CUF: Unafiki wenu ndio anguko lenu

CUF imepotoshwa na Hamad. Hamad karudi ccm kama Mrema na Lamwai walivyofanya, nyie wanachama na washabiki wa cuf sasa mmepotea na sijui kama mtarudi kuwa chama cha siasa tena. Mnacheza na ccm nyie, CDM tunapigana na ccm kila kona na tunajua jinsi gani walivyo na hatari, nyie wa-cuf mliweka too much hope kwa Hamad na amewatosa kwenye mdomo wa mamba. Lipumba siku nyingi anachukua na kulipwa na ccm, poleni na lengo la cuf sasa muanze kuvaa nguo za kijani.

Hivi Zanzibar ni Mkoa au Nchi? Jazeni nyie wenyewe.
 

Hii umepata wapi Bosi wangu?
 
Tatizo si CUF si CCM wala si CHADEMA. Tatizo lenu ni wapenda damu za binaadamu basi.
 


Nafikiri pengine unaongozwa na chuki binafsi. Tangu lini mliwahi kuwa na habari na CUF na kwa kuangalia pengine hiyo CUF haianguki bali inapanda chati. Kwani kbla ya uchaguzi wa 2010 ilishawahi kupata viti ndani ya Tanganyika zaidi ya Kigamboni kwenye Wapemba wengi?
 

Nakubaliana nawe katika mambo mawili lakini hili la matamshi ya Lissu hayana mshiko wowote na ameshajibiwa hoja zake. Kuamuwa kujibu au kukaa kimya hi hiari yake.

Ama mambo mawili ninayokubaliana nawe ni hili la Muungano wa matata na kuhitajika kwa Katiba mpya. Tunahitaji Katiba mpya tatu, ile ya Zanzibar, ya Tanganyika na ya Muungano.
 
Sio kweli kuwa CUF haijajitangaza Bara, mbona ilifanya juhudi kubwa na hata kufikia kupata ubunge Bukoba. Tunasahau kuwa element ya udini ndio iliyowaangusha CUF Bara. Si mlikipa jina kuwa ni Chama cha Kidini? CCM walipiga debe, vyama vya upinzani vikafurahia kwa kuogopa kukosa umaarufu> Kibao kimegeuka na udini umekuwa issue moto na CCM ikaamuwa kuhamishia udini kwa CHADEMA na hivyo CHADEMA kuanza kuona ubaya wa unafiki.
CCM na CHADEMA wasipojihadhari kuna hatari kwa CUF kupata nguvu na ndio maana CUF wametulia wakiangalia vita vya panzi.
 
Ngekewa,

Inawezekana nina chuki binafsi na CUF. Inawezekana kwamba CDM haijawahi kuwa na habari na CUF. Na inawezekana chati ya CUF inapanda, Je hayo yote yanaondoaje unafiki wao wa kwenda kurudia waliyosema CDM (wakati wameshasema kufanya hivyo CDM walikuwa wanahatarisha amani na utulivu?) na hao wananchi wanaoenda kuwashtakia CCM ni wananchi wapi? Walioko Zanzibar au Tanganyika?

Siamini kwamba ni lazima 'vyama vya upinzani' viungane ili kuishinda CCM. Muungano huo utakuwa kama wa Zanzibar na Tanganyika. Au kama kitu kinachoitwa 'marriage of convinience'. Matatizo yake ni makubwa siku zote. Lengo litafikiwa lakini halitadumu. Angalia Kenya. Angalia Zanzibar.

Tafadhali angalia hoja yangu na si chuki unayodhani ninayo. Ukiweza ijibu hoja yangu.
 

Mkuu, nadhani unajua kama Tanzania kuna vyama vingi vya siasa na kila chama kina malengo yake na kila chama kina haki, naona utataka vyama vyote vifuate maelekezo kutoka kwa Chadema? NCCR, TLP, CUF, CHADEMA, wote wanaweza kupita Tanzania nzima wakafanya mikutano yao wananchi ndio wakuamua wamfate nani nadhani huu sio Unafiki kama unavyosema wewe. naona umekuwa indulgence na CUF kuliko CCM, pambana CCM kuwang'oa madarakani
 

Huwezi kuitoa CCm kama vyama vya kidini, kikanda na vinavyoongozwa na watu ambao hata kimaisha ni failure kama CUF,unaijua vizuri historia ya Lipumba from when he was at UDSM alikuwa anapendelea sana watu wa imani fulani hivi, soma kitabu kimoja kinaitwa" myth of mzee punch" kimeandikwa na mmoja wa wahanga wa mgomo wa UD 1990, Maalimu seif alitumia mbinu zake na uwezo wake wa kupndwa pemba kutafuta watu wa kumfuata, I promise you kama sheria ya kusajili chama ingekuwa hairuhusu kuwa na pande zote za Muungano CUF isingekuwepo bara for sure, maana hata udiwani huwa inashinda maeneo ambayao ya wapemba wengi, hata majimbo iliyochukuwa unguja ni pale penye wapemba wengi,Muulize Lwakatare kipi kilimtoa CUF, muulize Tambwe Hiza ,Muulize Professor safari na bwana mdogo mwalimu Mtatiro namsikitikia sana watamtoa tu kwenye reli hicho chama hakina sura ya kitaifa, kama wewe siye wa lile tabaka , Mapalala alitolewa Cuf kwa nini na wote hao ni watu wa dini moja why isiwe Hamad rashid au Lipumba afukuzwe CUF, mustafa wandwi wa msoma mbona hawafukuzwi??
 
CHADEMA KIPO KWA AJILI YA KUUWA WADUDU WANAORUKA NA WANAOTAMBAA, PIA KUMBUKA""TUNAANDAMANA ILI kuwashukuru WANANCHI kwa kura nyingi walizokipa CHADEMA, na kuiwajibisha serikali.NA : "Tunaandamana kushinikiza uwajibikaji wa serikali...wakitekeleza tunayosema, tutaandamana tena kuwapongeza
 
Kuiondoa CCM madarakani ni kuwaondoa CUF madarakani pia huko Zanzibar. Au hilo halionekani?

Hivi leo hii CDM ikienda Zanzibar kufanya mkutano au maandamano wanampinga nani? Huu sio unafiki? Tunawezaje kuongelea CCM bila CUF? Mimi siwezi, labda wapo wanaoweza.
 
nimeona madiwani wa cuf mwanza, nimeona madiwani wa cuf musoma ( mara), nimeona madiwani kagera, kumbe wapemba wengi. hapo kwenye red tufahamishe vizuri wewe chadema-kata
 
unafiki na udini wao ndo uliowaangusha, hadi sasaivi wamebaki pumba tu, mahindi yote yako chadema.
 
chief masanja (mkandamizaji????) nashukuru kwa kuzungumzia jambo hilo kwa undani japo hujaenda ndani sana. its so possible hivyo ndivyo ilivyotokea. karume anaonekana was forced na kwa kutoelewa kwake. kama una zaidi mwaga hapa tafadhali tupate uwanja mpana wa kuchangia
 
Ni kazi kweli kutumikia Mabwana wawili.
Ni kweli CUF wanawachanganya watanzania. Chadema ilipokwenda kuishitaki CCM na serikali yake kwa wananchi, CUF nao alidandia band wagon wakidai kuwa CHADEMA wanahatarisha amani. Sasa nao wameanza hizo ziara ya kuishitaki CCM na serikali yake kwa wananchi, wanapoulizwa kama wenyewe hawahatarishi amani, eti wanadai wenyewe hawahatarishi amani kwa sababu hawafanyi maandano. Huu ni upumbavu mtupu, mfanye maandamano au msifanye lengo ni lile lile kuishitaki CCM na serikali yake kwa wananchi. Kutakuwa na viongozi ambao wataoa hotuba zao, wataeleza ni jinsi gani CCM na serikali yake wana-ignore matatizo ya wananchi.
Chadema wamefanya maandamano ya amani kuanzia Mara hadi Kagera hatukusikia mtu kauawa au kuvunjiwa duka kwa sababu ya hayo maandamano. Kulikuwa na utulivu kwa sababu Taarifa za Kiitelijinsia alikuwa amekwenda kwenye semina na hakuwepo wa kukaimu nafasi yake. Na katika kuhitimisha viongozi wa Chadema walizungumza na wananchi hadharani kama ambavyo CUF inafanya. Na yale ambayo Chadema walizungumzia ndiyo yaleyale CUF wanaenda kuyazungumzia. Sasa tatizo liko wapi?
Tunaelewa kuwa CUF ni sehemu ya serikali inayoongozwa na CCM, na haya matatizo yanawagusa hata wananchi wa Zanzibar. Sasa hatujui huko Zenji wataenda na gia gani, je Hamad atahudhuria au atakuwa na emergence trip overseas.

Shariff Hamad alikuwa mbele kuwasemea wananchi matatizo yao, tangu ameukwaa Umakamu wa Rais basi hawezi kuzungumzia hali halisi ya wananchi. Hata kwenye hizo ziara hawezi hata kuonekana mara moja, anao muda wa kwenda kufungua tamasha UAE lakini hawezi kukutana na wananchi. Au inawezekana tangu Hamad apate Umakamu basi na matatizo ya Zanzibar yamekwisha............dhat iz so swiiti.
 
kweli kabisa ulichokise[****, unafiki wao wananchi wenye nia ya ukombozi halisi wa nchi hii tumeshswaonaOTE=MsandoAlberto;1758931]Nawasalim WanaCUF,

Bila kung'ata wala kumung'unya maneno ninyi ni wanafiki. Wanafiki sana.

Kwa nini nawashutumu? Kwa sababu tabia ya unafiki haijifichi. Hata kama wengine wote hawaioni ila mwenye tabia anajua kwamba anachofanya ni unafiki.

Mnawashutumu CDM kwamba ni kikwazo cha upinzani. Mnasema CDM wanadharau maamuzi ya ya wazanzibari kuhusu serikali ya umoja wa kitaifa.

Mara mnakurupuka na kusema mnaenda kuwashtaki CCM kwa wananchi. Wananchi wapi? Watanzania Bara peke yake au pamoja na Visiwani?

Hayo mnayoenda kuwashtakia kwa wananchi, i.e. Malipo ya dowans, bei za bidhaa, mgawo wa umeme, nk wananchi wanaishi nayo. Wanayajua. Pia CDM wameshawaambia.

Lakini, kama CCM ndio chanzo, ni huku Bara peke yake? CCM wameshindwa Bara peke yake? Visiwani mnamshtaki nani?

Hapa ndipo unafiki unapokuwa wazi. Hakuna asiyeuona unafiki wenu. Visiwani ninyi ni serikali. Matatizo ya wananchi mnatakiwa kuyatatua kama serikali. Hicho ndicho mlichokubaliana na CCM.

Huku Bara ninyi ni upinzani mkishirikiana na TLP, NCCR na UDP. Mnapinga au kukosoa wanayofanya CCM. Mnajidai kutokuona tatizo hapo. Hata kama muungano una matatizo hii nchi bado ni moja. Hatuna serikali tatu.

Tuna serikali mbili. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inawakilishwa kwenye Serikali ya Jamhuri. Kwa hiyo mpo kwenye Serikali.

Je mnataka tuamini mnaenda kujishtaki au hamna uwezo wa kuleta mabadiliko mkiwa ndani ya serikali yenu? Mnataka kuwa serikali na upinzani kwa pamoja?

Huwezi kula keki yako na kubaki nayo; you can not eat your cake and have it.

CUF, you have made a political mistake and error. Rectify it. The train is moving. Acheni kuwa wanafiki. It will push this country further down the abyss.[/QUOTE]
 
chatu dume "nimeona madiwani wa cuf mwanza, nimeona madiwani wa cuf musoma ( mara), nimeona madiwani kagera, kumbe wapemba wengi. hapo kwenye red tufahamishe vizuri wewe chadema-kata"

Njoo mwanza CUF wana diwani mmoja wa kata ya Mirongo ambayo iko kati kati ya jiji la mwanza na mitaa inayounda hiyo kata ni Unguja, rufiji, Uhuru nk, ana angalia wakazi wengi wa mitaa hiyo ni watu gani maana majina tu ya mitaa yanakutambulisha , my brother dont shout as if you have never been to school, CDM alaways huwa hatuongei kama hatuna ushahidi, ni sera na ipo kwenye katiba ya CDM, tofauti na nyinyi CCM,CCMb ambao Umakamba na Umatatiro umewajaa ( uropokaji na ukurupukaji)
 
Chadema ni chama cha kanisa tu muna wasi wasi na ccm kuweka raisi muislamu ndio hasira zote muna ona maslahi ya kanisa yanahatarishwa.
kwani kuna ushahidi majimbo mengine mulishirikiana na ccm kuchakachuwa matokeo ili cuf isishinde
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…