Antennah
JF-Expert Member
- Oct 14, 2015
- 6,933
- 9,033
Basi bhana leo nimerudi nyumbani baada ya kupiga sana mzigo kwa mwezi mzima katika taasisi fulani.
Kabla sijafika nyumbani nikaona sio mbaya kama nikipitia maeneo fulani kupata moja moto moja baridi.
Kiukweli ilifika point nikawa sijielewi kabisaa basi hapo nikaamua tu niende nyumbani.
Baada ya kufika nyumbani inaonesha niliwapigia simu baadhi ya watu kadhaa kutoka kwenye phone book yangu, sasa shida ni kwamba
Kuna huyu mwanangu anaitwa tonny, mpaka dakika hii ananipigia zaidi ya mara ya nne anapiga simu kunishukuru sana, yani mpaka naona kabisa unyenyekevu mkubwa kwenye sauti yake, na ananiambia eti kesho atakuja nyumbani nimpe info kwa undani zaidi juu ya mchongo niliompatia ili aanze kuutekeleza.
Asichokijua ni kwamba mi sikumbuki lolote na sikumbuki kama kuna mchingo wowote nimeutoa kwa mtu yeyote, mi mwenyewe hapa natamani atokee mtu anipe mchongo, sasa sielewi imekuaje leo mimi ndo nimekua mtoa mchongo.
Ndugu zangu wale wa kula vitu, hebu nisaidieni, itakua nimemuahidi kumpa mchongo wa aina gani huyu janja.
Kabla sijafika nyumbani nikaona sio mbaya kama nikipitia maeneo fulani kupata moja moto moja baridi.
Kiukweli ilifika point nikawa sijielewi kabisaa basi hapo nikaamua tu niende nyumbani.
Baada ya kufika nyumbani inaonesha niliwapigia simu baadhi ya watu kadhaa kutoka kwenye phone book yangu, sasa shida ni kwamba
Kuna huyu mwanangu anaitwa tonny, mpaka dakika hii ananipigia zaidi ya mara ya nne anapiga simu kunishukuru sana, yani mpaka naona kabisa unyenyekevu mkubwa kwenye sauti yake, na ananiambia eti kesho atakuja nyumbani nimpe info kwa undani zaidi juu ya mchongo niliompatia ili aanze kuutekeleza.
Asichokijua ni kwamba mi sikumbuki lolote na sikumbuki kama kuna mchingo wowote nimeutoa kwa mtu yeyote, mi mwenyewe hapa natamani atokee mtu anipe mchongo, sasa sielewi imekuaje leo mimi ndo nimekua mtoa mchongo.
Ndugu zangu wale wa kula vitu, hebu nisaidieni, itakua nimemuahidi kumpa mchongo wa aina gani huyu janja.