GAZETI
JF-Expert Member
- Feb 24, 2011
- 5,277
- 6,673
Habarini wana JF, Majuma kama matatu yaliyopita dadaangu ambaye ni mtoto wa rafiki mkubwa wa mama yangu mzazi alifanya jaribio la kumuua mtoto wake wa kumzaa. Tatizo ni kwamba alipata ujauzito baada ya Kubakwa na kijana fulani (Ametoroka yasemekana anaonekana mkoani Arusha ni dereva tax kwa sasa), huyo dadaangu ni mwalimu na huyo mtoto ana miaka mitatu. Ilibidi itumike mbinu isiyo rasmi kuwapoza Polisi. Hata hivyo baada ya kuhojiwa na watu wa karibu anasema kuwa huwa anasikia hasira sana kila anapomuona yule mtoto na anamchukia kutoka moyoni Kwani amefanana sana na baba mbakaji. Kikubwa kingine kinachomfanya amchukie ni kuwa uchumba wake ulivunjika baada ya kupata mimba hiyo iliyotokana na kubakwa. Mchumaake alikuwa masomoni South Africa aliporudi na kulikuta hilo akaghairi
YUKO SAHIHI KUMCHUKIA MWANAE KWA KUWA ALIPATIKANA BAADA YA KUBAKWA?
YUKO SAHIHI KUMCHUKIA MWANAE KWA KUWA ALIPATIKANA BAADA YA KUBAKWA?