Dah! Leo nimeponenea chupchup, asanteni sana Polisi

The Genius

JF-Expert Member
May 29, 2018
820
2,070
Wapendwa leo kuna tukio la kuhuzunisha limenitokea. Nilikuwa nimesimama maeneo ya Morocco nikisubiri gari, ghafla nikamuona mama mtu mzima analia kwa sauti kubwa, mda huo huo nilikuwa nimeshika simu yangu nachati na mtu. Ikanibidi nisogee karibu ili nijue ni nini kimemtokea yule mama, kumbe yule mama ameibiwa simu yake basi aliponiona mimi akasema simu yake aliyoibiwa mimi ndo nimeishikilia.

Watu wakaanza kunipiga kwa silaha mbalimbali na kuniumiza vibaya sana lakini nashukuru Mungu askari walikuwa karibu na walifika eneo la tukio na kunichukua mimi pamoja na yule mama na kutupeleka kituoni. Baada ya kufika kituoni yule mama akapewa simu na afande ili apige kwenye ile simu yangu wahakikishe kama simu niya yule mama au lah!. Basi akapiga simu yake haikuita kwenye ile simu yangu aliyodai ni yake, bali iliita huko kwake na kupokelewa na dada wa kazi. Kumbe yule mama alidhani mimi nimemuibia simu yake maana ilifanana na yake.

Polisi wakashauri tuelewane pale pale, huwezi amini yule mama alitaka kunipa Milioni 40 cash kama fidia.
Bahati mbaya mkojo ukanibana ikabidi niamke kwenye hii ndoto na kwenda kukujoa chooni.

Hili liwe fundisho kwa watu wote, kabla hujalala msinywe maji mengi ili msije mkakosa dili la hela kama hili. .
 
Back
Top Bottom