Siku hizi hakuna cha kustaajabisha kinachotoka kinywani mwa Mwenye nchi yake. Kilichonishangaza leo, ni roho iliniuma kwa niaba ya mamia ya vijana hapa nchini, ambao leo wameambiwa wazi kwa kila namna isipokuwa kwa maneno dhahiri, kuwa hapa nchini kuna anayetoa toa na kutwaa, anayepangia kiasi unachostahili kufikia katika maisha. Mjuaji wa yote. Mungu Mtu. Tuliotaharuki ile siku tuliposikia JINA LAKE LIHIMIDIWE, tulikuwa hatujaelewa somo.
Hivi mtu mwenye mapenzi mema anawezaje kuwaambia vijana wasiwe ambitious?
Kwamba ukiwa Mkurugenzi au Mkuu wa Mkoa, usijaribu kuwa na ndoto ya kuutaka Ubunge au Urais?
Utovu wa nidhamu wa viongozi walioambiwa wakajipe semina elekezi, na wanaoona wenzao wa kanda maalum wakikosa nidhamu ndo wanakingiwa kifua, ni ishu tofauti kabisa na kutishia watu wasijaribu kuota zaidi. Yeye huko kote alikopita alitatua matatizo yote?
Yeye mbona hakuridhika alipoteuliwa na wizara kuwa mwalimu huko Sengerema?
Kwahiyo Masauni, Mwinyi na Mbarawa ndo wasitegemee tena maisha kwenye siasa wakikosa urais Zanzibar?
Vijana wa nchi hii kwakweli wamepatwa.
Mwenyezi Mungu aliyeko mbinguni, awasimamie hiki kikombe nacho kipite. Leo nimethibitisha kwa masikio na macho yangu, kuwa NENO LINAISHI.
Mhubiri 4:3 BHN
Lakini ana heri zaidi kuliko wafu na walio hai, yule ambaye bado hajazaliwa na kuona maovu yote yanayotendwa hapa duniani.
Hivi mtu mwenye mapenzi mema anawezaje kuwaambia vijana wasiwe ambitious?
Kwamba ukiwa Mkurugenzi au Mkuu wa Mkoa, usijaribu kuwa na ndoto ya kuutaka Ubunge au Urais?
Utovu wa nidhamu wa viongozi walioambiwa wakajipe semina elekezi, na wanaoona wenzao wa kanda maalum wakikosa nidhamu ndo wanakingiwa kifua, ni ishu tofauti kabisa na kutishia watu wasijaribu kuota zaidi. Yeye huko kote alikopita alitatua matatizo yote?
Yeye mbona hakuridhika alipoteuliwa na wizara kuwa mwalimu huko Sengerema?
Kwahiyo Masauni, Mwinyi na Mbarawa ndo wasitegemee tena maisha kwenye siasa wakikosa urais Zanzibar?
Vijana wa nchi hii kwakweli wamepatwa.
Mwenyezi Mungu aliyeko mbinguni, awasimamie hiki kikombe nacho kipite. Leo nimethibitisha kwa masikio na macho yangu, kuwa NENO LINAISHI.
Mhubiri 4:3 BHN
Lakini ana heri zaidi kuliko wafu na walio hai, yule ambaye bado hajazaliwa na kuona maovu yote yanayotendwa hapa duniani.