Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
HATUA ya Mwenyekiti wa makampuni ya IPP, Reginald Mengi, kutaja hadharani majina ya baadhi ya wafanyabiashara na mwanasiasa mmoja kuwa ni mafisadi papa imeonekana dhahiri kuligawa taifa katika makundi mawili yaliyoanza kujengeana chuki.
Makundi hayo ambayo yako ndani na nje ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), serikalini na nje ya chama hicho tawala ni yale ambayo ama yanamuunga mkono au kumpinga.
Miongoni mwa watu ambao wameshaonyesha kuguswa na hoja hiyo na kuitolea kauli ama za kuonyesha msimamo wao, au wakishikwa na kigugumizi cha kuisemea kwa ujasiri ni pamoja na Rais Jakaya Kikwete, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Simba Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, George Mkuchika na Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba.
Mbali ya hao, wengine ambao nao wameweka mguu katika hoja hiyo ni wabunge, Dk. Wilibrod Slaa (CHADEMA), Anne Kilango (CCM), Christopher ole Sendeka na wanasiasa wengine kutoka makundi tofauti ya kisiasa....!
_______________________
Je wanamageuzi wa Tanzania ambao kwa pamoja tunashiriki katika kuushawishi umma wa KiTanzania uachane na siasa za CCM na kuelekea kwenye mageuzi makubwa ya kiutawala ,inakuwajekuwaje tunafikishwa katika hitimisho la aina hii ,kuwa tumegawanyika kwa maana sote ni wafuasi wa Sultani CCM ila tunafanya kazi nyuma ya pazia.
Kwa maana Vyama vya upinzani navyo vinaonyeshwa kuwa vimejibanza katika kambi za CCM ,kwa jinsi habari hiyo hapo juu ,mwananchi wa kawaida akiona na kusoma habari hii ,kusema kweli itamvunja moyo kabisa na kuona kuwa kumbe hata wakuu nao ni washangiliaji na wanakingia kifua upande mmoja kati ya pande za CCM.
Napenda kutoa onyo kwa wakuu wa Vyama vya Upinzani kama walivyoainishwa hapo juu ,CUF (Lipumba) ,CHADEMA (W.Slaa) ,kuwa wakae mbali na kuacha kuwakumbatia waliotapakaa mavi (Machafu) ,wasiwakaribie wala wasiwatetee kwa kutoa maelezo ambayo yatawaonyesha wapo upande fulani ,hilo ni kosa katika siasa za upinzani dhidi ya chama tawala ,tena ni kosa kubwa sana ,linaweza kuhatarisha msimamo wa Chama dhidi ya serikali tawala.
Mambo haya ya ufisadi yanayotokea ndani ya Chama Tawala ni turufu kubwa sana inayohitaji kutunzwa na kuenziwa kwa hali na mali ,isipotezwe kwa maana hiyo ni faida kwa upande wa upinzani.
Ikiwa utagongana na waandishi habari ambao huwa na mitego yao na lengo lao ,mara nyingi kuwadai viongozi wetu wakuu ,kuwa msimamo wao upo wapi kutokana na madai ya fisadi huyu dhidi ya fisadi yule au yaliyosemwa nao ,hili ni suala mtego ambalo namna watakavyoliandika na kulifanyia usanii ni kama tuonavyo hapo juu.
Upinzani ni kuponda tu mpaka kieleweke na si kujibamiza katika kambi yeyote ile ya Chama tawala ,mafisadi hawa wanatafuta huruma ya wananchi na kwa hivyo hujaribu kila njia ikiwemo kuwahusisha viongozi wakuu wa Vyama vya upinzani na kinachotokea ni wafuasi wa vyama pinzani kusapoti wakuu wao na hapo kupata mlegezo kwa kiasi fulani kwa hawa mafisadi maana imani inayojengwa na kiongozi mkuu inamuokoa mmoja na kumzamisha mwengine na hivyo hata wale wananchi wenye moyo mwepesi inakuwa ni rahisi kuona kuwa fulani amesemwa ni msafi na mwengine ni fisadi.
Hilo halitakiwi kabisa hawa wananchi wanaotoka kwa mfano huko Tabora inakuwa wameshapata sababu kuwa hata fulani kasema kweli ,itakuwa tumekosa tunalolikusudia katika kuwagaragiza wafuasi wa sultani CCM mbele ya macho ya wananchi ,jamani tusichaguwe kama tunagandamiza basi iwe kwa wote mkubwa kwa mdogo ni kuwachanganya tu kwenye kapu moja hakuna msalie mtume. Wameoza wote hakuna nyangumi wala papa.
Kama tulikuwa tunasema Serikali ya Sultani CCM inakamata dagaa ni kuiambia kazi bado hatutaki madagaa peke yao ,kuna wengine ,ikikamata mapapa tunasema itazame nyavu yako imetoboka kuna manyangumi wamechana na kuirarua na sasa wanapeta wakamate na hao ni kuiweka serikali katika hali bize na ngumu ,na si kuwapa nafasi kuwa wamefanya vyema ,Serikali iliyoko madarakani haitakiwi hata sekunde moja kuonyeshwa kuwa imefanya wema ,ni kuiponda tu ,ndio nikasema hata kama imepeleka sindano za bindamu kwenye vijiji upinzani udai kumepelekwa sindano za kudungia ng'ombe ,lazima tuende opposite direction ,mi ningefurahi sana kama Lipumba na Slaa wangesema wote ni mafisadi ,kazi yao ingekuwa kwisha ,hakuna kujiuma uma na kuonyesha kubabaika ,huu utakuwa ni udhaifu kwa viongozi wetu hawa nani asiejua kuwa Mengi anaisaidia CCM ,nani asie jua kuwa Rostam anaisadia CCM ,viongozi wetu mmeshikwa na udhaifu gani hata kufika kujibambika upande mmoja ?
Tunataka Sultani CCM ajione hana pa kushika wafuasi wake wote wawe ni wenye kuangamizwa na kuunganishwa na ufisadi na si watenda haki ,jamani ndio pakawepo upinzani ,msifikiri upinzani ni lele mama na kulegezeana kamba ,hilo halipo ndipo mkamuona Seif Sharifu anatoka kipovu kwa kumkandia Kikwete ,si kama anataka sifa au aonekane shujaa hapana anaonyesha hisia za upinzani katika jukwaa la kisiasa na kutaka kuyazidi mawazo ya mwananchi wa kawaida na kumhamisha mwananchi katika mawazo ya Kikwete ni kiongozi bora au CCM ni Chama bora ,ni lazima umtaje mhusika kwa jina kabisa ikiwa kweli au si kweli na siasa inaruhusu hilo ,ndio ukasikia wengine wakijibu ni muongo ,hao ni CCM lakini ujumbe umeshafika na wananchi wanalainika kidogo kidogo ,kwa sababu unapozungumza inakuwa kama unapanda mbegu kwa msikilizaji na mvua za maneno ndizo zitakazoifanya mbegu ile ianze kuchipua na kuota na kushika kasi ,hivyo mbegu tunayoihitaji kupandwa ni kuwa CCM wote ni mafisadi hakuna aliebora ,vita vya wao kwa wao visitunafasishe kumtetea au kumkingia kifua mmoja wao ni kuwachanganya wote mbele ya macho ya wananchi.
Makundi hayo ambayo yako ndani na nje ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), serikalini na nje ya chama hicho tawala ni yale ambayo ama yanamuunga mkono au kumpinga.
Miongoni mwa watu ambao wameshaonyesha kuguswa na hoja hiyo na kuitolea kauli ama za kuonyesha msimamo wao, au wakishikwa na kigugumizi cha kuisemea kwa ujasiri ni pamoja na Rais Jakaya Kikwete, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Simba Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, George Mkuchika na Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba.
Mbali ya hao, wengine ambao nao wameweka mguu katika hoja hiyo ni wabunge, Dk. Wilibrod Slaa (CHADEMA), Anne Kilango (CCM), Christopher ole Sendeka na wanasiasa wengine kutoka makundi tofauti ya kisiasa....!
_______________________
Je wanamageuzi wa Tanzania ambao kwa pamoja tunashiriki katika kuushawishi umma wa KiTanzania uachane na siasa za CCM na kuelekea kwenye mageuzi makubwa ya kiutawala ,inakuwajekuwaje tunafikishwa katika hitimisho la aina hii ,kuwa tumegawanyika kwa maana sote ni wafuasi wa Sultani CCM ila tunafanya kazi nyuma ya pazia.
Kwa maana Vyama vya upinzani navyo vinaonyeshwa kuwa vimejibanza katika kambi za CCM ,kwa jinsi habari hiyo hapo juu ,mwananchi wa kawaida akiona na kusoma habari hii ,kusema kweli itamvunja moyo kabisa na kuona kuwa kumbe hata wakuu nao ni washangiliaji na wanakingia kifua upande mmoja kati ya pande za CCM.
Napenda kutoa onyo kwa wakuu wa Vyama vya Upinzani kama walivyoainishwa hapo juu ,CUF (Lipumba) ,CHADEMA (W.Slaa) ,kuwa wakae mbali na kuacha kuwakumbatia waliotapakaa mavi (Machafu) ,wasiwakaribie wala wasiwatetee kwa kutoa maelezo ambayo yatawaonyesha wapo upande fulani ,hilo ni kosa katika siasa za upinzani dhidi ya chama tawala ,tena ni kosa kubwa sana ,linaweza kuhatarisha msimamo wa Chama dhidi ya serikali tawala.
Mambo haya ya ufisadi yanayotokea ndani ya Chama Tawala ni turufu kubwa sana inayohitaji kutunzwa na kuenziwa kwa hali na mali ,isipotezwe kwa maana hiyo ni faida kwa upande wa upinzani.
Ikiwa utagongana na waandishi habari ambao huwa na mitego yao na lengo lao ,mara nyingi kuwadai viongozi wetu wakuu ,kuwa msimamo wao upo wapi kutokana na madai ya fisadi huyu dhidi ya fisadi yule au yaliyosemwa nao ,hili ni suala mtego ambalo namna watakavyoliandika na kulifanyia usanii ni kama tuonavyo hapo juu.
Upinzani ni kuponda tu mpaka kieleweke na si kujibamiza katika kambi yeyote ile ya Chama tawala ,mafisadi hawa wanatafuta huruma ya wananchi na kwa hivyo hujaribu kila njia ikiwemo kuwahusisha viongozi wakuu wa Vyama vya upinzani na kinachotokea ni wafuasi wa vyama pinzani kusapoti wakuu wao na hapo kupata mlegezo kwa kiasi fulani kwa hawa mafisadi maana imani inayojengwa na kiongozi mkuu inamuokoa mmoja na kumzamisha mwengine na hivyo hata wale wananchi wenye moyo mwepesi inakuwa ni rahisi kuona kuwa fulani amesemwa ni msafi na mwengine ni fisadi.
Hilo halitakiwi kabisa hawa wananchi wanaotoka kwa mfano huko Tabora inakuwa wameshapata sababu kuwa hata fulani kasema kweli ,itakuwa tumekosa tunalolikusudia katika kuwagaragiza wafuasi wa sultani CCM mbele ya macho ya wananchi ,jamani tusichaguwe kama tunagandamiza basi iwe kwa wote mkubwa kwa mdogo ni kuwachanganya tu kwenye kapu moja hakuna msalie mtume. Wameoza wote hakuna nyangumi wala papa.
Kama tulikuwa tunasema Serikali ya Sultani CCM inakamata dagaa ni kuiambia kazi bado hatutaki madagaa peke yao ,kuna wengine ,ikikamata mapapa tunasema itazame nyavu yako imetoboka kuna manyangumi wamechana na kuirarua na sasa wanapeta wakamate na hao ni kuiweka serikali katika hali bize na ngumu ,na si kuwapa nafasi kuwa wamefanya vyema ,Serikali iliyoko madarakani haitakiwi hata sekunde moja kuonyeshwa kuwa imefanya wema ,ni kuiponda tu ,ndio nikasema hata kama imepeleka sindano za bindamu kwenye vijiji upinzani udai kumepelekwa sindano za kudungia ng'ombe ,lazima tuende opposite direction ,mi ningefurahi sana kama Lipumba na Slaa wangesema wote ni mafisadi ,kazi yao ingekuwa kwisha ,hakuna kujiuma uma na kuonyesha kubabaika ,huu utakuwa ni udhaifu kwa viongozi wetu hawa nani asiejua kuwa Mengi anaisaidia CCM ,nani asie jua kuwa Rostam anaisadia CCM ,viongozi wetu mmeshikwa na udhaifu gani hata kufika kujibambika upande mmoja ?
Tunataka Sultani CCM ajione hana pa kushika wafuasi wake wote wawe ni wenye kuangamizwa na kuunganishwa na ufisadi na si watenda haki ,jamani ndio pakawepo upinzani ,msifikiri upinzani ni lele mama na kulegezeana kamba ,hilo halipo ndipo mkamuona Seif Sharifu anatoka kipovu kwa kumkandia Kikwete ,si kama anataka sifa au aonekane shujaa hapana anaonyesha hisia za upinzani katika jukwaa la kisiasa na kutaka kuyazidi mawazo ya mwananchi wa kawaida na kumhamisha mwananchi katika mawazo ya Kikwete ni kiongozi bora au CCM ni Chama bora ,ni lazima umtaje mhusika kwa jina kabisa ikiwa kweli au si kweli na siasa inaruhusu hilo ,ndio ukasikia wengine wakijibu ni muongo ,hao ni CCM lakini ujumbe umeshafika na wananchi wanalainika kidogo kidogo ,kwa sababu unapozungumza inakuwa kama unapanda mbegu kwa msikilizaji na mvua za maneno ndizo zitakazoifanya mbegu ile ianze kuchipua na kuota na kushika kasi ,hivyo mbegu tunayoihitaji kupandwa ni kuwa CCM wote ni mafisadi hakuna aliebora ,vita vya wao kwa wao visitunafasishe kumtetea au kumkingia kifua mmoja wao ni kuwachanganya wote mbele ya macho ya wananchi.
Last edited: