hannibali
JF-Expert Member
- Jul 7, 2020
- 468
- 427
Habari za muda huu wanaJF, niende moja kwa moja kwenye mada
Leo nilienda dispensary moja ( jina linahifadhiwa) kwa tatizo langu binafsi, sasa nilikaa na mama mmoja ambaye ametoka kwa Daktari alikuwa anasumbuliwa na tatizo la UTI, tulikaa pamoja tukawa tunapiga stori mbili tatu yule mama alikuwa ana ujauzito wa miezi mitatu pia.
Nilitahamaki kuona aina ya dawa ambazo alikuwa amepewa na daktari; dawa zilikuwa na composition za namna hii. Doxycycline. 100mg
Acid bacillus 60 spores Mecoson.
Dawa hii ipo katika mfumo wa kitaalamu kama capsule. Dawa hii ina uwezo wa kuingilia mfumo wa utengenezwaji wa mtoto ikitumiwa katika miezi mitatu ya mwanzo ya mimba na madhara yake inaweza kusababisha mtoto kuzaliwa akiwa na viungo dhaifu na mara nyingine hata ulemavu.
Nilimuuliza huyu mama kwamba kwanini daktari amekupa dawa hii akanambia yeye hajui nikamuuliza au hajui hali yako akanambia anajua hali yangu na alishamwambia.
Nikaona ngoja niende kwa daktari huyo kumuhoji vizuri kwanini aliamua kumpa dawa hizi. Kwakweli nilistaajabu kuona daktari hana majibu ya kueleweka zaidi ya janja janja za hapa na pale. Kwakweli niliondoka nae yule mama kwenda kumchukulia dawa sehemu nyingine sikuweza kuvumilia kwani yale yalikuwa kama mauaji.
Leo nilienda dispensary moja ( jina linahifadhiwa) kwa tatizo langu binafsi, sasa nilikaa na mama mmoja ambaye ametoka kwa Daktari alikuwa anasumbuliwa na tatizo la UTI, tulikaa pamoja tukawa tunapiga stori mbili tatu yule mama alikuwa ana ujauzito wa miezi mitatu pia.
Nilitahamaki kuona aina ya dawa ambazo alikuwa amepewa na daktari; dawa zilikuwa na composition za namna hii. Doxycycline. 100mg
Acid bacillus 60 spores Mecoson.
Dawa hii ipo katika mfumo wa kitaalamu kama capsule. Dawa hii ina uwezo wa kuingilia mfumo wa utengenezwaji wa mtoto ikitumiwa katika miezi mitatu ya mwanzo ya mimba na madhara yake inaweza kusababisha mtoto kuzaliwa akiwa na viungo dhaifu na mara nyingine hata ulemavu.
Nilimuuliza huyu mama kwamba kwanini daktari amekupa dawa hii akanambia yeye hajui nikamuuliza au hajui hali yako akanambia anajua hali yangu na alishamwambia.
Nikaona ngoja niende kwa daktari huyo kumuhoji vizuri kwanini aliamua kumpa dawa hizi. Kwakweli nilistaajabu kuona daktari hana majibu ya kueleweka zaidi ya janja janja za hapa na pale. Kwakweli niliondoka nae yule mama kwenda kumchukulia dawa sehemu nyingine sikuweza kuvumilia kwani yale yalikuwa kama mauaji.