Zawadi Ngoda
JF-Expert Member
- Aug 13, 2009
- 3,796
- 1,849
Mgombea wa ubunge kwa tiketi ya CHADEMA Igunga alitumia dakika 20 katika moja ya kampeni zake nilizohudhuria kueleza kuwa CUF ni CCM-B. Kwa muda wote huo nilikuwa nasubiri kusikia jinsi atavyotatua matatizo ya wanaigunga (maji, kilimo, elimu n.k) pale akichaguliwa kuwa mbunge. Kwa bahati mbaya uvumilivu wangu ulikwisha baada ya dakika 20, kwani alikuwa ameganda kwenye topic moja "CUF ni CCM-B". Ukweli niliondoka kimya kimya, sijui kama baadae alizungumzia matatizo yanayowakabili wananchi wa Igunga na ufumbuzi wake. sidhani!
Alipokuja Tindu Lisu (mbunge-CHADEMA) Katika kampeni hizo nilikuwa na hamu sana ya kumsikiliza kwani nimemsoma katika magazeti tu. Huyu alitumia dakika 30 kueleza kuwa CUF ni CCM-B. Ilipofikia dakika ya 30 niliondoka kistaarabu bila kumwabia yeyote yule hata rafiki yangu niliyekuja naye pale.
Katika uchaguzi mkuu 2015, eti hiyo ndio 'KARATA DUME' wanayoitegemea kuieleza Tanzania nzima. Inawezekanaje kuingia IKULU kwa kuwaeleza wananchi milioni 30 kuwa CUF ni CCM- B.
Wananchi wanataka kujua ni jinsi gani CHADEMA MNA dawa ya kuondoa matatizo yao yanayowakabili kila siku? Umasikini, elimu, matibabu, miundo mbinu, kilimo duni njaa n.k
Kwa mtindo wa kampeni hizo ninahakikisha kuwa Tanzania hatuna vyama vya upinzani, na hasa CHADEMA ndio bure kabisa. Najuta kwenda kwenye kampeni zao, huwezi kujifunza lolote lile.
Alipokuja Tindu Lisu (mbunge-CHADEMA) Katika kampeni hizo nilikuwa na hamu sana ya kumsikiliza kwani nimemsoma katika magazeti tu. Huyu alitumia dakika 30 kueleza kuwa CUF ni CCM-B. Ilipofikia dakika ya 30 niliondoka kistaarabu bila kumwabia yeyote yule hata rafiki yangu niliyekuja naye pale.
Katika uchaguzi mkuu 2015, eti hiyo ndio 'KARATA DUME' wanayoitegemea kuieleza Tanzania nzima. Inawezekanaje kuingia IKULU kwa kuwaeleza wananchi milioni 30 kuwa CUF ni CCM- B.
Wananchi wanataka kujua ni jinsi gani CHADEMA MNA dawa ya kuondoa matatizo yao yanayowakabili kila siku? Umasikini, elimu, matibabu, miundo mbinu, kilimo duni njaa n.k
Kwa mtindo wa kampeni hizo ninahakikisha kuwa Tanzania hatuna vyama vya upinzani, na hasa CHADEMA ndio bure kabisa. Najuta kwenda kwenye kampeni zao, huwezi kujifunza lolote lile.