CUF yatoa tamko la kuyalaani mauaji ya Daudi Mwangosi

Domy

JF-Expert Member
Dec 12, 2011
4,700
1,086
Mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF ameitaka serikali ya rais Kikwete iwajibike.

Akiongea na DW radio amesema jeshi la polisi haliwezi kukaa kando kutokana na kifo cha kijana DAUD MWANGOSI,Amesema askari aliyelipua bomu anatakiwa kufunguliwa kesi ya mauaji mara moja,

vile vile amehoji kulikuwa na haja gani kumshambulia kwa kumpiga virungu mwandishi wa habari wakati anafahamika?

Ameongeza kwamba Polisi walitakiwa kujiuliza mkutano utazuiaje watu kuhesabiwa? kabla ya kutumia nguvu.vile vile kasema wananchi hatuwezi kuendelea na mambo ya kipumbavu yanayofanywa na serikali hii.

Nawasilisha.
 
Hiyo ndo strength kubwa ya Lipumba. Ukweli na uwazi. Mkutano utazuiaje watu kuhesabiwa? Safi sana Prof.
 
Mauaji ya namna hiyo yashawahi tokea mwezi April mwaka jana huko Afrika kusini

Andries Tatane alishambuliwa na polisi mbele ya kamera na kisha kuuawa kwa kutumia risasi za mpira

Jeshi la polisi liliwafungulia mashtaka askari sita. Kati yao wawili walijibu shitaka la mauaji na wanne shitaka la shambulio
 
Kweli kabisa Prof. Tangia hapo tuliambiwa kuwa shughuli zote zitaendelea kama kawaida wakati wa sensa cha ajabu serikali imekuwa kigeugeu!
 
anguko kubwa la serkali hii ya mheshmiwa,kwanza kura ktk uchaguz kutoka 80 asilimia hadi 60.kujiuzulu kwa mawaziri,kushndwa kwa zoezi la sensa,kushuka kwa kiwango cha elimu wasojua kusoma kuingia kidato cha kwanza nk
 
2015 sio mbal. Serikali ya CCM ndio mwisho. Mungu awalaani 'all Killer cops'
 
ANNEL TEN – IRINGA




Mwenyekiti Wa Cuf Taifa Prof Ibrahim Lipumba-Wa Pili Kushoto akisoma
Tamko,kulia kwake ni Mh Kambaya, kushoto kwake ni Mh Mketo na Mh
Chalamila.

CUF – Chama cha Wananchi tunalaani mauaji ya mwandishi wa Habari wa Channel Ten kituo cha Mkoa wa Iringa yaliyofanywa na jeshi la Polisi, ambaye pia alikuwa ni Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoani humo (IPC) Daud Mwangosi aliyeuwawa kwa kupigwa na bomu (kama inavyosemekana) katika vurugu za kisiasa baina ya Jeshi la Polisi na Wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) juzi Jumapili, Septemba 2, 2012 katika kijiji cha Nyololo, wilayani Mufindi mkoani Iringa.

Kwa mujibu wa taarifa zinazotatanisha zilizotolewa na Vyombo vya Habari pamoja na kunukuu taarifa za jeshi la Polisi, kuwa Mwandishi huyo aliuwawa kwa mlipuko akiwa mikononi mwa jeshi hilo la Polisi hadi kupelekea hata Askari Polisi waliokuwa karibu yake kujeruhiwa na mwengine kukimbizwa Hospitali. Taarifa hizo zinazotatanisha zinasema kwamba Mwandishi huyo alikimbilia kwa jeshi la Polisi kama kujisalimisha hadi kufikia kukumbatiana na OCS aliyekuwepo katika eneo hilo la tukio hili ni kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi, lakini wakati huohuo vyombo hivyo hivyo vya Habari vinaripoti kuwa Marehemu alikwenda kumtetea mwandishi mwenzake wa vyombo vya IPP Media na Polisi huyo OCS alikuwa akimuhami marehemu asiendelee kupata kipigo kutoka kwa askari wenzake kwani alikuwa akimfahamu, ndipo hapo alipopigwa na mlipuko huo na kutawanya matumbo yake nje.

Tukio kama hili la mauaji kwa raia katika vurugu za kisiasa baina ya wafuasi wa CHADEMA na Jeshi la Polisi si la kwanza, ukiacha lile lililotokea siku za nyuma kule Arusha lililopelekea watu watatu kuuawa, tukio jengine la kusikitisha ni lile lililotokea Agosti 27, Jumatatu ya wiki iliyopita mjini Morogoro ambapo mtu mmoja alietambulika kwa jina la Ali Nzona (Muuza magazeti) alieuwawa katika vurugu kama hizo, ambapo taarifa zake zinautata wakati ambapo CHADEMA wakidai ameuwawa kwa risasi, taarifa ya Jeshi la Polisi inasema ameuwawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani. Inasemekana kuwa chanzo cha vurugu zote hizi za Morogoro na Iringa, ni kwa sababu Chama cha Demokrasia na Maendeleo kimekaidi amri ya Jeshi la Polisi kutokukusanyika ama kufanya maandamano katika kipindi hiki cha zoezi la uandikishaji sensa likiendelea hadi hapo litakapomalizika ambapo awali lilipangwa limemalizike Septemba 1, na baadae kuongezwa siku hadi Septemba 8, awali katika makubalino ya CHADEMA na Jeshi la Polisi kabla ya mkutano huo ni kwamba walitakiwa waendelee na mikutano yao.

Kwa mtazamo huu CUF – Chama cha Wananchi tunaona wanaopaswa kubeba lawama hili ni jeshi la Polisi na wala si CHADEMA, kwani kama tulivyoeleza awali ilitosha kuheshimu makubaliano yaliyokuwa yamefanyika baina yao, hata kama kulitokea vurugu haikuhitajika kutumika nguvu kubwa kiasi hiki. CUF pamoja na kulaani mauaji hayo yanaendelea kutokea lakini pia tunasikitishwa na kupotea kwa nguvu kazi ya Taifa kwa sababu zinazoweza kuepukika, ili hali kuna uwezekano mkubwa kama busara zingetumika kwa pande zote zinazohusika mauaji kama haya yasingetokea, kwani tunaamini katika vurugu kama hizo zilizotokea hakuna zoezi lolote la sensa lililoendelea kufanyika katika maeneo hayo husika kwa wakati huo.

Kama hivyo ndivyo ilivyo hakukuwa na ulazima wowote wakuzuia watu kukusanyika au kuandamana, kwani wanaokusanyika na kuandamana sio wote, bado kuna watu watakao bakia katika makazi yao ambao wangetosha kutoa taarifa za ndugu na jamaa zao ambao hawapo au hata kuhesabiwa kwa siku zingine kwani zoezi bado linaendelea, na waandikishaji sensa wangeweza kuendelea na majukumu yao bila hofu wala vitisho juu usalama wa maisha yao kutokana na vurugu, kama ambavyo ilivyotokea.

CUF – Kwa kipindi kirefu tumekuwa tukilililalamikia jeshi la Polisi kuwa liache kufanya kazi kwa ukada bali lizingatie maadili yake ya kazi ambayo ni kulinda usalama wa raia na mali zake, matukio kama haya ya jeshi la Polisi yalianza ndani ya chama chetu, ambapo itakumbukwa mauaji ya kimbari yaliyofanywa na jeshi hilo Januari 26 na 27 mwaka 2001 wakati tulipokuwa tukidai Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, Tume Huru ya Uchaguzi na kurudiwa kwa Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar wa mwaka 2000.

CUF Tunamuomba Rais Jakaya Mrisho Kikwete kuunda Tume Huru itakayoshirikisha Watetezi wa Haki za Binadamu, Madaktari, Wakuu Jeshi la Polisi na Upelelezi na Wajumbe wengine kutoka vyama vya siasa ili kuchunguza mauaji haya yenye taarifa za kutatanisha, ili kuupata ukweli utakaofanyiwa kazi ya kukomesha mauaji kama haya yasiendelee kutokea, ambayo tunahisi yataendelea kutokea kama hatua madhubuti hazikuchukuliwa.



Prof. Ibrahim H. Lipumba
MWENYEKITI

 
anguko kubwa la serkali hii ya mheshmiwa,kwanza kura ktk uchaguz kutoka 80 asilimia hadi 60.kujiuzulu kwa mawaziri,kushndwa kwa zoezi la sensa,kushuka kwa kiwango cha elimu wasojua kusoma kuingia kidato cha kwanza nk

migomo kila kukicha,utekaji na utesaji.
 
4/09/2012

CUF – Chama cha Wananchi tunalaani mauaji ya mwandishi wa Habari wa Channel Ten kituo cha Mkoa wa Iringa yaliyofanywa na jeshi la Polisi, ambaye pia alikuwa ni Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoani humo (IPC) Daud Mwangosi aliyeuwawa kwa kupigwa na bomu (kama inavyosemekana) katika vurugu za kisiasa baina ya Jeshi la Polisi na Wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) juzi Jumapili, Septemba 2, 2012 katika kijiji cha Nyololo, wilayani Mufindi mkoani Iringa.

Kwa mujibu wa taarifa zinazotatanisha zilizotolewa na Vyombo vya Habari pamoja na kunukuu taarifa za jeshi la Polisi, kuwa Mwandishi huyo aliuwawa kwa mlipuko akiwa mikononi mwa jeshi hilo la Polisi hadi kupelekea hata Askari Polisi waliokuwa karibu yake kujeruhiwa na mwengine kukimbizwa Hospitali. Taarifa hizo zinazotatanisha zinasema kwamba Mwandishi huyo alikimbilia kwa jeshi la Polisi kama kujisalimisha hadi kufikia kukumbatiana na OCS aliyekuwepo katika eneo hilo la tukio hili ni kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi, lakini wakati huohuo vyombo hivyo hivyo vya Habari vinaripoti kuwa Marehemu alikwenda kumtetea mwandishi mwenzake wa vyombo vya IPP Media na Polisi huyo OCS alikuwa akimuhami marehemu asiendelee kupata kipigo kutoka kwa askari wenzake kwani alikuwa akimfahamu, ndipo hapo alipopigwa na mlipuko huo na kutawanya matumbo yake nje.

Tukio kama hili la mauaji kwa raia katika vurugu za kisiasa baina ya wafuasi wa CHADEMA na Jeshi la Polisi si la kwanza, ukiacha lile lililotokea siku za nyuma kule Arusha lililopelekea watu watatu kuuawa, tukio jengine la kusikitisha ni lile lililotokea Agosti 27, Jumatatu ya wiki iliyopita mjini Morogoro ambapo mtu mmoja alietambulika kwa jina la Ali Nzona (Muuza magazeti) alieuwawa katika vurugu kama hizo, ambapo taarifa zake zinautata wakati ambapo CHADEMA wakidai ameuwawa kwa risasi, taarifa ya Jeshi la Polisi inasema ameuwawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani. Inasemekana kuwa chanzo cha vurugu zote hizi za Morogoro na Iringa, ni kwa sababu Chama cha Demokrasia na Maendeleo kimekaidi amri ya Jeshi la Polisi kutokukusanyika ama kufanya maandamano katika kipindi hiki cha zoezi la uandikishaji sensa likiendelea hadi hapo litakapomalizika ambapo awali lilipangwa limemalizike Septemba 1, na baadae kuongezwa siku hadi Septemba 8, awali katika makubalino ya CHADEMA na Jeshi la Polisi kabla ya mkutano huo ni kwamba walitakiwa waendelee na mikutano yao.

Kwa mtazamo huu CUF – Chama cha Wananchi tunaona wanaopaswa kubeba lawama hili ni jeshi la Polisi na wala si CHADEMA, kwani kama tulivyoeleza awali ilitosha kuheshimu makubaliano yaliyokuwa yamefanyika baina yao, hata kama kulitokea vurugu haikuhitajika kutumika nguvu kubwa kiasi hiki. CUF pamoja na kulaani mauaji hayo yanaendelea kutokea lakini pia tunasikitishwa na kupotea kwa nguvu kazi ya Taifa kwa sababu zinazoweza kuepukika, ili hali kuna uwezekano mkubwa kama busara zingetumika kwa pande zote zinazohusika mauaji kama haya yasingetokea, kwani tunaamini katika vurugu kama hizo zilizotokea hakuna zoezi lolote la sensa lililoendelea kufanyika katika maeneo hayo husika kwa wakati huo.

Kama hivyo ndivyo ilivyo hakukuwa na ulazima wowote wakuzuia watu kukusanyika au kuandamana, kwani wanaokusanyika na kuandamana sio wote, bado kuna watu watakao bakia katika makazi yao ambao wangetosha kutoa taarifa za ndugu na jamaa zao ambao hawapo au hata kuhesabiwa kwa siku zingine kwani zoezi bado linaendelea, na waandikishaji sensa wangeweza kuendelea na majukumu yao bila hofu wala vitisho juu usalama wa maisha yao kutokana na vurugu, kama ambavyo ilivyotokea.

CUF – Kwa kipindi kirefu tumekuwa tukilililalamikia jeshi la Polisi kuwa liache kufanya kazi kwa ukada bali lizingatie maadili yake ya kazi ambayo ni kulinda usalama wa raia na mali zake, matukio kama haya ya jeshi la Polisi yalianza ndani ya chama chetu, ambapo itakumbukwa mauaji ya kimbari yaliyofanywa na jeshi hilo Januari 26 na 27 mwaka 2001 wakati tulipokuwa tukidai Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, Tume Huru ya Uchaguzi na kurudiwa kwa Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar wa mwaka 2000.

CUF Tunamuomba Rais Jakaya Mrisho Kikwete kuunda Tume Huru itakayoshirikisha Watetezi wa Haki za Binadamu, Madaktari, Wakuu Jeshi la Polisi na Upelelezi na Wajumbe wengine kutoka vyama vya siasa ili kuchunguza mauaji haya yenye taarifa za kutatanisha, ili kuupata ukweli utakaofanyiwa kazi ya kukomesha mauaji kama haya yasiendelee kutokea, ambayo tunahisi yataendelea kutokea kama hatua madhubuti hazikuchukuliwa.

Prof. Ibrahim H. Lipumba
MWENYEKITI

 
Bravo Prof Lipumba. No one is safe these days mikononi mwa polisi. Juzi kijana wa Msamvu, jana mwandishi..who knows who is next? We all need to protect ourselves from the state and its brutal organs!
 
Bravo Prof Lipumba. No one is safe these days mikononi mwa polisi. Juzi kijana wa Msamvu, jana mwandishi..who knows who is next? We all need to protect ourselves from the state and its brutal organs!


hakyanani hili li serikali ni la kuondoa madarakani hata kabla ya muda. kama wao hawafuati sheria za nchi, wanaua watu kwa matashi yao, kwa nini na sie wananchi tusiwaondoe kwa matashi yetu????????????? sidhani kama kuna haja ya kusubiri mpaka 2015, wananchi tujipangeni tuwang'oe madarakani hawa WAUAJI. hawana tena sifa ya serikali ambayo pamoja na mambo mengine ni kuwahakikishia usalama raia wake.




Tuendeleeni kuwaelimisha wananchi, waelimike ili waling'oe madarakan hili li serikali la ccm MAONGO/MAJAMBAZI/MAFISADI/WAUAJI.
 
Ah!ah!kwenye matukio hukutana watu wengi......na cuf wameibuka leo safi sana lipumba
 
wa Habari wa Channel Ten kituo cha Mkoa wa Iringa yaliyofanywa na jeshi la Polisi, ambaye pia alikuwa ni Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoani humo (IPC) Daud Mwangosi aliyeuwawa kwa kupigwa na bomu (kama inavyosemekana) katika vurugu za kisiasa baina ya Jeshi la Polisi na Wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) juzi Jumapili, Septemba 2, 2012 katika kijiji cha Nyololo, wilayani Mufindi mkoani Iringa.

Kwa mujibu wa taarifa zinazotatanisha zilizotolewa na Vyombo vya Habari pamoja na kunukuu taarifa za jeshi la Polisi, kuwa Mwandishi huyo aliuwawa kwa mlipuko akiwa mikononi mwa jeshi hilo la Polisi hadi kupelekea hata Askari Polisi waliokuwa karibu yake kujeruhiwa na mwengine kukimbizwa Hospitali. Taarifa hizo zinazotatanisha zinasema kwamba Mwandishi huyo alikimbilia kwa jeshi la Polisi kama kujisalimisha hadi kufikia kukumbatiana na OCS aliyekuwepo katika eneo hilo la tukio hili ni kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi, lakini wakati huohuo vyombo hivyo hivyo vya Habari vinaripoti kuwa Marehemu alikwenda kumtetea mwandishi mwenzake wa vyombo vya IPP Media na Polisi huyo OCS alikuwa akimuhami marehemu asiendelee kupata kipigo kutoka kwa askari wenzake kwani alikuwa akimfahamu, ndipo hapo alipopigwa na mlipuko huo na kutawanya matumbo yake nje.

Tukio kama hili la mauaji kwa raia katika vurugu za kisiasa baina ya wafuasi wa CHADEMA na Jeshi la Polisi si la kwanza, ukiacha lile lililotokea siku za nyuma kule Arusha lililopelekea watu watatu kuuawa, tukio jengine la kusikitisha ni lile lililotokea Agosti 27, Jumatatu ya wiki iliyopita mjini Morogoro ambapo mtu mmoja alietambulika kwa jina la Ali Nzona (Muuza magazeti) alieuwawa katika vurugu kama hizo, ambapo taarifa zake zinautata wakati ambapo CHADEMA wakidai ameuwawa kwa risasi, taarifa ya Jeshi la Polisi inasema ameuwawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani. Inasemekana kuwa chanzo cha vurugu zote hizi za Morogoro na Iringa, ni kwa sababu Chama cha Demokrasia na Maendeleo kimekaidi amri ya Jeshi la Polisi kutokukusanyika ama kufanya maandamano katika kipindi hiki cha zoezi la uandikishaji sensa likiendelea hadi hapo litakapomalizika ambapo awali lilipangwa limemalizike Septemba 1, na baadae kuongezwa siku hadi Septemba 8, awali katika makubalino ya CHADEMA na Jeshi la Polisi kabla ya mkutano huo ni kwamba walitakiwa waendelee na mikutano yao.

Kwa mtazamo huu CUF – Chama cha Wananchi tunaona wanaopaswa kubeba lawama hili ni jeshi la Polisi na wala si CHADEMA, kwani kama tulivyoeleza awali ilitosha kuheshimu makubaliano yaliyokuwa yamefanyika baina yao, hata kama kulitokea vurugu haikuhitajika kutumika nguvu kubwa kiasi hiki. CUF pamoja na kulaani mauaji hayo yanaendelea kutokea lakini pia tunasikitishwa na kupotea kwa nguvu kazi ya Taifa kwa sababu zinazoweza kuepukika, ili hali kuna uwezekano mkubwa kama busara zingetumika kwa pande zote zinazohusika mauaji kama haya yasingetokea, kwani tunaamini katika vurugu kama hizo zilizotokea hakuna zoezi lolote la sensa lililoendelea kufanyika katika maeneo hayo husika kwa wakati huo.

Kama hivyo ndivyo ilivyo hakukuwa na ulazima wowote wakuzuia watu kukusanyika au kuandamana, kwani wanaokusanyika na kuandamana sio wote, bado kuna watu watakao bakia katika makazi yao ambao wangetosha kutoa taarifa za ndugu na jamaa zao ambao hawapo au hata kuhesabiwa kwa siku zingine kwani zoezi bado linaendelea, na waandikishaji sensa wangeweza kuendelea na majukumu yao bila hofu wala vitisho juu usalama wa maisha yao kutokana na vurugu, kama ambavyo ilivyotokea.

CUF – Kwa kipindi kirefu tumekuwa tukilililalamikia jeshi la Polisi kuwa liache kufanya kazi kwa ukada bali lizingatie maadili yake ya kazi ambayo ni kulinda usalama wa raia na mali zake, matukio kama haya ya jeshi la Polisi yalianza ndani ya chama chetu, ambapo itakumbukwa mauaji ya kimbari yaliyofanywa na jeshi hilo Januari 26 na 27 mwaka 2001 wakati tulipokuwa tukidai Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, Tume Huru ya Uchaguzi na kurudiwa kwa Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar wa mwaka 2000.

CUF Tunamuomba Rais Jakaya Mrisho Kikwete kuunda Tume Huru itakayoshirikisha Watetezi wa Haki za Binadamu, Madaktari, Wakuu Jeshi la Polisi na Upelelezi na Wajumbe wengine kutoka vyama vya siasa ili kuchunguza mauaji haya yenye taarifa za kutatanisha, ili kuupata ukweli utakaofanyiwa kazi ya kukomesha mauaji kama haya yasiendelee kutokea, ambayo tunahisi yataendelea kutokea kama hatua madhubuti hazikuchukuliwa.

Prof. Ibrahim H. Lipumba
MWENYEKITI[/SIZE][/FONT][/COLOR]
[/LEFT][/QUOTE]
 
lipumba nimekupenda kwa kuwa wazi. wewe ni mtanzania na kiongozi wa kuigwa. kwa bahati mbaya serikali haitaki kukutumia kwa sababu za kisiasa lakini nje ya nchi wanakufagilia. tunataka katiba mpya ambayo utaruhusu kila mtu mwenye tarent kutumika kaitika kuleta maendeleo. hivi kikwete kumtumia lipumba unaona nini ? atakusaidia kwani yeye ni mtaalamu sana zaidi ya hao wataalamu waliopo sedrikalini kazi kuiba pesa tu
 
Nilikua sipendi siasa lakini haya mauaji ya watu wasio na hatia yanayofanywa na serikali dhalimu ya chama cha mapinduzi yananivutia kuanza Anti-CCM compaign hadi waniue na mimi. RIP Kamanda...wao wamekuua ila mali za nchi hii wanazozitafuna zitawanenepesha firigisi walizo nazo
 
naona wamesikia maoni ya mwanajf mmoja aliyehoji kwa nini cuf hawajatoa tamko?
 
Back
Top Bottom