CUF waishambulia CHADEMA


mi naona cuf wanafiki ,mbona wakati wakiwa wapinzani zanzibar walikuwa wanaenda kujaliana na ccm wenyewe waka waacha vyama vingine havikushirikishwa mpaka wamefunga ndoa na ccm kama angekuwa na moyo huo huo kule zanzibar wakati wa majaliano ya muafaka angewaambia ccm,lazima vyama vingine vishirikishwe lakini wameenda wamejadili wenyewe vyama vingine nakumbuka vilipiga kelele lakini wapi mi nafikri cuf sio wapinzani tena wao wapo na ccm kama vyama tawala
 

Kama walishindwa kuungana kabla ya uchaguzi na kusimamisha mgombea mmoja wa kiti ya urais (yaani wakawa wa1 toka huko) ya nini leo muanze propanganda za kiccm eti Chadema wamekosea?? CUF walishapata hiyo nafasi na waijutie kama hawakuitumia vema vinginevo wajipange upya.
Alafu hivi inakujaje akilini kuunda kambi ya upinzani na wapinzani waliokuwa wanampigia kapeni jk, tusiwe watu wa kukurupuka na kuanza kublame na MAADAM CHADEMA HAWAJAVUNJA SHERIA/KANUNI MIMI SIONI TATIZO LOLOTE.
 
CUF yenyewe imeshajifia,2015 ndo kabisa tutaisahau huku bara!
Hamad ajiulize kilichowapata huku bara nini?
Cuf ni wanafiki kabisa,hasa huyu hamad unaongea PRIVATE na Mbowe unakuja kutoa hadharani ili nini?
Hata kama Chadema haitaki kuungana na vya kama TLP(mrema-ccm b),UDP(cheyo- neutral),NCCR(mbatia -CCM b) ni sawa kabisa coz hawa wote ni mamluki/traitor.
Chadema kaaeni na msimamo wenu hata hao CUF achaneni nao kabisaaa...mamluki wala orojo
 
Kuna wakati wa kujadili hoja na kuweka ushabiki wa vyama vyetu pembeni na hii ndo source ya umaskini wa wanasiasa na washabiki wa siasa Tanzania.Hamad Rashid amezungumzia ubaguzi uliofanywa na CHADEMA na wakataka kuwashirikisha CUF,kwakuwa CUF wakakataa imekuwa ishu,wangekubali wana CHADEMA mngeona sawa ila kwa kuwa ombi limekataliwa ni ishu.
Miaka mitano iliyopita Hamad Rashid alikuwa kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni,alishirikisha vyama vyote na akawapa nafasi waunge kutoka vyama vyote,iweje leo CHADEMA wabague wenzao,maslahi ya wananchi yako wapi hapa?hii ni kuweka maslahi ya CHADEMA mbele and this will destroy the party.CHADEMA wana grounds zipi za msingi za kutenga NCCR-Mageuzi,UDP,TLP ukiacha tofauti za kisiasa za baadhi ya wabunge na viongozi wa CHADEMA,tuwe objective na si subjective kwenye yale tunayoyataka kuyatekeleza kwa maslahi ya nchi na si maslahi na sifa za Mwenyekiti wa chama fulani na katibu wake.
 
Hapa tukubali tukatae kuna element za udini, japo kuna deeper issues than this. Nilitegemea kusikia maneno ya busara yangetoka kwa Hamad Rashid, matokeo yake katoa pumba tupu. Totaly immatured!
Ndg yangu,kwanini asitoe pumba wkt amevaa viatu vikubwa sana kupita saizi yake halisi..Ana uwezo wa kuwa kuwa katibu kata na si mbunge wa kariba ya wabungewengi wa huku bara,mtu kachaguliwa na watu elfu tatu,nne mpaka tano wa lingane uelewa na mtu liyechaguliwa na watu elfu 30000,mimi nafikiri anayewajibika kwa watu wengi zaidi anakuwa anakuwa tofauti na hawa wajumbe wa nyumba kumi wa cuf.Hamad Rashid angekuwa anashiriki vikao vya mabaraza ya kata asingepwaya namna hii,Asamehewe.
 

Chadema inabidi wajiepushe na mapandikizi ili wasiweze kuwa-sabotage.
 
Wakuu nazidi kuwaumiza kichwa.. Msiseme nawatakia mabaya Chadema ila ndio ktk kuelemishana.
Ebu nambieni Chadema mwaka huu wamepata viti vingapi toka majimbo 239 maanake sipati hizo asilimia 12 Nakumbuka mwaka 2005 kulikuwa na majimbo 229 au 230 (sina hakika) na CUF walipata wajimbo 19 tu.
 
CUF si wapinzani wa kweli tena, hukushuhudia jinsi Mnyaa alivyojitoa kwenye race ya unaibu spika na kumuunga mkono Ndugai? Jambo ambalo hata katibu wa kambi yao ya upinzani isiyo rasmi Mr Kafulila hakulijua. Alisema wanaendeleza sera yao ya kuunganisha vyama vyao, na ndiyo maana wabunge wa CCM walimpa Ubunge wa SADC kwa kishindo. Nini Tafsiri ya wabunge wa CUF kukalia viti vya wabunge wa CHADEMA mara baada ya wabunge hao kutoka? tena kitendo kilichofanyika ndani ya dakika moja tu, inamaanisha wakati CHADEMA wanapanga kususia hotuba ya JK, CUF walikuwa wanapanga jinsi ya kurithi viti vyao kwa muda ambao wao watatoka, TAFAKARI. NCCR bado wanamachungu ya Mwenyekiti wao kuangushwa na Mgombea wa CHADEMA kule kawe, wanajiandaa kwenda mahakamani kupinga Ushindi wa Mdee, MREMA wakati wa kampeni alisikika waziwazi akimpigia kampeni Kikwete na kumsifia kwamba anastahili kupewa nafasi kuongoza kwa kipindi cha pili, Mr CHEYO alivuliwa uwaziri kivuli na HAMAD kwa kuunga mkono bajeti ya serikali kinyume na makubaliano ya Kambi katika Bajeti ya 2010/2011 je atakuwa na jipyi ndani ya miezi minne tu baada ya kuungana na serikali ya CCM. Kwa facts hizo, acha CHADEMA waunde kambi ya upinzani PEKE YAO kwani ndiyo wapinzani wa kweli waliopo Bungeni.
 
Hivi CUF bado inafadhiliwa na wale waarabu waliomwekea ngumu mwasisi wa chama hicho James Mapalala ati kwamba wasingeendelea kukifadhili hadi waone jina la Mwenyekiti muislamu? Kama huamini hili mtafute Mapalala na baadhi ya waasisi wa chama hicho kwa upande wa bara watakuthibitishia.
CCM na CUF watahukumiwa na wananchi wanaowadharau na kuwasaliti miezi sitini ijayo au siku 1830 zijazo ambazo wao wanajidanganya ziko mbali sana. Kumbe sasa wananchi tumeelewa mabadiliko ya kweli nchi hii yatasimamiwa na CHADEMA tu wengine wote au vibakauchumi au vibaraka.
Mungu ibariki Tanzania.
 

thanks sir umetekeleza wajibu wako
 

wanatuchelewesha na wameifanya tanganyika mgodi na koloni lao itawatokea puani sasa watanganyika wameamka mwanangu!
 
hawa wanaumoja iweje wawe kambi ya upinzani huku bara wanaviti vingapi shiha ni huoulezi
 

mwanangu Mbowe ulienda ushirikiane na cuf gani maana umeenda kuomba mkeka ambao mbuzi kaula hakuna ubishi cuf imesha pasuka mapande manne.,... 1cuf Udini 2cufMageuzi 3cufUpemba 4cufCcm umeipata hiyo kivyao hirtoria itamuandika adui no moja wa TANGANYIKA!
 

mwanangu Mbowe ulienda ushirikiane na cuf gani maana umeenda kuomba mkeka ambao mbuzi kaula hakuna ubishi cuf imesha pasuka mapande manne.,... 1cuf Udini 2cufMageuzi 3cufUpemba 4cufCcm umeipata hiyo kivyao hirtoria itamuandika adui no moja wa TANGANYIKA!
 

pumba hiyo mwanangu roho ya chadema tumeivaa sasa hakuna wa kutubadilisha mpaka kieleweke si muazini wala shehe mtaji upo wasomi vijana waliopigika wafanyakazi we ulie tu ulipewa buku badala ya kununua unga robo ule na wanao umenunua miwani thanks kivyako mwana!
 
Wapenda Mageuzi wa Kweli ndani ya CUF (Kama wapo) Wajiondoe haraka kutoka katika undumilakuwili wa CUF.
 
Tena afadhali CDM hamkuwashirikisha hawa CUF maana hao tayari ni CCM wangetusaidia nini ila kutuharibi mikakati yetu ya kuijenga nchi yetu. Wao wameahidiwa pipi na vyeo bandia! Hamad nilidhani kuwa ni intelligent kumbe a total disgrace!!!
 
CUF wana mimba ya ccm ndo maana wanakataa kila kitu cha chadema. Simnajua mtu mwenye mimba? Ukimpa bigjii anatapika, ukimpa ugali ndo kwanza anaona unajidai kweli ndoa yenu inatisha make hata mwezi bado lakini nyodo kibao!!!!

CUF tunajua kwenye uchaguzi ulio pita mmetumia dini ili kushinda uchaguzi nani asiyejua hayo?
 
Mkandara,
Kweli mkuu wangu nakuelewa sana na najua base ya argument yako lakini umakini unaodhani wanatakiwa kuwa nao Chadema wakishawakaribisha CUF na kuwa nao ili wapate manufaa ya kujua kila wanachopanga wapendwa wao CCm ndio wasi wasi ule ule unaojaribu kuwafanya Chadema wawaogope zaidi CUF.
Najua ni kiasi gani unatamani kuona ushirikiano wa vyama pinzani, lakini pia nafurahi kuona unajua hatari iliyopo katika muungano huo. Nikwambie ukweli ni rahisi kuungana na CUF na NCCR kuliko kuungana na Mrema au Cheyo. Nina hakika kwa NCCR isingekuwa vigumu kwao kuungana nao kama si mgogoro wa mwenyekiti wao na Chama. Hata hivyo tusikate tamaa. Bado kuna nafasi, ambayo wote wakiona umuhimu wa mwenzie watachukua hatua stahiki. Tusiumize vichwa sana. Hiyo ndio politics yenyewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…