CUF yataka serikali tatu



Hapo kwnye red ndio kwenye mtego wa Wazenji kwa Tanganyiaka ili wapate sababu ya kuuvunja muunagano kabisa.
 
Tusubiri hapo Mkoa wa Mjini magharibi na kask. Pemba ndo penye shughuli na population kubwa.
 
Hapo kwnye red ndio kwenye mtego wa Wazenji kwa Tanganyiaka ili wapate sababu ya kuuvunja muunagano kabisa.
Hapana, hesabu zao ni kuwa Tanganyika ikirudi watakuwa na mambo yao na yale yanayowashinda watayaleta katika muungano. Hawana sababu ya kukataa muungano kama wanataka.

Ukitaka kujua hilo, hakuna hata mmoja anayesema vunja muungano. Wanajua wazi kuwa;
-Asilimia 7 ya pato la taifa wanalopata bure halitakuwepo.
-Wanajua kuwa soko lao la biashara na ajira ni Tanganyika wala si Kenya, Uganda n.k.
-Wanajua kuwa ukaribu wao na Zambia, Malawi, Rwanda n.k ni kwa vile wapo ndani ya Tanzania
-Wanajua kuwa mzigo wa elimu ya juu utakuwa wao
-Wanajua kuwa bajeti ya ulinzi na usalama itakuwa yao
-Wanajua ugumu wa kuwekeza kama si Watanzania
-Wanajua tatizo la ardhi leo na siku zijazo linalowakabili

Na kwa kukuthibitishia hili, hata siku moja hutasikia wakidai Passport zao kwasababu wanajua uwepo wa Passport ni kikwazo kwao. Ndiyo maana wanahangaika kutafuta njia za kubaki wakiwa wamejibanza kwa Watanganyika
- Mara wanataka uhusiano maalumu, ukiwauliza wa nini na kwanini isiwe SADC hawana jibu
- Wanataka uhusiano wa EU, ukiwauliza kwanini isiwe EAC hawana jibu
-Wanataka mkataba, ukiwauliza wa mambo gani, hawana jibu
-Sasa wamekuja na kiroja cha mwanasheria wa BLW kuwa tuwe na ushirikiano wa Swiss! kwi kwi! mwanasheria!!

Wao wanachotakiwa ni kupaza sauti katika tume kama walivyokuwa wanapaza katika mikutano ya UAMSHO.
Wasidai Tanganyika wadai ZNZ kwasababu wakiipata ZNZ ya neema automatically Tanganyika itakuwepo

LET THEM GO, LET ZNZ GO ASAP!
 

Nguruvi3,

..nimefanya ka-research kadogo kuhusu "muungano wa Swiss." kwa kweli sielewi Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar alikuwa anataka kusema nini alipopendekeza muungano wetu uwe kama wa Swiss.

..ni vigumu sana kuelewa wa-Znz wanataka mashirikiano yao na Tanganyika yawe ya namna gani, kwasababu kila kukicha linaibuka jambo jipya.

..naomba wataalamu na wadadisi mtuhabarishe kuhusu "muungano wa Swiss" ili tuweze kujua uzuri na ubovu wa mapendekezo ya mwanasheria mkuu wa ZNZ.
 
Joka kuu, ndio maana kila nikimtaja naweka kwiki za kicheko. Nadhani mimi kama wewe kuna kitu hatukielewi.
Ni jambo jema tukawaalika wanajamvi wote watusaidie. Hapa jamvini kahawa ilizunguka lolote linazungumzwa.
Hapa kwenye busati nimewaona hawa wafuatao wakiwa na kashata, na waje basi 'tuhangaike nao'

Wote kwa pamoja Wakuu;
Nonda, Takashi,Baru baru, Mwiba,Mkataba, Abdulsahaf,Toical, Jasusi, Ngongo, Jmushi1, Mzee Mwanakijiji, Mkandara, Kichuguu, sweke34, Pasco, Ben saanane, miss Judith, Mshikachuma,Ngambo ngali, Kimbunga, Nyani Ngabu, Ritz, Ogah, Mwita Maranya,chama nk
 

Nguruvi3,

..ingependeza kama AG wa Zanzibar na wenzake wangeweka details katika mapendekezo wanayotoa.

..naona kila mara wanakuja na jipya. hata suala la "muungano wa mkataba" mtu wa kwanza kumsikia akipendekeza ni huyu AG wa Zanzibar. sasa labda wangekwenda mbali na kuwaeleza wananchi ni nini kitakuwepo ktk huo "mkataba."

..nadhani hawa Zanzibari elites wanawadanganya walalahoi wa mitaani. hawawaelezi ukweli kwamba basically madaraka waliyonayo Zanzibar/SMZ ni very close to the maximum u can get in any form of union/federation/confederation.
 
Wala hakuna doubt na elites wanavyowadanganya walalahoi. Utasikia mtu anasema mkataba, muulize uweje hana jibu. Fikiria hapa tumewauliza akina Baru baru, Nonda, Takashi n.k. hakuna anayekuja na kitu 'tangible'
Ahmed Rajabu kila siku anazunguka mbuyu, mara EU, mara Mkataba na matokeo yake sasa AG ameibuka na kituko kutoka Geneva. Ipo siku tutasikia muungano kama wa California na New York (mungu saidia na epusha njozi hizi batili).

Naunga mkono hoja yako kuwa sasa ni wakati WZNZ waweke details na specifics wanataka nini hasa.
Hivi utaongleaje mkataba kama huna japo 'frame work' yake
Hivi utaongeleaje serikali 3 kama hujui zita operate vipi!

Hapa WZN wana mawili
1. Sema muungano basi, tuvunje jahazi na Tanganyika ichukue mbao zake, ZNZ irudishe sarafu na passport
2. Sema YES muungano, weka details una propose nini

Nilisoma makala ya Zitto, japo sikubaliani naye katika baadhi ya hoja lakini nakubaliana naye kuwa alikuwa na details na specifics za muungano uweje.

Sikubaliani na AG wa Unguja kwasababu anabwaga neno swiss kama dumu la maji lisilo na mwanzo au mwisho
Sikubaliani na Ahmed Rajabu kwasababu hajawahi kutoa details za anachokihubiri zaidi ya kusema ZNZ itakuwa kama Dubai, watu watagawiwa pilau kila siku, makaimati yatagawanywa na mashekha kila asubuhi na uwezekano wa bomba la maziwa na asali kutoka Oman upo kama wznz watakuwa kitu kimoja!
 
Mkuu unajua wasema maneno mazito sana hapa.. Sasa inakuwaje tume hiyoo inakusanya maoni ya wananchi wao wanakuja na kusema tuunde serikali tatu, mara tuunde jumuiya kama ya Ulaya ya nini yote haya wakati jibu ni moja tu.. Wazanzibar hatuutaki Muungano - kwisha!. Vunja muungano - Toeni wote jibu moja tu sio kuitaka katiba iwe hivi ama vile wakati katiba hutengenezwa baada ya nchi kuwa huru. Hamuutaki muungano hii katiba mpya ya nini kwenu?..Kadhi kaingia mjini mnaitaka talaka humuitaki?.. semeni!
 

Bw Mkubwa,

Mimi binafsi sio mwanasiasa na wala sio mwana sheria...Mimi ni civil engineer by profession , Masuala ya Zanzibar na Muungano yananiuma kama raia mwengine wowote yule. Kutokua mwansiasa au mwanasheria haina maana kama mimi ni mjinga...Naelewa kinachoendelea , ila kazi hiyo ya uchambuzi wa siasa na sheria tunawaachia wenye taaluma hiyo.

Mimi (sisi) tanataka Zanzibar huru kama iliyokua kabla ya Muungano. Jinsi gani tutafika huko hiyo ni kazi ya wanasiasa na sheria kutuelekeza. Hao hao wanasisa na wanasheria wanapotaka kujenga nyumba zao hutufuata sisi, sio kama wao ni wajinga bali hiyo sio taaluma yao.
 
100% nakubaliana nao serikali 3 ndo muhimu zaidi
 
..pia wa-ZNZ waelewe kwamba "UHURU" wanaoutaka hautapatikana hata ktk "muungano wa mkataba" unaofanana na EU.
Mkuu,

Huo "Muungano wa Mkataba" which is actually ridiculous kwa sababu hata huu wa sasa pia ulikuwa wa mkataba (na ningeomba Maalim Seif asikie kwamba idea yake ni funny maana yeye ndie mmoja wa walio u popularize huo msemo wa "Muungano wa Mkataba") anyhow, huo "Muungano wa Mkataba" mimi sina tatizo nao saaana so long as kila mmoja ana nchi yake yenye serikali yake na hakuna kusogelea wala kunusa serikali ya mwenzio, sitaki kusikia sijui Mbunge wa Zanzibar yuko Dodoma, sijui Makamu wa Rais atoke Zanzibar, sijui kiongozi wa Zanzibar anakuja Bara kuzindua sijui mradi, au Waziri Mzanzibar, nothing, kila upande kivyake!
 

Tuaiga tunasaidiwa ushauri sio vibaya ,ila hao wanaosaidiwa bado katika nchi zao hakuna msimamo,bado demokrasia ni ndoto,uendeshaji wa nchi ni wa kitabaka kwa maana maendeleo hayaonekani kwa kila mwananchi ,wananchi wasio na kazi hawalipwi ila mwananchi huyo asie na kazi na halipwi bado analipa kodi ,Zanzibar ina mipango ya kuwalipa wananchi wasio na kazi,mambo yao yatakapokuwa mazuri.

Mnakubali mambo mengine mnakataa mengine,hivi huoni kama hapo hapana nia ya dhati na zaidi nchi zetu hizi haziaminiki kabisa ,kisiasa na kiutawala anytime kunavurugika kila mtu na mbao zake hakuna kugawana ,kilichoko kwako ndio chako na ubabe wa siku hizi kurudishiwa inaweza kuchukua karne nzima,na haohao washauri ndio haohao watakaoanzisha uhuni.Pindi wakiona tunaelekea ,uhuru wowote wanaoutaka Zanzibar ni bora waachiwe wapumue ,kwani ndio utakuwa mwisho wa dunia ,mtoto akilia wembe tunasema mpe ,WaZaznibari wachukue nchi yao wajipange watakavyo.
 

Nafikiri hapa tulipo huo ukweli haukwepeki. Kelele zimezidi sana sasa
 
Mbona hizi habari hatuzisikii kutoka upande wa tanganyika ,Za zanzibar zinatangazwa kama mpira ama kweli zumari ikipulizwa Zanzibar walio maziwa makuu huhemkwa !

Watanganyika wanamuogopa hayati nyerere, yani hadi leo wanaendeleza mawazo yanyerere kama vile wao hawana mawazo.
 
Mimi ni mtanganyika, kwa hili nawaunga mkono wazanzabari, wana akili na maono ya mbali. Sie bara huku mtu anasema kwa sababu baba alisema serikali mbili basi na mimi nataka serikali mbili.
 
Wakuu,
Kwa hali ilivyo serikali 3 haiwezekani. Hebu tuelezeni hiyo ya muungano itakuwa na kazi zipi ambazo hazitaingiliana na serikali za nchi husika. Mfano, ZNZ wanasema wanataka kuwa na maamuzi kuhusu mambo ya nje, sasa hapa Rais wa muungano atakuwa na kazi gani. Pili, hiyo serikali ya muungano itaendeshwaje ili hali kuna anayetoa 10 na mwingine 0 ili tuwe na 10.

Mkataba hauwezekani, Mtanganyika atataka kujua kila kipengele cha mkataba atafaidika na nini hasa.
Kwasasa hakuna chochote wala lolote ambalo Mtanganyika anaweza kusema kutoweka kwa ZNZ katika muungano kutamuathiri. Hakuna na kama kipo kipengele kimoja tu weka jamvini.

Serikali 2 haiwezekani kwasababu kuna kutoaminiana na mmoja kuwa mtoaji mwingine kuwa mpokeaji.

Mahusiano maalumu haiwezekani kwasababu tutakuwa tunaua spirit ya EAC, SADC nk. Kama kuna anayejua mahusiano yapi tuwe nayo, weka hapa jamvini.

Mwisho, ubaguzi na matusi ya ZNZ sasa yamewachosha Watanganyika, ndiyo maana wamekaa kimya ili ZNZ waende zao.

LET ZNZ GO is the only solution
 
Sisi bara hatutaki muungano. Nendeni zenu na serikali yenu.
 
nani kasema?
Wananchi wengi ni % ngapi?
Serikali tatu? Pesa zipo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…