Hivi karibuni kumekuwa na taarifa za uongo na propaganda zinazoenezwa na Hamadi Rashid kwenye vyombo vya habari kwamba zaidi ya wanachama 1000 wa CUF wa mikoa ya Dar es Salaam na maeneo mengine wamerudisha kadi na kumkabidhi Hamad Rashid.
CUF imefuatilia na kubaini habari hizi ni za uongo na chama kimebaini kwamba kadi anazoonesha kwa waandishi wa habari si za wanachama bali ni za kutengenezwa ambazo aliziandaa wakati wa Kura za maoni za kuwapata wagombea wa Ubunge na uwakilishi kwa uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 na Chama kuzuia uingizaji wa wanachama wapya muda mfupi kabla ya kura za maoni.
Kwa wakati huo Hamadi alikuwa ameandaa Kadi mpya 7000 ziweze kumsaidia katika kinyang'anyiro hicho, hivyo basi hakuna wanachama 1000 waliompelekea kadi kwani wanaCUF wako ngangari na chama kipo imara kwa kuwa wanatambua kuwa wao si wanachama wa UHS (United Hamad Suppoters), bali wao wanachama wa The Civic United Front hivyo hawapo kwa maslahi ya mtu binafsi.
Chama cha wanachi CUF kinatoa tahadhari kwa wanachama wake kwamba kumekuwa na zoezi la kununua kadi za wanchama wa CUF na Hamad kwa kutumia watu mbalimbali,Hivyo mwanachama yoyote asikubali kutoa kadi yake kwa namna yoyote na kwa mtu yeyote.
CUF imefuatilia na kubaini habari hizi ni za uongo na chama kimebaini kwamba kadi anazoonesha kwa waandishi wa habari si za wanachama bali ni za kutengenezwa ambazo aliziandaa wakati wa Kura za maoni za kuwapata wagombea wa Ubunge na uwakilishi kwa uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 na Chama kuzuia uingizaji wa wanachama wapya muda mfupi kabla ya kura za maoni.
Kwa wakati huo Hamadi alikuwa ameandaa Kadi mpya 7000 ziweze kumsaidia katika kinyang'anyiro hicho, hivyo basi hakuna wanachama 1000 waliompelekea kadi kwani wanaCUF wako ngangari na chama kipo imara kwa kuwa wanatambua kuwa wao si wanachama wa UHS (United Hamad Suppoters), bali wao wanachama wa The Civic United Front hivyo hawapo kwa maslahi ya mtu binafsi.
Chama cha wanachi CUF kinatoa tahadhari kwa wanachama wake kwamba kumekuwa na zoezi la kununua kadi za wanchama wa CUF na Hamad kwa kutumia watu mbalimbali,Hivyo mwanachama yoyote asikubali kutoa kadi yake kwa namna yoyote na kwa mtu yeyote.
HAKI SAWA KWA WOTE
IMETOLEWA NA AMINA MWIDAU
MKURUGENZI WA HAKI ZA BINADAMU NA UENEZI
IMETOLEWA NA AMINA MWIDAU
MKURUGENZI WA HAKI ZA BINADAMU NA UENEZI