Leo nimejuta kupanda daladala

LIKUD

JF-Expert Member
Dec 26, 2012
15,121
27,128
Katikati ya safari si akapanda jamaa mmoja akawa anaongea kwenye simu na mwenzake. Namnukuu ( nukuu yangu ni baada ya jamaa kuongea kwenye simu kuhusu mada hiyo kwa kama dakika 20 hivi)

" Basi bana yule binti wangu wa kufikia Naa ambae yupo form four mwaka huu akawa amepotea nyumbani.

Siku hiyo ilikuwa jumamosi mtoto kaenda sokoni hakurudi.

Usiku hatukulala. Tukaanza kuhangaika polisi na hospitali kote huko hatukufanikiwa.

Siku 4 zote bila bila.

Baadae mke wangu akashawishiwa na rafiki zake waende kwa mganga.

Mganga akawaambia Naa ametekwa na wachawi na hao wachawi wana taka kumtoa sadaka kwa jitu kubwa ( limsukule) limnyonye damu .

Lilikuwa linasubiri siku ya saba ifike tu limnyonye damu na hiyo ilikuwa siku ya 5 so 2 days are loading. Mke wangu kusikia hivyo kazimia. Alipo zinduka wakanipigia simu kuniambia hiyo taarifa. Mke wangu kapanic vibaya sana.

Na Mimi kama unavyo nijua ndugu yangu mambo ya kipuuzi puuzi ( uchawi) huwaga siamini kabisa. So nikamwambia mke wangu hebu Achana na hayo mambo Naa atarudi tu kama ni kumtafuta tutumie njia nyingine sio hizo.

Mke wangu akaniambia " ooh au kwa sababu sio Mtoto wako?"

Siku hiyo sikulala kwa amani nyumbani mke wangu anakesha analia kesho yake asubuhi hakula siku nzima anasema twende tukamsikilize mganga Anacho kitaka. Mimi msimamo wangu ukawa pale pale. Mara ikafika siku ya saba ambayo ndio mganga alisema Naa ananyonywa damu na hilo lijitu.. kweli bana siku hiyo mida kama ya saa 7 mchana tukapigiwa simu na mama mkwe wangu analia anamtaja Naa. Mke wangu kusikia mama ake analia huku anamtaja Naa na yeye akazimia ... Nilipomuuliza mama mkwe kuna nini, akaniambia.....

STORY IKAKATISHWA,MPIGA STORY AKASEMA " KONDA ZUIA HAPA NIMEFIKA"

Abiria wote tulibaki na huzuni hatujui story imeishia wapi...

Ulivyo sikitika wewe kutoa jua muendelezo wa hiyo story ndio na Mimi nilivyo sikitika hivyo hivyo. Nimeileta hii story hapa ili tusikitike wote.

Nyie mnaopiga story za hivi muwege mnazimalizia basi wajameni
 
Katikati ya safari si akapanda jamaa mmoja akawa anaongea kwenye simu na mwenzake. Namnukuu ( nukuu yangu ni baada ya jamaa kuongea kwenye simu kuhusu mada hiyo kwa kama dakika 20 hivi)...
Nimeshawahi kukaa uswahilini sana, mtoto akipotea utakuta wanasema twende kwa mtaalamu. imani za kishirikina tupu, wamemwacha Mungu wa kweli anayeweza kutatua matatizo yao wanang'ang'ania kwa wachawi, hii kufuru jueni kuwa kuna siku Mungu atawahukumia adhabu.
 
I think, It's not about making the right call. It's about making a call and making it right....🤨
 
Back
Top Bottom