenyezi MUNGU chanjo ipatikane na imepatikana,na hvyo anawashauri mapadre wakachome chanjo-Punguza mihemuko
 
Askofu kasema tuliomba chanjo kaweka uwingi

Ina maana Sio Siri ndani ya Jimbo la Dar es salaam .Maana Akisema tuliomba Chanjo Ina maana hiyo hadhira ilihusika aliyohutubia

Nani ndani ya Katoliki aliomba na huyo Askofu kuombea chanjo? Muongo ataje hata padri au sista au bruda yeyote waliyeomba naye.Muongo
Ficha ujinga mkuu,sala ya kuombea janga la CORONA iliidhinishwa na TEC na ilikuwa inasaliwa makanisa yote katoliki Tanzania.Sasa ulitaka waje wakusalie na huko msikitini kwako wakati wewe siyo mroma?
 
Back
Top Bottom