Dada wa kazi anajua ratiba zangu kuliko Mke wangu!

Usiingie kwenye huo mtego. Mwondoe haraka sana utafute ambaye atatekeleza maelekezo ya bosi wake (mkeo) bila kuzidisha au kupunguza.

Asithubutu kuizidi huduma ya mkeo kwa namna yoyote. Kuhusu kukuhudumia wewe, apigwe marufuku, na afanye hivyo kama akitumwa.

Naamini utauelewa ushauri wangu.
Daaaahhhh yaani mtu anaonyesha bidii na kujituma kwenye kazi yake ili apate rizki yake halafu wewe unashauri amuondoe(amfukuze) kazi ni haki kweli?
Unajua katika huo mshahara anaoupata kuna watu wangapi nyuma yake wanamtegemea?
Hapo kwa ushauri wangu ni bora amuongezee mshahara ili kumpa molari zaidi kwenye kazi na kumfanya aone jitihada yake inathaminiwa.
 
Daaaahhhh yaani mtu anaonyesha bidii na kujituma kwenye kazi yake ili apate rizki yake halafu wewe unashauri amuondoe(amfukuze) kazi ni haki kweli?
Unajua katika huo mshahara anaoupata kuna watu wangapi nyuma yake wanamtegemea?
Hapo kwa ushauri wangu ni bora amuongezee mshahara ili kumpa molari zaidi kwenye kazi na kumfanya aone jitihada yake inathaminiwa.
Ni maamuzi yake pia. Ana uhuru wa kuchagua
 
Usiingie kwenye huo mtego. Mwondoe haraka sana utafute ambaye atatekeleza maelekezo ya bosi wake (mkeo) bila kuzidisha au kupunguza.

Asithubutu kuizidi huduma ya mkeo kwa namna yoyote. Kuhusu kukuhudumia wewe, apigwe marufuku, na afanye hivyo kama akitumwa.

Naamini utauelewa ushauri wangu.
Hajui kuwa kuna housegirls wanakuja nyumba za watu kuvuruga tu ndoa kujifanya wanajua caring kumbe wanawinda.....bora tu afukuze mapema kabla ya kufikwa na aibu.
 
Daaaahhhh yaani mtu anaonyesha bidii na kujituma kwenye kazi yake ili apate rizki yake halafu wewe unashauri amuondoe(amfukuze) kazi ni haki kweli?
Unajua katika huo mshahara anaoupata kuna watu wangapi nyuma yake wanamtegemea?
Hapo kwa ushauri wangu ni bora amuongezee mshahara ili kumpa molari zaidi kwenye kazi na kumfanya aone jitihada yake inathaminiwa.
Ulivyosema pia inawezekana ni kujituma ila
na vp km kaja kwa malengo yake binafsi? Labda tujue kabila gani huyo msichana kwanza.
 
Habari za weekend!

Kama ilivyoa ada. Mimi ni mtu mzima kiasi nina mke na watoto wawili. Nyumbani mke wangu anajituma si kwamba ni mvivu la hasha. Anafanya mambo yote kama mke. Lakini kuna jambo moja linanishangaza, hivi karibuni tumepata msichana wa kazi hana muda mrefu ni kama miezi miwili lakini tangu amefika nimeona mabadiliko ya ghafla sana.

1. Haambiwi kitu huwa anafanya kabla hujamuuliza mf. nimezoea kumwambia mke wangu nitayarishie maji ya kuoga. Yeye kabla hujasema unakuta tayari ameshaandaa.

2. Hasubiri nimwambie nataka chai au chakula nikitoka tuu kama ni asubuhi tayari ameshaniandalia chai mezani hivyo hivyo nikirudi nyumbani ananiwekea chakula mezani. Mke wangu mpaka nimwambie. Nimeona tofauti kubwa sana ya mkewangu na huyu dada wa kazi.

Ni hayo tuu.
Ndio maana akawa dada wa kazi..hayo ni majukumu yake!
 
Kuna mwanasaikolojia mmoja alisema kila mwanaume anatafsiri yake kuhusu kuheshimiwa na kupendwa na mwanamke..unajua jambo hilo hadi umeleta hapa means limekugusa sana hadi ndani ya moyo wako...kitendo cha kufanyiwa jambo na mwanamke(house girl) bila kumwambia ni jambo lilokuvutia na kuona ni kitu unahitaji kifanyike ...huyo housegirl akiongeza kasi tu kidogo basi atauteka moyo wako.
 
Back
Top Bottom