"CUF ni CCM- B". - Kampeni ya CHADEMA Igunga na uchaguzi mkuu 2015

Zawadi Ngoda

JF-Expert Member
Aug 13, 2009
3,796
1,849
Mgombea wa ubunge kwa tiketi ya CHADEMA Igunga alitumia dakika 20 katika moja ya kampeni zake nilizohudhuria kueleza kuwa CUF ni CCM-B. Kwa muda wote huo nilikuwa nasubiri kusikia jinsi atavyotatua matatizo ya wanaigunga (maji, kilimo, elimu n.k) pale akichaguliwa kuwa mbunge. Kwa bahati mbaya uvumilivu wangu ulikwisha baada ya dakika 20, kwani alikuwa ameganda kwenye topic moja "CUF ni CCM-B". Ukweli niliondoka kimya kimya, sijui kama baadae alizungumzia matatizo yanayowakabili wananchi wa Igunga na ufumbuzi wake. sidhani!

Alipokuja Tindu Lisu (mbunge-CHADEMA) Katika kampeni hizo nilikuwa na hamu sana ya kumsikiliza kwani nimemsoma katika magazeti tu. Huyu alitumia dakika 30 kueleza kuwa CUF ni CCM-B. Ilipofikia dakika ya 30 niliondoka kistaarabu bila kumwabia yeyote yule hata rafiki yangu niliyekuja naye pale.

Katika uchaguzi mkuu 2015, eti hiyo ndio 'KARATA DUME' wanayoitegemea kuieleza Tanzania nzima. Inawezekanaje kuingia IKULU kwa kuwaeleza wananchi milioni 30 kuwa CUF ni CCM- B.

Wananchi wanataka kujua ni jinsi gani CHADEMA MNA dawa ya kuondoa matatizo yao yanayowakabili kila siku? Umasikini, elimu, matibabu, miundo mbinu, kilimo duni njaa n.k

Kwa mtindo wa kampeni hizo ninahakikisha kuwa Tanzania hatuna vyama vya upinzani, na hasa CHADEMA ndio bure kabisa. Najuta kwenda kwenye kampeni zao, huwezi kujifunza lolote lile.
 
Usichague chama wewe chagua "mgombea" kwa uwezo wake..

Mimi nimeshaacha mambo ya chama naangalia "uwezo wa mgombea" period

Vyama vyote na kelele tu
 
Usichague chama wewe chagua "mgombea" kwa uwezo wake..

Mimi nimeshaacha mambo ya chama naangalia "uwezo wa mgombea" period

Vyama vyote na kelele tu
huyo mtu anakuwa mgombea binafsi au??
unajichanganya changanya tu!!
 
Mgombea wa ubunge kwa tiketi ya CHADEMA Igunga alitumia dakika 20 katika moja ya kampeni zake nilizohudhuria kueleza kuwa CUF ni CCM-B. Kwa muda wote huo nilikuwa nasubiri kusikia jinsi atavyotatua matatizo ya wanaigunga (maji, kilimo, elimu n.k) pale akichaguliwa kuwa mbunge. Kwa bahati mbaya uvumilivu wangu ulikwisha baada ya dakika 20, kwani alikuwa ameganda kwenye topic moja "CUF ni CCM-B". Ukweli niliondoka kimya kimya, sijui kama baadae alizungumzia matatizo yanayowakabili wananchi wa Igunga na ufumbuzi wake. sidhani!

Alipokuja Tindu Lisu (mbunge-CHADEMA) Katika kampeni hizo nilikuwa na hamu sana ya kumsikiliza kwani nimemsoma katika magazeti tu. Huyu alitumia dakika 30 kueleza kuwa CUF ni CCM-B. Ilipofikia dakika ya 30 niliondoka kistaarabu bila kumwabia yeyote yule hata rafiki yangu niliyekuja naye pale.

Katika uchaguzi mkuu 2015, eti hiyo ndio 'KARATA DUME' wanayoitegemea kuieleza Tanzania nzima. Inawezekanaje kuingia IKULU kwa kuwaeleza wananchi milioni 30 kuwa CUF ni CCM- B.

Wananchi wanataka kujua ni jinsi gani CHADEMA MNA dawa ya kuondoa matatizo yao yanayowakabili kila siku? Umasikini, elimu, matibabu, miundo mbinu, kilimo duni njaa n.k

Kwa mtindo wa kampeni hizo ninahakikisha kuwa Tanzania hatuna vyama vya upinzani, na hasa CHADEMA ndio bure kabisa. Najuta kwenda kwenye kampeni zao, huwezi kujifunza lolote lile.
Wewe mwenyewe umetaja CFF ni CCM-B mara ngapi hapo juu???

Hebu tukumbushe CUF walipata kura ngapi kule Igunga.
 
Usichague chama wewe chagua "mgombea" kwa uwezo wake..

Mimi nimeshaacha mambo ya chama naangalia "uwezo wa mgombea" period

Vyama vyote na kelele tu

Hiyo ni mpya, nafikiri sasa hivi nianze kampeni ya kuwaelewesha watanzania kuchagua mtu na sio chama. Lakini kuna wanaoamini kuwa ukiwa umezungukwa katika CHAMA na akina Chako changu na changu ni changu, hata ukiwa mzuri namna gani hutaweza kuongoza nchi vizuri.

Kwa hiyo naomba unishawishi ni vipi unaweza kuondoa ufisadi ikiwa wewe ni mgombea wa CCM? Nauliza hivi kwa nimekutana na watu wsemao kuwa hata ukiwa kiongozi mzuri maadam umechaguliwa kwa tiketi ya CCM huwezi kuondoa rushwa. Nawe wasema vinginevy, hebu nipashe.
 
Wewe mwenyewe umetaja CFF ni CCM-B mara ngapi hapo juu???

Hebu tukumbushe CUF walipata kura ngapi kule Igunga.

Sizungumzii CUF, NAzungumzia CHADEMA NA KAMPENI ZAKE. Shauku yangu si kura ngapi walipata CHADEMA, bali ni ufinyu wa kampeni zao.
 
Bado tu mnaweweseka na Igunga? Kazi iliyokuwepo kule mnaitambua, ukichanganya na damu mliyoimwaga kumpa kafumu msalaba wa ubunge itachukua mda kuacha kuweweseka.
 
swala si nini CDM/CUF itawafanyia nini. Ahadi na porojo za uchaguzi CCM imeshaahidi ahadi nyingi ambazo hata hazitatekelezwa. jK anaahadi ngapi?
Basi elewa watu wameshachoka na ahadi wanaangalia mtu na chama haitaji uende chuo kikuu kulitambua hilo.
 
Wewe mwenyewe umetaja CFF ni CCM-B mara ngapi hapo juu???

Hebu tukumbushe CUF walipata kura ngapi kule Igunga.

Na wewe unaweza kutukumbusha magamba walipata kura ngapi????hebu acheni upinzani wa kijinga ndani ya upinzani,haiwezekani watu wooooote wasiokua magamba wakawa chadema na kama ambavyo ilivyo ni ngumu kwa watu wote wasiokuwa magamba kuwa cuf,huo ndio ukweli na hiyo ndio demokrasia duniani kote iko hivyo!sasa nini cha kufanya hapa ili kuwazidi magamba ujanja wao,vyama vyote vya upinzani viungane,cuf na chadema waliwahi kuonyesha mfano wa kuungana na kusimamisha mgombea mmoja wa urais na pia kuachiana majimbo,lakini sijui wameingiwa na wazimu gani sijui eti ndio wamekuwa wapinzani ndani ya upinzani!!!sidhani kama kweli wote wana nia thabiti ya kuwaondoa magamba madarakani...hali hii iko kwa viongozi mpaka kwenu nyie humu ndani mnaojifanya wakereketwa uchwara wa chadema na vyama vingine vya upinzani,mnashambuliana wenyewe kwa wenyewe!!!
 
Pole sana kwa yaliyokukuta, achana na mikutano yao, hawana sera zaidi ni taarabu tu i.e majungu.
 
Mtoa mada acha uongo. Propaganda za kijinga unamhadithia nani? Hivi watu ZAIDI ya 23000 waliopigia kura CDM unadhani waliichagua kwa ajili gani? Kwa taarifa yako muda wa kudanganya watu haupo tena. Lengo lazima magamba wang'oke 2015. Ebu tazama ulivyojichanganya kwenye post yako "baada ya dak 20 niliondoka. Je ulimsikieje Lissu dak 30 wakati ulikuwa hupo?" Ndio nyie mliokuwa mkidanganya watu kuwa "mkichagua upinzani wataleta vita".
 
Mgombea wa ubunge kwa tiketi ya CHADEMA Igunga alitumia dakika 20 katika moja ya kampeni zake nilizohudhuria kueleza kuwa CUF ni CCM-B. Kwa muda wote huo nilikuwa nasubiri kusikia jinsi atavyotatua matatizo ya wanaigunga (maji, kilimo, elimu n.k) pale akichaguliwa kuwa mbunge. Kwa bahati mbaya uvumilivu wangu ulikwisha baada ya dakika 20, kwani alikuwa ameganda kwenye topic moja "CUF ni CCM-B". Ukweli niliondoka kimya kimya, sijui kama baadae alizungumzia matatizo yanayowakabili wananchi wa Igunga na ufumbuzi wake. sidhani!

Alipokuja Tindu Lisu (mbunge-CHADEMA) Katika kampeni hizo nilikuwa na hamu sana ya kumsikiliza kwani nimemsoma katika magazeti tu. Huyu alitumia dakika 30 kueleza kuwa CUF ni CCM-B. Ilipofikia dakika ya 30 niliondoka kistaarabu bila kumwabia yeyote yule hata rafiki yangu niliyekuja naye pale.

Katika uchaguzi mkuu 2015, eti hiyo ndio 'KARATA DUME' wanayoitegemea kuieleza Tanzania nzima. Inawezekanaje kuingia IKULU kwa kuwaeleza wananchi milioni 30 kuwa CUF ni CCM- B.

Wananchi wanataka kujua ni jinsi gani CHADEMA MNA dawa ya kuondoa matatizo yao yanayowakabili kila siku? Umasikini, elimu, matibabu, miundo mbinu, kilimo duni njaa n.k

Kwa mtindo wa kampeni hizo ninahakikisha kuwa Tanzania hatuna vyama vya upinzani, na hasa CHADEMA ndio bure kabisa. Najuta kwenda kwenye kampeni zao, huwezi kujifunza lolote lile.

Kwa kuwa uwezo wako wa kufikiri ni mdogo, acha nikusaidie kureason ni kwa nini zilitumiwa dkk 20 kuiponda CUF. CUF ilikuwa ikijinadi kuwa yenyewe pia ni chama pinzani. Katika mazingira kama Tz, maendeleo ya watu yamezuiwa na mfumo mbovu pamoja na sera zisozotekelezwa za CCM. Hatua ya kwanza ya kutatua kero ya wananchi ni kuwafungua macho kwa kuwaeleza mabaya na maovu ya ccm. Sasa kwa kuwa lengo ni kuleta maendeleo kwa kuindoa ccm madarakani, ni vizuri na sahihi kuilezea uma ni jinsi gani na kivipi cuf ni ccm b. Upo? Tumia akili kufikiri, usitumie masaburi!
 
Mleta mdaa nazani umekuja kishabiki kwanini nakwambia ivi?ebu tujuze aadi ambazo cuf walizitoa igunga zaidi ya kuiponda cdm kwamba imekuja kugawa kura za upinzani.pia ivi unajua sababu zilizosababisha cuf kuitwa ccmb?na je ulishawai kujiuliza ni kwanini chama kinapokubalika kwa wakati fulani apa tanzania huweza kuundiwa zengwe ili kiweze kudhoofishwa?
 
Wazo la leo: kuing'oa ccm CDM inabidi isimame peke yake na kisiungane na chama chochote cha upinzani. Vyama vingine ni CCM B, CCM C, CCM........J. Msilogwe mkadanganywa hata kwa lugha gani kuungana. Hata hivyo kuna ushirika gani kati ya sera za CDM na vyama vingine? Kila chama kina sera yake. Mkitaka kuungana, ili muungano uonekane wa dhati inabidi kila chama kukana sera zake na kuanza sera mpya. Je hii inawezekana? CDM songa mbele ushindi ni dhahiri 2015. Isipokuwa anzeni kuandaa watu kuanzia sasa.
 
Wazo la leo: kuing'oa ccm CDM inabidi isimame peke yake na kisiungane na chama chochote cha upinzani. Vyama vingine ni CCM B, CCM C, CCM........J. Msilogwe mkadanganywa hata kwa lugha gani kuungana. Hata hivyo kuna ushirika gani kati ya sera za CDM na vyama vingine? Kila chama kina sera yake. Mkitaka kuungana, ili muungano uonekane wa dhati inabidi kila chama kukana sera zake na kuanza sera mpya. Je hii inawezekana? CDM songa mbele ushindi ni dhahiri 2015. Isipokuwa anzeni kuandaa watu kuanzia sasa.

Ccm ndo sana inafurahi kuona upinzani kutofautiana ukweli tofauti hizi za kupeana majina ya ccm b hazina faida
 
Back
Top Bottom