Mpwayungu Village
JF-Expert Member
- Jul 21, 2021
- 14,304
- 29,835
Samahani kwa kutokusalimia.
Nipo katika tafakuri nzito yenye sonono ndani ya moyo wangu, binafsi nikionaga mwafrika ananyanyasika ndani ya nchi yake moyo wangu huwa unalipuka na kukosa amani kabisa. Kama mna kumbukumbu kuna siku niliwahi kutoa thread kulaani na kulalamika kwa nilichokikuta nilipoenda kumtembelea Dada angu na kukuta wanamnyanyasa na kumpa kipolo cha wali wa kwenye friji wao wanakula cha siku hiyo kikiwa cha moto na mpishi ni dada angu ila kula chakula kilichopikwa siku hiyo hatakiwi, sio taratibu ni sheria.
Sasa Jana nilienda kumuona tena Upanga, nilichokikuta sikuamini macho yangu mpaka nilipovua miwani ndipo nikajua haikuwa illusion Bali ni ukweli wa macho ya nyama. Nikifika saa saba mchana akanipokea nikakaa sebleni, nilipofika nilimkuta yeye na wakaka fulani ni wahindi lakini cha ajabu niliposalimia hawakupokea wao wakawa busy kuangalia movie kwenye laptop, nikajua hawajaskia nikasalimia tena kwa sauti nikaona wamenitazama ila ni mmoja tu akapokea salamu kwa tabu sana tena sauti ya chini ila kwa kuwa sio jambo geni Kwangu sikujali.
Ajabu nilichokiona Kuna watoto walitoka shuleni kuingia tu nikaona mmoja kaenda kwa Dada bila kunisalimia akaanza kumshika matiti mwingine wa pili akijalibu kumkatia kiuno huku akiguniza ashiii ashiii ashiiit, nikajisemea huu upuuzi siwezi kuuvumilia, nikawaambia kuweni na adabu lakini cha ajabu mmoja akaenda kumsukuma kichwa Dada angu akisema tumiminie Chai hujui tumetoka shule tuna njaa?. Wale waliokuwa wanaangalia movie wakaingia ndani huku wakilalama kwa lugha zao wakuonesha kukwazika kwa uwepo wangu.
Dakika tano baadae akaingia mama mwenye nyumba kwa mujibu wa Dada angu alivoniambia, alipoingia nilisalimia lakini hakupokea ila akamwambia Dada yangu tutoke ndani twende nje anataka apumzike sebleni. Nilijiskia huzuni kuona hawathamini wageni wa mfanyakazi na wanatutreat kama wanyama ilihali wao ni wahindi na sisi ni watanzania wazawa wenye nchi yetu.
USHAURI : Dada zangu napiga magoti kuwaomba msije kwenda nchi yoyote ya kiarabu au kwa wahindi kule utaishi kama mnyama, please kama ni kazi tafuta ndani ya Africa our motherland. Africa ni nzuri yenye uadilifu mkubwa na upendo ni Bara lenye bahari, maziwa, mito, mabwawa, milima, mabonde, mazao ya kutosha, ardhi yenye rutba na mifugo ya kila aina, Madini ya kutosha, our Africa is blessed jamani kwa wahindi mnatafuta nini jamani .
Nipo katika tafakuri nzito yenye sonono ndani ya moyo wangu, binafsi nikionaga mwafrika ananyanyasika ndani ya nchi yake moyo wangu huwa unalipuka na kukosa amani kabisa. Kama mna kumbukumbu kuna siku niliwahi kutoa thread kulaani na kulalamika kwa nilichokikuta nilipoenda kumtembelea Dada angu na kukuta wanamnyanyasa na kumpa kipolo cha wali wa kwenye friji wao wanakula cha siku hiyo kikiwa cha moto na mpishi ni dada angu ila kula chakula kilichopikwa siku hiyo hatakiwi, sio taratibu ni sheria.
Sasa Jana nilienda kumuona tena Upanga, nilichokikuta sikuamini macho yangu mpaka nilipovua miwani ndipo nikajua haikuwa illusion Bali ni ukweli wa macho ya nyama. Nikifika saa saba mchana akanipokea nikakaa sebleni, nilipofika nilimkuta yeye na wakaka fulani ni wahindi lakini cha ajabu niliposalimia hawakupokea wao wakawa busy kuangalia movie kwenye laptop, nikajua hawajaskia nikasalimia tena kwa sauti nikaona wamenitazama ila ni mmoja tu akapokea salamu kwa tabu sana tena sauti ya chini ila kwa kuwa sio jambo geni Kwangu sikujali.
Ajabu nilichokiona Kuna watoto walitoka shuleni kuingia tu nikaona mmoja kaenda kwa Dada bila kunisalimia akaanza kumshika matiti mwingine wa pili akijalibu kumkatia kiuno huku akiguniza ashiii ashiii ashiiit, nikajisemea huu upuuzi siwezi kuuvumilia, nikawaambia kuweni na adabu lakini cha ajabu mmoja akaenda kumsukuma kichwa Dada angu akisema tumiminie Chai hujui tumetoka shule tuna njaa?. Wale waliokuwa wanaangalia movie wakaingia ndani huku wakilalama kwa lugha zao wakuonesha kukwazika kwa uwepo wangu.
Dakika tano baadae akaingia mama mwenye nyumba kwa mujibu wa Dada angu alivoniambia, alipoingia nilisalimia lakini hakupokea ila akamwambia Dada yangu tutoke ndani twende nje anataka apumzike sebleni. Nilijiskia huzuni kuona hawathamini wageni wa mfanyakazi na wanatutreat kama wanyama ilihali wao ni wahindi na sisi ni watanzania wazawa wenye nchi yetu.
USHAURI : Dada zangu napiga magoti kuwaomba msije kwenda nchi yoyote ya kiarabu au kwa wahindi kule utaishi kama mnyama, please kama ni kazi tafuta ndani ya Africa our motherland. Africa ni nzuri yenye uadilifu mkubwa na upendo ni Bara lenye bahari, maziwa, mito, mabwawa, milima, mabonde, mazao ya kutosha, ardhi yenye rutba na mifugo ya kila aina, Madini ya kutosha, our Africa is blessed jamani kwa wahindi mnatafuta nini jamani .