Damu ya hedhi na ibada za kiimani

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,514
Nitangulie kuomba radhi kwa wale watakaokereka na hii mada..Nina heshima kubwa kwa akina mama wote na privacy yao..naomba tuichukulie hii kwa muktadha wa maarifa, elimu na ufunuo wa dunia ya upande wa imani
Makuzi yetu yametulea kutufundisha kwamba damu husika ni uchafu na jambo la Siri sana... Wahusika kwenye hili hufanya ni jambo la siri huku wengine wakijichukia kabisa

Kwa dhima ya udugu wa kishetani damu ya hedhi ni kitu cha thamani kubwa kwakuwa imebeba uhai nguvu na kiwakilishi cha maisha marefu, ikijulikana kama nyota ya moto kiashiria cha mungu mwezi...kwenye ibada za kishetani alama nyekundu ni kiwakilishi cha hiyo damu na hata wale ANNUNAKI(malaika walioanguka) wanaichukulia kama dhahabu ya miungu kwa imani yao

Hedhi mzunguko wake unatawaliwa na mizunguko ya mwezi na kuna mahusiano ya moja kwa moja kati ya damu ya hedhi mzunguko wa mwezi na mwanamke!
Kwa wenzetu wahindi hii wanaita SOMA na Greece ikijulikana kama AMBROSIA...Tafsiri kwa muktadha wao ikiwa asali ya miungu. ...

Mwezi ni alama ya makazi ya mungu na malaika wa kike. Hivyo basi ibada yoyote inayouhusika na kunywa damu ya hedhi, hiyo ni ibada ya kuabudu mwezi kwa maana ya kumuabudu mwanamke

Hapa kuna mifakarano kwa baadhi ya wayahudi kwakuwa baadhi yao hupenda kufuata kalenda ya mwezi na hata miungu yao mingi ikiwa ni masanamu ya kike lakini wale wanaojiita Israeties wakipinga hilo kwakuwa wanaamini anayepaswa kuabudiwa ni mungu jua hivyo kuabudu mwezi ni kuruhusu kutawaliwa na mwanamke....

Tukiachana na hao hapa kwetu damu ya hedhi hutumika kutengeneza dawa za mvuto wa kimapenzi na ishu za kishirikina kufarakanisha ama hata kupatanisha...!

Vyovyote iwavyo hiki tunachodhani ni uchafu kina siri yenye nguvu kubwa kwenye ulimwengu wa roho
mooncycle1.jpg
 
Tukiachana na hao hapa kwetu damu ya hedhi hutumika kutengeneza dawa za mvuto wa kimapenzi na ishu za kishirikina kufarakanisha ama hata kupatanisha...!
je dawa hizo zinatengenezewa na damu mbichi ya hedhi au iliyokauka? Je mchawi anaeza kukudhuru kupitia pedi iliyotumika? tuanzie hapo.
 
Tukiachana na hao hapa kwetu damu ya hedhi hutumika kutengeneza dawa za mvuto wa kimapenzi na ishu za kishirikina kufarakanisha ama hata kupatanisha...!
je dawa hizo zinatengenezewa na damu mbichi ya hedhi au iliyokauka? Je mchawi anaeza kukudhuru kupitia pedi iliyotumika? tuanzie hapo.
Preferable mbichi epuka kabisa kuexpose ile kitu si kwa mchawi tu hata adui
 
Preferable mbichi epuka kabisa kuexpose ile kitu si kwa mchawi tu hata adui
Kutokana na mazingira ya mjini wengi wetu tunazitupa kwenye public toilet,hatuna mahala pa kuchomea! je tutafanyaje kujilinda na wachawi au adui? au tusubiri zikauke...
 
Mh! Kwa wanawake nawaonya kuruhusu tendo la ndoa ukiwa ktk siku hizi. kwani wanaume huzitumia damu hizi kuwaibia nyota (mwezi katika astrology) wanawake wenye nyota nzuri za kuzaliwa nazo.
 
Asante Mshana Jr kwa hii mambo
@ Charty...
namna yakutupa inashauriwa uzichome Moto au Loweka kwenye Maji then choma....
Kwa wanawake Mchawi akikamata hiyo Kitu inatakiwa Maarifa mengi kujinasua vinginevyo umekwisha
 
Back
Top Bottom