Dakika 45 ITV: Jobu Ndugai apasua siri jinsi nchi inavyofilisiwa na serikali iliyoko madarakani

Magamba Matatu(3) na Wana JF,
Hii ndio tatizo la Wabunge wa Chama Tawala kuwa wengi na kupitisha kila kitu hata kama kibaya, kuna haja ya kuwa na Wabunge wengi wa Upinzani watakaoleta Ushindani wa Hoja. Huu ni Uoga wa hali ya juu, Mh Ndugai kwanza ni mzoefu wa miaka mingi, anajua kinachoendelea ana cheo cha Unaibu Spika, sasa atashindwaje kukemea na kubadilisha mambo yote yasiyokuwa na tija na Taifa letu, au analinda kibarua chake ?? Anataka kujisafisha kuwa wao Wabunge wanalipwa kidogo kuliko mihimili mingine yaani Serikali na Mahakama ?? Tuacheni Siasa za kinafiki, tujenge Nchi yetu.
My Take: Tunamtaka Mh Ndugai atuambie Mahakama na Serikali Viongozi wao wanalipwa Posho Tshs ngapi ?? Ili wananchi ambao ndio wenye Nchi tuamue !!! otherwise Samaki mmoja akioza wote wameoza. Sipo Upande wowote haya ni Maoni na Mawazo yangu tu
Nawakilisha

Lakini kasema kuwa siyo vizurikutaja posho za watu, ila cha msingi kasisitiza kuwa kama watanzania wakijua posho hizo wanazolipwa hiyo mihimili ya mahakama na serikali basi watajinyonga tena sana, ila ilikuwa imebaki kidogo aanze kuzitaja hizo posho baada ya mtangazaji kumbana ila akagundua angekiweka kitumbua chake rehani akasema hawezi kuweka mambo hadharani kama alivyoweka mshahara wa Mh waziri mstaafu Sumaye, Ndugai alidai kuwa Sumaye anapta posho kama za wabunge japo kastaafu,, duuu nilitamani hiki kipindi kiwe dakika 90 na siyo 45 kwani Ndugai alikuwa anaelekea kumwaga kila kitu.
 
Binafsi sijaweza kufahamu kwa nini watu wanalipwa Tz 150,000 kama mshahara wao serikalini, ukiwambia hautoshi wanakushangaa! Na ukichunguza maisha yao si wafanya biashara lakini wana nyumba magari na watoto wanasoma shule za gharama! Kwa mtindo huu wa Job nimefahamu kuwa usiri wa serikali ndo maana watu tunaibiwa! Sasa imagine badala ya Job ku-justify posho wanayopeana wabunge yeye anasema zipo posho nyingine mkizifahamu watz mtajinyonga! Kwa maana nyingine, yeye anatushangaa kwa kuwa mbumbumbu kuhusu namna wakubwa wanakula nchi. Swali la kujiuliza hapa ni je...Kazi ya Posho ni nini? Na Kazi ya Mshahara ni nini? Kwa sisi tulio wengi, Posho ni malipo haramu endapo inalipwa kama ziada ya fedha ya kujikimu - I mean Daily Subsistance Allowance (DSA). Kwa maana nyingine, hakuna mtu anayeweza ku-justify malipo ya posho iwe ndogo au kubwa,,,,kwa kuwa ni wizi wa aina fulani. Ndo maana wakati fulani (sijui siku hizi) wafadhili walikuwa wanaiambia serikali kama ni mambo ya posho tumia makusanyo yako ya ndani wala si fedha zetu za misaada!
Lakini jambo jingine ninalolisoma hapa kwenye kauri ya mh Job ni kwamba kumbe mtu anaweza kutumia gharama ku-justify upotofu. Kimsingi uwepo wa miposho mingine kwa mihimili mingine hakuondoi MAUMIVU tunayoyapata sisi walipa kodi....na hasa zile za PAYEE na kwenye mafuta! Hii inauma sana na si haki hata mbele za Mungu kutukamua sisi na kisha nyinyi viongozi kujipangia mlipwe kiasi gani kutokana na jasho letu! This is not acceptable!
Kahiyo hoja ni kwamba Bunge sio wahujumu pekee. Je swali ni kwamba kiwango wanacholipwa wabunge ni haki kwa nchi masikini kama Tanzania?
 
Kwa hiyo ukimwona jambazi anapora na wewe unakuwa jambazi ili upore? Ujinga. Nyie kuleni hela za wavuja jasho wasio kula jasho lao, Mungu hawezi kusamehe upuuzi huu. Hivi hakuna kiongozi hata mmoja serikalini mwenye akili timamu?

Hivi Bunge si ndio linasimamia Serikali? Kwa nini Bunge liiskemee serikali kuacha kulipana posho badala yake na wao wanaingia kwenye huo mtego wa posho. Ukiwa ni oversight institution unatakiwa ujitenge na vitu vinavyoweza kukunyimna moral authority ya kuwakemea unaowasimamia. Kama bunge linasema na sisi tulipwe kama watu wa serikali badala ya kukemea hizo posho zinazoifilisi serikali basi Bunge limekosa moral authority na halipo kwa ajili ya wakulima, wakwezi, wavuvi, nk. Bunge sasa ndilo linatufilisi kwa kuwa tumewatuma wakaisimamie serikali yetu kwa niaba yetu wao wanaenda kuungana na serikali kula posho!! Hapa mbaya ni Bunge na wala si serikali.

Bunge linatuingiza hasara!!
 
Huyo Ndugai hana jipya, yeye na Makinda walipaswa kuliongoza Bunge kukataa posho na baadae wangeweza kuisimamia uondoaji wa baadhi ya posho kwenye Serikali na Mahakama. Anachothibitisha sasa ni ulafi wa Wabunge kwa kisingizio cha "mihimili mingine pia kufanya jambo hilo."
 
Job Ndugai kanisikitisha.
Nae anaingia kwenye orodha ya magamba yasiyofaa kuwa viongozi wa uma.
How the hell did he become a deputy speaker?
OTIS


beacuse he can be used and manipulated by the FISADIS the way the want.
Otherwise, they would not let him be a deputy speaker....
 
Huyo Ndugai hana jipya, yeye na Makinda walipaswa kuliongoza Bunge kukataa posho na baadae wangeweza kuisimamia uondoaji wa baadhi ya posho kwenye Serikali na Mahakama. Anachothibitisha sasa ni ulafi wa Wabunge kwa kisingizio cha "mihimili mingine pia kufanya jambo hilo."


Sijawahi na sitegemei kusikia Mtz anakataa pesa. Wao wana shida gani, wajinga ndio waliwao.
 
Hapa kuna tatizo la mashindano. Kwa kuwa walioko serikalini na mahakamani wanapokea nyingi ngoja na sisi tuwakomoe hawa wananchi kwa kupata nyingi. Swali langu ni kuwa wale wasio na sauti ni nani atawasemea? nani anajali kuumia kwa mnyonge nchi hii? Ndiyo maana sasa kila mwenye nguvu ameamua kufanya atakavyo kwa sababu tu ana nguvu. Watanzania na serikali yetu! Tumekwisha.....!!!!!!!!!!!!!! wanafunzi jiandaeni kufukuzwa zaidi. Madaktari jiandaeni kuumizwa zaidi, Tanesco wiki ijayo watapandisha tena kwa sababu wananguvu ya EWURA . Ushawahi kusikia juu ya nchi inayowala watu wake? Ni Tanzania ya KIKWETE!!!!!
 
Lakini kasema kuwa siyo vizurikutaja posho za watu, ila cha msingi kasisitiza kuwa kama watanzania wakijua posho hizo wanazolipwa hiyo mihimili ya mahakama na serikali basi watajinyonga tena sana, ila ilikuwa imebaki kidogo aanze kuzitaja hizo posho baada ya mtangazaji kumbana ila akagundua angekiweka kitumbua chake rehani akasema hawezi kuweka mambo hadharani kama alivyoweka mshahara wa Mh waziri mstaafu Sumaye, Ndugai alidai kuwa Sumaye anapta posho kama za wabunge japo kastaafu,, duuu nilitamani hiki kipindi kiwe dakika 90 na siyo 45 kwani Ndugai alikuwa anaelekea kumwaga kila kitu.

Nimegundua kwamba ana uwezo mdogo sana wa kujenga hoja. Alitumia muda kuelezea lile ambalo hakuulizwa, na bahati mbaya mtangazaji pia alimwacha, hatujui labda kwa kumtega ili aropoke lolote tu! kwa mtindo wa taarifa yoyote inaweza kuwa ya muhimu kwetu! Na hapo ndo akagusia kuhusu pesa wanazolipana TANAPA, TRA, NSSF kwa kusema kwamba pesa za wabunge, analipwa mfanyakazi wa level za kawaida tu katika mashirika haya. hapo tujiiulize wa juu inakuaje?!
Angepaswa kujibu swali la kwa nini anadhani wanastahili kulipwa posho walizojiongezea! sio kuhalalisha kosa kwa makosa mengine, wazungu wanasema 'two wrongs don't make one right'

 
Napingana na Job kujustify wizi kwa sababu wengine wanaiba pia. hebu tuwe na huruma kwa watanzania itafika mahala tutagoma kulipa kodi sijui mtajisikiaje. Nalaumu wengi wa sisi watanganyika tuna nidhamu ya uoga. Kwa upande wa posho ktk mihimili mingine atuambie ni kiwango gani cha posho wanazopata mwenye dondoo atuwekee kidogo. Mimi huwa naona kuna kitu hii inaitwa per DM if am not wrong kwa mfanyakazi wa kawaida aendae nje ya nchi ni zaidi ya dola 600 kwa siku x 1600 =96000 Kwa JK na timu yake? Inawezekana wabunge wengi hawapati hii kwa sababu vikao vyafanyika dodoma ambayo ni ndani ya nchi. Halafu tunadanganywa kwamba sisi ni waajiri wao thubutu? Mwajili gani hajui mfanyakazi wake anajilipa ngapi?
 
Pamoja na kumlaumu Ndugai, kuna haja y akuyajadili aliyoyasema pia. Jamani hii nchi imefikia mahali ambapo kila mtu anakufa na chake. Ndugai anayoyasema ni kweli wala hayana ubishi. Juzi tu kuna Assistance mmoja alihudhuria kikao kwa niaba ya bosi wake wizarani, alirudi baada ya masaa mawili na machozi usoni!!!!!!!

Analia kwani baada ya kikao cha masaa mawili walipewa bahasha yenye shilingi za kitanzania 800,000/= (laki nane) posho ya kikao!!! Aliposhangaa akaambiwa ni kwa kikao hiki tu lakini vingine posho yetu huwa shilingi millioni moja na laki mbili!!!

Ndugai anamaanisha anachokisema! Tukiyaona na kuyajua tutajinyonga kama sio kuipiga nchi kiberitii tukose wote...
 
Hivi Bunge si ndio linasimamia Serikali? Kwa nini Bunge liiskemee serikali kuacha kulipana posho badala yake na wao wanaingia kwenye huo mtego wa posho. Ukiwa ni oversight institution unatakiwa ujitenge na vitu vinavyoweza kukunyimna moral authority ya kuwakemea unaowasimamia. Kama bunge linasema na sisi tulipwe kama watu wa serikali badala ya kukemea hizo posho zinazoifilisi serikali basi Bunge limekosa moral authority na halipo kwa ajili ya wakulima, wakwezi, wavuvi, nk. Bunge sasa ndilo linatufilisi kwa kuwa tumewatuma wakaisimamie serikali yetu kwa niaba yetu wao wanaenda kuungana na serikali kula posho!! Hapa mbaya ni Bunge na wala si serikali.

Bunge linatuingiza hasara!!

si bunge linalokutana dodoma
 
Pamoja na kumlaumu Ndugai, kuna haja y akuyajadili aliyoyasema pia. Jamani hii nchi imefikia mahali ambapo kila mtu anakufa na chake. Ndugai anayoyasema ni kweli wala hayana ubishi. Juzi tu kuna Assistance mmoja alihudhuria kikao kwa niaba ya bosi wake wizarani, alirudi baada ya masaa mawili na machozi usoni!!!!!!!

Analia kwani baada ya kikao cha masaa mawili walipewa bahasha yenye shilingi za kitanzania 800,000/= (laki nane) posho ya kikao!!! Aliposhangaa akaambiwa ni kwa kikao hiki tu lakini vingine posho yetu huwa shilingi millioni moja na laki mbili!!!

Ndugai anamaanisha anachokisema! Tukiyaona na kuyajua tutajinyonga kama sio kuipiga nchi kiberitii tukose wote...

kulaleki,
kweli hii dhahama
 
Ndugai asifananishe majaji na wabunge, majaji ni proffesional wakati wabunge ni siasa tu mdomoni. kweli ccm imekuwa kila kiongozi ni kambale, mtoto ana ndevu, mama ana mdevu na baba ana ndevu. hakuna kuheshimiana.

Ndugu yangu inawezekana katika mazingira ya utawala wa sheria lakini katika nchi hii sidhani kama inaangaliwa professionalism. Nitoe mfano wa uteuzi wa Jaji mkuu katika kipindi hiki kama kweli ilizingatiwa hiyo hali kwamba ni muda gani huyu jamaa amekuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa mpaka kustahili kupata uJaji Mkuu? Lakini vilevile kama kulipwa kiwango kikubwa ni sababu ya profession je Waziri Mkuu anatakiwa kua na utaalam gani kiasi cha kustahili akiacha/akistaafu alipwe 80% ya mshahara wa WM aliyepo kazini? Fungua macho ndugu yangu jiulize kama profession inazingatiwa kwa nini maprofessor wanaacha kazi zao na kukimbilia ubunge. Ukipata jibu unaweza kuelewa kwanini Ndugai anazungumzia namna hiyo. Ni maslahi binafsi tu yanayowasukuma.
 
Job Ndugai kanisikitisha.
Nae anaingia kwenye orodha ya magamba yasiyofaa kuwa viongozi wa uma.
How the hell did he become a deputy speaker?
OTIS

Mkuu swali lako zuri sana hiyo ndio ilikuwa matunda ya RA na Lowassa ndio walimpa hiyo nafasi na Anna Makinda kumkomoa Sita
 
Kwa hio kwasababu wapo hao wanaolipwa hivyo basi na wao kujilipa mamilioni sio tatizo eeeh, no ni yale yale ya kujustify upuuzi na ujinga
 
Naibu Spika Jobu Ndugai amedai kuwa watanzania inabidi wasilaumu sana wabunge kuongezewa posho, Ndugai kasema kuwa kuna muhimili mitatu ya nchi ambayo niBUNGE, SERIKALI NAMAHAKAMA, Ndugai kasema kama watanzania wangejua ni kiasi cha posho kubwa wanacholipwa viongozi wa seikali na mahakama basi watanzania wangejinyonga kabisa badala ya kulaumu hizi wabunge ambacho ambacho kadai kuwa ni kidogo kuliko wananchi wanavyofikilia,

Hii kauli ya Ndugai ilimshitua hadi mtangazaji baada ya kusikia kuwa nchi hii kuna zaiudi ya maefu ya wafanyakazi wanapokea posho za kutisha kuliko hata wabunge, Ndugai kadai wabunge ni wafanyakazi wasiozidi hata 350 lakini ndoo wamenyooshewa kidole na waandishi wa habari bila kufahamu kuwa kuna posho zinalipwa mara 10 zaidi ya hizo zao kwa siku na kudai kuwa ni maelfu ya wafanyakazi wa mihimili ya serikali na mahakama na hii ndoo imefanya hadi wabunge waamue kujiongezea.

Huyo ndoo Ndugai kaamua kutoboa siri iliyojificha, ama kweli kumbe wafanyakazi wanaweza kulipwa kima cha chini kisichopungua 350000, hapa ndoo nimeamini baada ya Ndugai kumwaga mboga,.

Nilkuwa sijui kama wabunge ni wafanyakazi. Kumbe ukipigiwa kura unapata ajira? Huyu jamaa nadhani uwezo wake wa kuelewa ni mdogo sana unless amenukuliwa vibaya......kazi za kuchaguliwa mara nyingi zinapaswa kuwa za kujitolea
 
Back
Top Bottom